< Psalms 68 >

1 For the Chief Musician. A Psalm by David. A song. Let God arise! Let his enemies be scattered! Let them who hate him also flee before him.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 As smoke is driven away, so drive them away. As wax melts before the fire, so let the wicked perish at the presence of God.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 But let the righteous be glad. Let them rejoice before God. Yes, let them rejoice with gladness.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Sing to God! Sing praises to his name! Extol him who rides on the clouds: to the LORD, his name! Rejoice before him!
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 A father of the fatherless, and a defender of the widows, is God in his holy habitation.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 God sets the lonely in families. He brings out the prisoners with singing, but the rebellious dwell in a sun-scorched land.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 God, when you went out before your people, when you marched through the wilderness... (Selah)
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 The earth trembled. The sky also poured down rain at the presence of the God of Sinai— at the presence of God, the God of Israel.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 You, God, sent a plentiful rain. You confirmed your inheritance when it was weary.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 Your congregation lived therein. You, God, prepared your goodness for the poor.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 The Lord announced the word. The ones who proclaim it are a great company.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 “Kings of armies flee! They flee!” She who waits at home divides the plunder,
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 while you sleep amongst the camp fires, the wings of a dove sheathed with silver, her feathers with shining gold.
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 When the Almighty scattered kings in her, it snowed on Zalmon.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 The mountains of Bashan are majestic mountains. The mountains of Bashan are rugged.
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 Why do you look in envy, you rugged mountains, at the mountain where God chooses to reign? Yes, the LORD will dwell there forever.
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 The chariots of God are tens of thousands and thousands of thousands. The Lord is amongst them, from Sinai, into the sanctuary.
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 You have ascended on high. You have led away captives. You have received gifts amongst people, yes, amongst the rebellious also, that the LORD God might dwell there.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 Blessed be the Lord, who daily bears our burdens, even the God who is our salvation. (Selah)
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 God is to us a God of deliverance. To GOD, the Lord, belongs escape from death.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 But God will strike through the head of his enemies, the hairy scalp of such a one as still continues in his guiltiness.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 The Lord said, “I will bring you again from Bashan, I will bring you again from the depths of the sea,
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 that you may crush them, dipping your foot in blood, that the tongues of your dogs may have their portion from your enemies.”
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 They have seen your processions, God, even the processions of my God, my King, into the sanctuary.
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 The singers went before, the minstrels followed after, amongst the ladies playing with tambourines,
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 “Bless God in the congregations, even the Lord in the assembly of Israel!”
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 There is little Benjamin, their ruler, the princes of Judah, their council, the princes of Zebulun, and the princes of Naphtali.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 Your God has commanded your strength. Strengthen, God, that which you have done for us.
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 Because of your temple at Jerusalem, kings shall bring presents to you.
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Rebuke the wild animal of the reeds, the multitude of the bulls with the calves of the peoples. Trample under foot the bars of silver. Scatter the nations who delight in war.
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Princes shall come out of Egypt. Ethiopia shall hurry to stretch out her hands to God.
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Sing to God, you kingdoms of the earth! Sing praises to the Lord— (Selah)
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 to him who rides on the heaven of heavens, which are of old; behold, he utters his voice, a mighty voice.
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 Ascribe strength to God! His excellency is over Israel, his strength is in the skies.
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 You are awesome, God, in your sanctuaries. The God of Israel gives strength and power to his people. Praise be to God!
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Psalms 68 >