< Psalms 106 >

1 Praise Yahweh! Give thanks to Yahweh, for he is good, for his loving kindness endures forever.
Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Who can utter the mighty acts of Yahweh, or fully declare all his praise?
Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
3 Blessed are those who keep justice. Blessed is one who does what is right at all times.
Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
4 Remember me, Yahweh, with the favor that you show to your people. Visit me with your salvation,
Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
5 that I may see the prosperity of your chosen, that I may rejoice in the gladness of your nation, that I may glory with your inheritance.
Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
6 We have sinned with our fathers. We have committed iniquity. We have done wickedly.
Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
7 Our fathers didn’t understand your wonders in Egypt. They didn’t remember the multitude of your loving kindnesses, but were rebellious at the sea, even at the Red Sea.
Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
8 Nevertheless he saved them for his name’s sake, that he might make his mighty power known.
Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
9 He rebuked the Red Sea also, and it was dried up; so he led them through the depths, as through a desert.
Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
10 He saved them from the hand of him who hated them, and redeemed them from the hand of the enemy.
Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
11 The waters covered their adversaries. There was not one of them left.
Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
12 Then they believed his words. They sang his praise.
Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
13 They soon forgot his works. They didn’t wait for his counsel,
Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
14 but gave in to craving in the desert, and tested God in the wasteland.
Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
15 He gave them their request, but sent leanness into their soul.
Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
16 They envied Moses also in the camp, and Aaron, Yahweh’s saint.
Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
17 The earth opened and swallowed up Dathan, and covered the company of Abiram.
Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
18 A fire was kindled in their company. The flame burned up the wicked.
Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
19 They made a calf in Horeb, and worshiped a molten image.
Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
20 Thus they exchanged their glory for an image of a bull that eats grass.
Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
21 They forgot God, their Savior, who had done great things in Egypt,
Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
22 wondrous works in the land of Ham, and awesome things by the Red Sea.
Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
23 Therefore he said that he would destroy them, had Moses, his chosen, not stood before him in the breach, to turn away his wrath, so that he wouldn’t destroy them.
Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
24 Yes, they despised the pleasant land. They didn’t believe his word,
Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
25 but murmured in their tents, and didn’t listen to Yahweh’s voice.
bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
26 Therefore he swore to them that he would overthrow them in the wilderness,
Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
27 that he would overthrow their offspring among the nations, and scatter them in the lands.
akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
28 They joined themselves also to Baal Peor, and ate the sacrifices of the dead.
Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
29 Thus they provoked him to anger with their deeds. The plague broke in on them.
Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
30 Then Phinehas stood up and executed judgment, so the plague was stopped.
Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
31 That was credited to him for righteousness, for all generations to come.
Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
32 They angered him also at the waters of Meribah, so that Moses was troubled for their sakes;
Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
33 because they were rebellious against his spirit, he spoke rashly with his lips.
Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
34 They didn’t destroy the peoples, as Yahweh commanded them,
Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
35 but mixed themselves with the nations, and learned their works.
bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
36 They served their idols, which became a snare to them.
nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
37 Yes, they sacrificed their sons and their daughters to demons.
Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
38 They shed innocent blood, even the blood of their sons and of their daughters, whom they sacrificed to the idols of Canaan. The land was polluted with blood.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
39 Thus they were defiled with their works, and prostituted themselves in their deeds.
Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
40 Therefore Yahweh burned with anger against his people. He abhorred his inheritance.
Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
41 He gave them into the hand of the nations. Those who hated them ruled over them.
Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
42 Their enemies also oppressed them. They were brought into subjection under their hand.
Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
43 He rescued them many times, but they were rebellious in their counsel, and were brought low in their iniquity.
Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
44 Nevertheless he regarded their distress, when he heard their cry.
Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
45 He remembered for them his covenant, and repented according to the multitude of his loving kindnesses.
Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
46 He made them also to be pitied by all those who carried them captive.
Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
47 Save us, Yahweh, our God, gather us from among the nations, to give thanks to your holy name, to triumph in your praise!
Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
48 Blessed be Yahweh, the God of Israel, from everlasting even to everlasting! Let all the people say, “Amen.” Praise Yah!
Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.

< Psalms 106 >