< Matthew 14 >

1 At that time, Herod the tetrarch heard the report concerning Jesus,
Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.
2 and said to his servants, “This is John the Baptizer. He is risen from the dead. That is why these powers work in him.”
Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”
3 For Herod had arrested John, bound him, and put him in prison for the sake of Herodias, his brother Philip’s wife.
Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.
4 For John said to him, “It is not lawful for you to have her.”
Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”
5 When he would have put him to death, he feared the multitude, because they counted him as a prophet.
Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.
6 But when Herod’s birthday came, the daughter of Herodias danced among them and pleased Herod.
Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.
7 Therefore he promised with an oath to give her whatever she should ask.
Katika kujibu kili aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.
8 She, being prompted by her mother, said, “Give me here on a platter the head of John the Baptizer.”
Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
9 The king was grieved, but for the sake of his oaths and of those who sat at the table with him, he commanded it to be given,
Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.
10 and he sent and beheaded John in the prison.
Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani
11 His head was brought on a platter and given to the young lady; and she brought it to her mother.
ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.
12 His disciples came, took the body, and buried it. Then they went and told Jesus.
Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.
13 Now when Jesus heard this, he withdrew from there in a boat to a deserted place apart. When the multitudes heard it, they followed him on foot from the cities.
Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.
14 Jesus went out, and he saw a great multitude. He had compassion on them and healed their sick.
Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.
15 When evening had come, his disciples came to him, saying, “This place is deserted, and the hour is already late. Send the multitudes away, that they may go into the villages, and buy themselves food.”
Jioni ilipotimia, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.
16 But Jesus said to them, “They don’t need to go away. You give them something to eat.”
Lakini Yesu akawaambia, ''Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”
17 They told him, “We only have here five loaves and two fish.”
Wakamwambia, ''Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”''
18 He said, “Bring them here to me.”
Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”
19 He commanded the multitudes to sit down on the grass; and he took the five loaves and the two fish, and looking up to heaven, he blessed, broke and gave the loaves to the disciples; and the disciples gave to the multitudes.
Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini ya nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.
20 They all ate and were filled. They took up twelve baskets full of that which remained left over from the broken pieces.
Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.
21 Those who ate were about five thousand men, in addition to women and children.
Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.
22 Immediately Jesus made the disciples get into the boat and go ahead of him to the other side, while he sent the multitudes away.
Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.
23 After he had sent the multitudes away, he went up into the mountain by himself to pray. When evening had come, he was there alone.
Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.
24 But the boat was now in the middle of the sea, distressed by the waves, for the wind was contrary.
Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mpisho.
25 In the fourth watch of the night, Jesus came to them, walking on the sea.
Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.
26 When the disciples saw him walking on the sea, they were troubled, saying, “It’s a ghost!” and they cried out for fear.
Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,'' na kupaaza sauti katika hali ya uoga.
27 But immediately Jesus spoke to them, saying, “Cheer up! It is I! Don’t be afraid.”
Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! ni mimi! msiogope.”
28 Peter answered him and said, “Lord, if it is you, command me to come to you on the waters.”
Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.''
29 He said, “Come!” Peter stepped down from the boat and walked on the waters to come to Jesus.
Yesu akasema, “Njoo.'' Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.
30 But when he saw that the wind was strong, he was afraid, and beginning to sink, he cried out, saying, “Lord, save me!”
Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!''
31 Immediately Jesus stretched out his hand, took hold of him, and said to him, “You of little faith, why did you doubt?”
Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”
32 When they got up into the boat, the wind ceased.
Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulikoma kuvuma.
33 Those who were in the boat came and worshiped him, saying, “You are truly the Son of God!”
Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”
34 When they had crossed over, they came to the land of Gennesaret.
Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.
35 When the people of that place recognized him, they sent into all that surrounding region and brought to him all who were sick;
Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.
36 and they begged him that they might just touch the fringe of his garment. As many as touched it were made whole.
Walimsihi kwamba waweze kugusha pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.

< Matthew 14 >