< Matthew 27 >

1 Now when morning had come, all the chief priests and the elders of the people took counsel against Yeshua to put him to death.
Muda wa asubuhi ulipofika, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua.
2 They bound him, led him away, and delivered him up to Pontius Pilate, the governor.
Walimfunga, walimwongoza, na kumfikisha kwa Liwali Pilato.
3 Then Judah, who betrayed him, when he saw that Yeshua was condemned, felt remorse, and brought back the thirty pieces of silver to the chief priests and elders,
Kisha wakati Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti, aliona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, alijuta na kurudisha vipande thelathini vya fedha kwa mkuu wa makuhani na wazee,
4 saying, “I have sinned in that I betrayed innocent blood.” But they said, “What is that to us? You see to it.”
na akasema, “Nimefanya dhambi kwa kuisaliti damu isiyo na hatia.” Lakini wakajibu, “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie hayo mwenyewe.”
5 He threw down the pieces of silver in the sanctuary and departed. Then he went away and hanged himself.
Kisha alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu, na kuondoka zake na kujinyonga mwenyewe.
6 The chief priests took the pieces of silver and said, “It’s not lawful to put them into the treasury, since it is the price of blood.”
Mkuu wa makuhani alivichukua vile vipande vya fedha na kusema, “Si halali kuiweka fedha hii katika hazina, kwa sababu ni gharama ya damu.”
7 They took counsel, and bought the potter’s field with them to bury strangers in.
Walijadiliana kwa pamoja na fedha ikatumika kununulia shamba la mfinyazi la kuzika wageni.
8 Therefore that field has been called “The Field of Blood” to this day.
Kwa sababu hii shamba hilo limekuwa likiitwa, “Shamba la damu” hadi leo hii.
9 Then that which was spoken through Jeremiah the prophet was fulfilled, saying, “They took the thirty pieces of silver, the price of him upon whom a price had been set, whom some of the children of Israel priced,
Kisha lile neno lililokuwa limenenwa na nabii Yeremia lilitimia, kusema, “Walitwaa vipande thelathini vya fedha, gharama iliyopangwa na watu wa Israel kwa ajili yake,
10 and they gave them for the potter’s field, as the Lord commanded me.”
na waliitumia kwa shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyokuwa amenielekeza.”
11 Now Yeshua stood before the governor; and the governor asked him, saying, “Are you the King of the Jews?” Yeshua said to him, “So you say.”
Sasa Yesu alisimama mbele ya liwali, na liwali akamwuliza, “Je! Wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu alimjibu, “Wewe wasema hivyo.”
12 When he was accused by the chief priests and elders, he answered nothing.
Lakini wakati aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu chochote.
13 Then Pilate said to him, “Don’t you hear how many things they testify against you?”
Kisha Pilato alimwambia, “Hujayasikia mashitaka yote dhidi yako?”
14 He gave him no answer, not even one word, so that the governor marvelled greatly.
Lakini hakumjibu hata neno moja, hivyo liwali alijawa na mshangao.
15 Now at the feast the governor was accustomed to release to the multitude one prisoner whom they desired.
Sasa katika sikukuu ilikuwa desturi ya liwali kumfungua mfungwa mmoja anayechaguliwa na umati.
16 They had then a notable prisoner called Barabbas.
Wakati huo walikuwa na mfungwa sugu jina lake Baraba.
17 When therefore they were gathered together, Pilate said to them, “Whom do you want me to release to you? Barabbas, or Yeshua who is called Messiah?”
Hivyo wakati walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato aliwauliza, “Ni nani mnataka tumfungue kwa ajili yenu?” Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”
18 For he knew that because of envy they had delivered him up.
Kwa sababu alijua kwamba wamekwisha kumkamata kwa sababu ya chuki.
19 While he was sitting on the judgement seat, his wife sent to him, saying, “Have nothing to do with that righteous man, for I have suffered many things today in a dream because of him.”
Wakati alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha hukumu, mke wake alimtumia neno na kusema, “Usitende jambo lolote kwa mtu huyo asiye na hatia. Kwani nimeteswa mno hata leo katika ndoto kwa sababu yake.”
20 Now the chief priests and the elders persuaded the multitudes to ask for Barabbas and destroy Yeshua.
Ndipo wakuu wa makuhani na wazee waliwashawishi makutano wamwombe Baraba, na Yesu auawe.
21 But the governor answered them, “Which of the two do you want me to release to you?” They said, “Barabbas!”
Liwali aliwauliza, “Ni yupi kati ya wawili mnataka mimi nimwachie kwenu?” Walisema, “Baraba.”
22 Pilate said to them, “What then shall I do to Yeshua who is called Messiah?” They all said to him, “Let him be crucified!”
