< Acts 2 >

1 Now when the day of Shavu`ot had come, they were all with one accord in one place.
Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
2 Suddenly there came from the sky a sound like the rushing of a mighty wind, and it filled all the house where they were sitting.
Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
3 Tongues like fire appeared and were distributed to them, and one sat on each of them.
Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
4 They were all filled with the Holy Spirit and began to speak with other languages, as the Spirit gave them the ability to speak.
Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
5 Now there were dwelling in Jerusalem Jews, devout men, from every nation under the sky.
Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu.
6 When this sound was heard, the multitude came together and were bewildered, because everyone heard them speaking in his own language.
Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 They were all amazed and marvelled, saying to one another, “Behold, aren’t all these who speak Galileans?
Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya?
8 How do we hear, everyone in our own native language?
Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa?
9 Parthians, Medes, Elamites, and people from Mesopotamia, Judea, Cappadocia, Pontus, Asia,
Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia,
10 Phrygia, Pamphylia, Egypt, the parts of Libya around Cyrene, visitors from Rome, both Jews and proselytes,
Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi,
11 Cretans and Arabians—we hear them speaking in our languages the mighty works of God!”
Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.”
12 They were all amazed and were perplexed, saying to one another, “What does this mean?”
Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”
13 Others, mocking, said, “They are filled with new wine.”
Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”
14 But Peter, standing up with the Eleven, lifted up his voice and spoke out to them, “You men of Judea and all you who dwell at Jerusalem, let this be known to you, and listen to my words.
Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize.
15 For these aren’t drunken, as you suppose, seeing it is only the third hour of the day.
Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi!
16 But this is what has been spoken through the prophet Joel:
La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
17 ‘It will be in the last days, says God, that I will pour out my Spirit on all flesh. Your sons and your daughters will prophesy. Your young men will see visions. Your old men will dream dreams.
“‘Katika siku za mwisho, asema Mungu, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18 Yes, and on my servants and on my handmaidens in those days, I will pour out my Spirit, and they will prophesy.
Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu, nao watatabiri.
19 I will show wonders in the sky above, and signs on the earth beneath: blood, and fire, and billows of smoke.
Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni, na ishara chini duniani: damu, moto, na mawimbi ya moshi.
20 The sun will be turned into darkness, and the moon into blood, before the great and glorious day of the Lord comes.
Jua litakuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana iliyo tukufu.
21 It will be that whoever will call on the name of the Lord will be saved.’
Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa.’
22 “Men of Israel, hear these words! Yeshua of Nazareth, a man approved by God to you by mighty works and wonders and signs which God did by him amongst you, even as you yourselves know,
“Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo.
23 him, being delivered up by the determined counsel and foreknowledge of God, you have taken by the hand of lawless men, crucified and killed;
Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani.
24 whom God raised up, having freed him from the agony of death, because it was not possible that he should be held by it.
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti.
25 For David says concerning him, ‘I saw the Lord always before my face, for he is on my right hand, that I should not be moved.
Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye: “‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
26 Therefore my heart was glad, and my tongue rejoiced. Moreover my flesh also will dwell in hope,
Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.
27 because you will not leave my soul in Sheol, neither will you allow your Holy One to see decay. (Hadēs g86)
Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs g86)
28 You made known to me the ways of life. You will make me full of gladness with your presence.’
Umenionyesha njia za uzima, utanijaza na furaha mbele zako.’
29 “Brothers, I may tell you freely of the patriarch David, that he both died and was buried, and his tomb is with us to this day.
“Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo.
30 Therefore, being a prophet, and knowing that God had sworn with an oath to him that of the fruit of his body, according to the flesh, he would raise up the Messiah to sit on his throne,
Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi.
31 he foreseeing this, spoke about the resurrection of the Messiah, that his soul wasn’t left in Sheol, and his flesh didn’t see decay. (Hadēs g86)
Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs g86)
32 This Yeshua God raised up, to which we all are witnesses.
Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.
33 Being therefore exalted by the right hand of God, and having received from the Father the promise of the Holy Spirit, he has poured out this which you now see and hear.
Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia.
34 For David didn’t ascend into the heavens, but he says himself, ‘The Lord said to my Lord, “Sit by my right hand
Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
35 until I make your enemies a footstool for your feet.”’
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
36 “Let all the house of Israel therefore know certainly that God has made him both Lord and Messiah, this Yeshua whom you crucified.”
“Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”
37 Now when they heard this, they were cut to the heart, and said to Peter and the rest of the emissaries, “Brothers, what shall we do?”
Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”
38 Peter said to them, “Repent and be immersed, every one of you, in the name of Yeshua the Messiah for the forgiveness of sins, and you will receive the gift of the Holy Spirit.
Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 For the promise is to you and to your children, and to all who are far off, even as many as the Lord our God will call to himself.”
Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”
40 With many other words he testified and exhorted them, saying, “Save yourselves from this crooked generation!”
Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.”
41 Then those who gladly received his word were immersed. There were added that day about three thousand souls.
Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.
42 They continued steadfastly in the emissaries’ teaching and fellowship, in the breaking of bread, and prayer.
Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali.
43 Fear came on every soul, and many wonders and signs were done through the emissaries.
Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume.
44 All who believed were together, and had all things in common.
Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika.
45 They sold their possessions and goods, and distributed them to all, according as anyone had need.
Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
46 Day by day, continuing steadfastly with one accord in the temple, and breaking bread at home, they took their food with gladness and singleness of heart,
Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe,
47 praising God and having favour with all the people. The Lord added to the assembly day by day those who were being saved.
wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.

< Acts 2 >