< Hebrews 10 >

1 For the law, having a shadow of the good to come, not the very image of the things, can never with the same sacrifices year by year, which they offer continually, make perfect those who draw near.
Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
2 Or else wouldn’t they have ceased to be offered, because the worshipers, having been once cleansed, would have had no more consciousness of sins?
Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
3 But in those sacrifices there is a yearly reminder of sins.
Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
4 For it is impossible that the blood of bulls and goats should take away sins.
kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
5 Therefore when he comes into the world, he says, “You didn’t desire sacrifice and offering, but you prepared a body for me.
Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema: “Dhabihu na sadaka hukuzitaka, bali mwili uliniandalia;
6 You had no pleasure in whole burnt offerings and sacrifices for sin.
sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukupendezwa nazo.
7 Then I said, ‘Behold, I have come (in the scroll of the book it is written of me) to do your will, O God.’”
Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja, imeandikwa kunihusu katika kitabu: Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”
8 Previously saying, “Sacrifices and offerings and whole burnt offerings and sacrifices for sin you didn’t desire, neither had pleasure in them” (those which are offered according to the law),
Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe).
9 then he has said, “Behold, I have come to do your will.” He takes away the first, that he may establish the second,
Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili.
10 by which will we have been sanctified through the offering of the body of Jesus Christ once for all.
Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.
11 Every priest indeed stands day by day serving and offering often the same sacrifices, which can never take away sins,
Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi.
12 but he, when he had offered one sacrifice for sins forever, sat down on the right hand of God,
Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu.
13 from that time waiting until his enemies are made the footstool of his feet.
Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake,
14 For by one offering he has perfected forever those who are being sanctified.
kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.
15 The Holy Spirit also testifies to us, for after saying,
Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:
16 “This is the covenant that I will make with them after those days,” says the Lord, “I will put my laws on their heart, I will also write them on their mind;” then he says,
“Hili ndilo Agano nitakalofanya nao baada ya siku hizo, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika katika nia zao.”
17 “I will remember their sins and their iniquities no more.”
Kisha aongeza kusema: “Dhambi zao na kutokutii kwao sitakumbuka tena.”
18 Now where remission of these is, there is no more offering for sin.
Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.
19 Having therefore, brothers, boldness to enter into the holy place by the blood of Jesus,
Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
20 by the way which he dedicated for us, a new and living way, through the veil, that is to say, his flesh,
kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake,
21 and having a great priest over God’s house,
basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
22 let’s draw near with a true heart in fullness of faith, having our hearts sprinkled from an evil conscience and having our body washed with pure water,
sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
23 let’s hold fast the confession of our hope without wavering; for he who promised is faithful.
Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu.
24 Let’s consider how to provoke one another to love and good works,
Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema.
25 not forsaking our own assembling together, as the custom of some is, but exhorting one another, and so much the more as you see the Day approaching.
Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.
26 For if we sin willfully after we have received the knowledge of the truth, there remains no more a sacrifice for sins,
Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.
27 but a certain fearful expectation of judgment, and a fierceness of fire which will devour the adversaries.
Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu.
28 A man who disregards Moses’ law dies without compassion on the word of two or three witnesses.
Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu.
29 How much worse punishment do you think he will be judged worthy of who has trodden under foot the Son of God, and has counted the blood of the covenant with which he was sanctified an unholy thing, and has insulted the Spirit of grace?
Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema?
30 For we know him who said, “Vengeance belongs to me. I will repay,” says the Lord. Again, “The Lord will judge his people.”
Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.”
31 It is a fearful thing to fall into the hands of the living God.
Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.
32 But remember the former days, in which, after you were enlightened, you endured a great struggle with sufferings:
Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu.
33 partly, being exposed to both reproaches and oppressions, and partly, becoming partakers with those who were treated so.
Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo.
34 For you both had compassion on me in my chains and joyfully accepted the plundering of your possessions, knowing that you have for yourselves a better possession and an enduring one in the heavens.
Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.
35 Therefore don’t throw away your boldness, which has a great reward.
Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno.
36 For you need endurance so that, having done the will of God, you may receive the promise.
Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi.
37 “In a very little while, he who comes will come and will not wait.
Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.
38 But the righteous one will live by faith. If he shrinks back, my soul has no pleasure in him.”
Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.”
39 But we are not of those who shrink back to destruction, but of those who have faith to the saving of the soul.
Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.

< Hebrews 10 >