Pilato akawaambia, “Nimtendee nini Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakajibu, “Msulibishe”
23 But the governor said, “Why? What evil has he done?” But they cried out exceedingly, saying, “Let him be crucified!”
Naye akasema, “Kwa nini, ni kosa gani ametenda?” Lakini walizidi kupaza sauti hata juu mno, “Msulibishe.”
24 So when Pilate saw that nothing was being gained, but rather that a disturbance was starting, he took water and washed his hands before the multitude, saying, “I am innocent of the blood of this righteous person. You see to it.”
Hivyo wakati Pilato alipoona hawezi kufanya lolote, lakini badala yake vurugu zilikuwa zimeanza, alitwaa maji akanawa mikono yake mbele ya umati, na kusema, “Mimi sina hatia juu ya damu ya mtu huyu asiye na hatia. Yaangalieni haya wenyewe.”
25 All the people answered, “May his blood be on us and on our children!”
Watu wote wakasema, “Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu.”
26 Then he released Barabbas to them, but Yeshua he flogged and delivered to be crucified.
Kisha akamfungulia Baraba kwao, lakini alimpiga mijeredi Yesu na kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa.
27 Then the governor’s soldiers took Yeshua into the Praetorium, and gathered the whole garrison together against him.
Kisha askari wa liwali wakamchukua Yesu mpaka Praitorio na kundi kubwa la maaskari wote wakamkusanyika.
28 They stripped him and put a scarlet robe on him.
Wakamvua nguo zake na kumvika kanzu ya rangi nyekundu.
29 They braided a crown of thorns and put it on his head, and a reed in his right hand; and they knelt down before him and mocked him, saying, “Hail, King of the Jews!”
Kisha wakatengeneza taji ya miiba na kuiweka juu ya kichwa chake, na walimwekea mwanzi katika mkono wake wa kuume. Walipiga magoti mbele yake na kumkejeri, wakisema, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi?”
30 They spat on him, and took the reed and struck him on the head.
Na walimtemea mate, na walitwaa mwanzi na kumpiga kichwani.
31 When they had mocked him, they took the robe off him, and put his clothes on him, and led him away to crucify him.
Wakati walipokuwa wakimkejeri, walimvua ile kanzu na kumvika nguo zake, na kumwongoza kwenda kumsulibisha.
32 As they came out, they found a man of Cyrene, Simon by name, and they compelled him to go with them, that he might carry his cross.
Walipotoka nje, walimwona mtu kutoka Krene jina lake Simeoni, ambaye walimlazimisha kwenda nao ili apate kuubeba msalaba wake.
33 When they came to a place called “Golgotha”, that is to say, “The place of a skull,”
Walipofika mahali paitwapo Galigotha, maana yake, “Eneo la fuvu la Kichwa.”
34 they gave him sour wine to drink mixed with gall. When he had tasted it, he would not drink.
Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo anywe. Lakini alipoionja, hakuweza kuinywa.
35 When they had crucified him, they divided his clothing amongst them, casting lots,
Wakati walipokuwa wamemsulibisha, waligawana mavazi yake kwa kupiga kura.
36 and they sat and watched him there.
Na waliketi na kumwangalia.
37 They set up over his head the accusation against him written, “THIS IS YESHUA, THE KING OF THE JEWS.”
Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake yakisomeka, “Huyu ni Yesu, mfalme wa Wayahudi.”
38 Then there were two robbers crucified with him, one on his right hand and one on the left.
Wanyang'anyi wawili walisulibiwa pamoja naye, mmoja upande wa kulia wake na mwingine wa kushoto.
39 Those who passed by blasphemed him, wagging their heads
Wale waliokuwa wakipita walimdhihaki, wakitikisa vichwa vyao
40 and saying, “You who destroy the temple and build it in three days, save yourself! If you are the Son of God, come down from the cross!”
na kusema, “Wewe uliyekuwa unataka kuliharibu hekalu na kulijenga katika siku tatu, jiokoe mwenyewe! Kama ni Mwana wa Mungu, shuka chini utoke msalabani!”
41 Likewise the chief priests also mocking with the scribes, the Pharisees, and the elders, said,
Katika hali ile ile wakuu wa makuhani walikuwa wakimkashifu, pamoja na waandishi na wazee, na kusema,
42 “He saved others, but he can’t save himself. If he is the King of Israel, let him come down from the cross now, and we will believe in him.
“Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi. Na ashuke chini toka msalabani, ndipo tutakapomwamini.
43 He trusts in God. Let God deliver him now, if he wants him; for he said, ‘I am the Son of God.’”
Alimtumaini Mungu. Acha Mungu amwokoe sasa kama anataka, kwa sababu alisema, 'Mimi ni Mwana wa Mungu.'”
44 The robbers also who were crucified with him cast on him the same reproach.
Na wale wanyang'anyi waliokuwa wamesulibiwa pamoja naye pia walisema maneno ya kumdhihaki.
