< Psalms 22 >

1 For the Chief Musician; set to “The Doe of the Morning.” A Psalm by David. My God, my God, why have you forsaken me? Why are you so far from helping me, and from the words of my groaning?
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
2 My God, I cry in the daytime, but you don’t answer; in the night season, and am not silent.
Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
3 But you are holy, you who inhabit the praises of Israel.
Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
4 Our fathers trusted in you. They trusted, and you delivered them.
Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
5 They cried to you, and were delivered. They trusted in you, and were not disappointed.
Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
6 But I am a worm, and no man; a reproach of men, and despised by the people.
Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
7 All those who see me mock me. They insult me with their lips. They shake their heads, saying,
Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
8 “He trusts in the LORD. Let him deliver him. Let him rescue him, since he delights in him.”
Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
9 But you brought me out of the womb. You made me trust while at my mother’s breasts.
Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
10 I was thrown on you from my mother’s womb. You are my God since my mother bore me.
Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
11 Don’t be far from me, for trouble is near. For there is no one to help.
Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
12 Many bulls have surrounded me. Strong bulls of Bashan have encircled me.
Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
13 They open their mouths wide against me, lions tearing prey and roaring.
Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
14 I am poured out like water. All my bones are out of joint. My heart is like wax. It is melted within me.
Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
15 My strength is dried up like a potsherd. My tongue sticks to the roof of my mouth. You have brought me into the dust of death.
Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
16 For dogs have surrounded me. A company of evildoers have enclosed me. They have pierced my hands and feet.
Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 I can count all of my bones. They look and stare at me.
Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
18 They divide my garments amongst them. They cast lots for my clothing.
Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
19 But don’t be far off, LORD. You are my help. Hurry to help me!
Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
20 Deliver my soul from the sword, my precious life from the power of the dog.
Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
21 Save me from the lion’s mouth! Yes, you have rescued me from the horns of the wild oxen.
Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
22 I will declare your name to my brothers. Amongst the assembly, I will praise you.
Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
23 You who fear the LORD, praise him! All you descendants of Jacob, glorify him! Stand in awe of him, all you descendants of Israel!
Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
24 For he has not despised nor abhorred the affliction of the afflicted, neither has he hidden his face from him; but when he cried to him, he heard.
Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
25 My praise of you comes in the great assembly. I will pay my vows before those who fear him.
Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
26 The humble shall eat and be satisfied. They shall praise the LORD who seek after him. Let your hearts live forever.
Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
27 All the ends of the earth shall remember and turn to the LORD. All the relatives of the nations shall worship before you.
Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
28 For the kingdom is the LORD’s. He is the ruler over the nations.
kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
29 All the rich ones of the earth shall eat and worship. All those who go down to the dust shall bow before him, even he who can’t keep his soul alive.
Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
30 Posterity shall serve him. Future generations shall be told about the Lord.
Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
31 They shall come and shall declare his righteousness to a people that shall be born, for he has done it.
Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.

< Psalms 22 >