< Job 36 >

1 Elihu also continued, and said,
Elihu aliendelea na kusema,
2 “Bear with me a little, and I will show you; for I still have something to say on God’s behalf.
“Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 I will get my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker.
Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
4 For truly my words are not false. One who is perfect in knowledge is with you.
Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
5 “Behold, God is mighty, and doesn’t despise anyone. He is mighty in strength of understanding.
Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
6 He doesn’t preserve the life of the wicked, but gives justice to the afflicted.
Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
7 He doesn’t withdraw his eyes from the righteous, but with kings on the throne, he sets them forever, and they are exalted.
Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
8 If they are bound in fetters, and are taken in the cords of afflictions,
Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
9 then he shows them their work, and their transgressions, that they have behaved themselves proudly.
kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
10 He also opens their ears to instruction, and commands that they return from iniquity.
Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
11 If they listen and serve him, they will spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
12 But if they don’t listen, they will perish by the sword; they will die without knowledge.
Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
13 “But those who are godless in heart lay up anger. They don’t cry for help when he binds them.
Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
14 They die in youth. Their life perishes among the unclean.
Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
15 He delivers the afflicted by their affliction, and opens their ear in oppression.
Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
16 Yes, he would have allured you out of distress, into a wide place, where there is no restriction. That which is set on your table would be full of fatness.
Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
17 “But you are full of the judgment of the wicked. Judgment and justice take hold of you.
Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
18 Don’t let riches entice you to wrath, neither let the great size of a bribe turn you aside.
Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
19 Would your wealth sustain you in distress, or all the might of your strength?
Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
20 Don’t desire the night, when people are cut off in their place.
Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
21 Take heed, don’t regard iniquity; for you have chosen this rather than affliction.
Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
22 Behold, God is exalted in his power. Who is a teacher like him?
Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who has prescribed his way for him? Or who can say, ‘You have committed unrighteousness’?
Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
24 “Remember that you magnify his work, about which men have sung.
Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
25 All men have looked on it. Man sees it afar off.
Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
26 Behold, God is great, and we don’t know him. The number of his years is unsearchable.
Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
27 For he draws up the drops of water, which distill in rain from his vapor,
Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
28 which the skies pour down and which drop on man abundantly.
ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
29 Indeed, can anyone understand the spreading of the clouds and the thunderings of his pavilion?
Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
30 Behold, he spreads his light around him. He covers the bottom of the sea.
Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
31 For by these he judges the people. He gives food in abundance.
Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
32 He covers his hands with the lightning, and commands it to strike the mark.
Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
33 Its noise tells about him, and the livestock also, concerning the storm that comes up.
Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.

< Job 36 >