45 Now from the sixth hour there was darkness over all the land until the ninth hour.
Sasa kutoka saa sita kulikuwa na giza katika nchi yote hadi saa tisa.
46 About the ninth hour Yeshua cried with a loud voice, saying, “Eli, Eli, lima sabachthani?” That is, “My God, my God, why have you forsaken me?”
Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama thabakithan?” akimaanisha, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
47 Some of them who stood there, when they heard it, said, “This man is calling Elijah.”
Wakati huo baadhi yao waliokuwa wamesimama pale walisikia, wakasema, “Anamwita Eliya.”
48 Immediately one of them ran and took a sponge, filled it with vinegar, put it on a reed, and gave him a drink.
Mara moja mmoja wao alikimbia kuchukua sifongo na kuijaza kinywaji kichungu, akaiweka juu ya mti na kumpa apate kunywa.
49 The rest said, “Let him be. Let’s see whether Elijah comes to save him.”
Nao waliosalia wakasema, “Mwacheni peke yake, acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
50 Yeshua cried again with a loud voice, and yielded up his spirit.
Kisha Yesu akalia tena kwa sauti kuu na akaitoa roho yake.
51 Behold, the veil of the temple was torn in two from the top to the bottom. The earth quaked and the rocks were split.
Tazama, Pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutokea juu hadi chini. Na ardhi ikatetemeka na miamba ikapasuka vipande.
52 The tombs were opened, and many bodies of the holy ones who had fallen asleep were raised;
Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.
53 and coming out of the tombs after his resurrection, they entered into the holy city and appeared to many.
Walitoka kwenye makaburi baada ya ufufuo wake, waliingia mji mtakatifu, na wakaonekana na wengi.
54 Now the centurion and those who were with him watching Yeshua, when they saw the earthquake and the things that were done, were terrified, saying, “Truly this was the Son of God!”
Basi yule akida na wale ambao walikuwa wakimtazama Yesu waliona tetemeko na mambo yaliyokuwa yakitokea, walijawa na woga sana na kusema, “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
55 Many women were there watching from afar, who had followed Yeshua from Galilee, serving him.
Wanawake wengi waliokuwa wakimfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa pale wakitazama kutoka kwa mbali.
56 Amongst them were Miriam Magdalene, Miriam the mother of Jacob and Yosi, and the mother of the sons of Zebedee.
Miongini mwao walikuwa Mariamu Magdarena, Mariamu mama yake Yakobo na Joseph, na mama wa watoto wa Zebedayo
57 When evening had come, a rich man from Arimathaea named Joseph, who himself was also Yeshua’s disciple, came.
Ilipofika jioni, alikuja mtu tajiri kutoka Arimathayo, aliyeitwa Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58 This man went to Pilate and asked for Yeshua’s body. Then Pilate commanded the body to be given up.
Alimwendea Pilato na kuuomba mwili wa Yesu. Kisha Pilato aliagiza apate kupewa.
59 Joseph took the body and wrapped it in a clean linen cloth
Yusufu aliuchukua mwili akaufunga na nguo ya sufi safi,
60 and laid it in his own new tomb, which he had cut out in the rock. Then he rolled a large stone against the door of the tomb, and departed.
na akaulaza katika kaburi jipya lake alilokuwa amelichonga mwambani. Kisha akavingirisha jiwe kubwa likafunika mlango wa kaburi na akaenda zake.
61 Miriam Magdalene was there, and the other Miriam, sitting opposite the tomb.
Mariamu Magdalena na Mariamu mwingine walikuwa pale, wamekaa kuelekea kaburi.
62 Now on the next day, which was the day after the Preparation Day, the chief priests and the Pharisees were gathered together to Pilate,
Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku baada ya maandalio, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja kwa Pilato.
63 saying, “Sir, we remember what that deceiver said while he was still alive: ‘After three days I will rise again.’
Wakamwambia, “Bwana, tunakumbuka kuwa wakati yule mdanganyifu alipokuwa hai, alisema, 'Baada ya siku tatu atafufuka tena.'
64 Command therefore that the tomb be made secure until the third day, lest perhaps his disciples come at night and steal him away, and tell the people, ‘He is risen from the dead;’ and the last deception will be worse than the first.”
Kwahiyo, agiza kwamba kaburi lilindwe salama mpaka siku ya tatu. Vinginevyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kumwiba na kusema kwa watu, 'Amefufuka kutoka wafu.' Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
65 Pilate said to them, “You have a guard. Go, make it as secure as you can.”
Pilato akawaambia, “Chukueni walinzi. Nendeni mkafanye hali ya usalama kama muwezavyo.”
66 So they went with the guard and made the tomb secure, sealing the stone.
Hivyo walikwenda na kufanya kaburi kuwa salama, jiwe liligongwa mhuri na kuweka walinzi.

< Matthew 27 >