< Amos 1 >

1 The words of Amos, who was among the herdsmen of Tekoa, which he saw concerning Israel in the days of Uzziah king of Judah and in the days of Jeroboam the son of Joash, king of Israel, two years before the earthquake.
Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
2 He said: “Yahweh will roar from Zion, and utter his voice from Jerusalem; and the pastures of the shepherds will mourn, and the top of Carmel will wither.”
Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
3 Yahweh says: “For three transgressions of Damascus, yes, for four, I will not turn away its punishment, because they have threshed Gilead with threshing instruments of iron;
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
4 but I will send a fire into the house of Hazael, and it will devour the palaces of Ben Hadad.
Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
5 I will break the bar of Damascus, and cut off the inhabitant from the valley of Aven, and him who holds the scepter from the house of Eden; and the people of Syria shall go into captivity to Kir,” says Yahweh.
Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
6 Yahweh says: “For three transgressions of Gaza, yes, for four, I will not turn away its punishment, because they carried away captive the whole community, to deliver them up to Edom;
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
7 but I will send a fire on the wall of Gaza, and it will devour its palaces.
nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
8 I will cut off the inhabitant from Ashdod, and him who holds the scepter from Ashkelon; and I will turn my hand against Ekron; and the remnant of the Philistines will perish,” says the Lord Yahweh.
Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
9 Yahweh says: “For three transgressions of Tyre, yes, for four, I will not turn away its punishment; because they delivered up the whole community to Edom, and didn’t remember the brotherly covenant;
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
10 but I will send a fire on the wall of Tyre, and it will devour its palaces.”
Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
11 Yahweh says: “For three transgressions of Edom, yes, for four, I will not turn away its punishment, because he pursued his brother with the sword and cast off all pity, and his anger raged continually, and he kept his wrath forever;
Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
12 but I will send a fire on Teman, and it will devour the palaces of Bozrah.”
Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
13 Yahweh says: “For three transgressions of the children of Ammon, yes, for four, I will not turn away its punishment, because they have ripped open the pregnant women of Gilead, that they may enlarge their border.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
14 But I will kindle a fire in the wall of Rabbah, and it will devour its palaces, with shouting in the day of battle, with a storm in the day of the whirlwind;
Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
15 and their king will go into captivity, he and his princes together,” says Yahweh.
Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.

< Amos 1 >