< Job 37 >

1 “Yes, at this my heart trembles, and is moved out of its place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Hear, oh, hear the noise of his voice, the sound that goes out of his mouth.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 He sends it out under the whole sky, and his lightning to the ends of the earth.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 After it a voice roars. He thunders with the voice of his majesty. He doesn’t hold back anything when his voice is heard.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 God thunders marvellously with his voice. He does great things, which we can’t comprehend.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 For he says to the snow, ‘Fall on the earth,’ likewise to the shower of rain, and to the showers of his mighty rain.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 He seals up the hand of every man, that all men whom he has made may know it.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Then the animals take cover, and remain in their dens.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Out of its room comes the storm, and cold out of the north.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 By the breath of God, ice is given, and the width of the waters is frozen.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Yes, he loads the thick cloud with moisture. He spreads abroad the cloud of his lightning.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 It is turned around by his guidance, that they may do whatever he commands them on the surface of the habitable world,
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 whether it is for correction, or for his land, or for loving kindness, that he causes it to come.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 “Listen to this, Job. Stand still, and consider the wondrous works of God.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Do you know how God controls them, and causes the lightning of his cloud to shine?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Do you know the workings of the clouds, the wondrous works of him who is perfect in knowledge?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 You whose clothing is warm when the earth is still by reason of the south wind?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Can you, with him, spread out the sky, which is strong as a cast metal mirror?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Teach us what we will tell him, for we can’t make our case by reason of darkness.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Will it be told him that I would speak? Or should a man wish that he were swallowed up?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Now men don’t see the light which is bright in the skies, but the wind passes, and clears them.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Out of the north comes golden splendour. With God is awesome majesty.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 We can’t reach the Almighty. He is exalted in power. In justice and great righteousness, he will not oppress.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Therefore men revere him. He doesn’t regard any who are wise of heart.”
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >