< Psalms 26 >

1 By David. Judge me, LORD, for I have walked in my integrity. I have trusted also in the LORD without wavering.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Examine me, LORD, and prove me. Try my heart and my mind.
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 For your loving kindness is before my eyes. I have walked in your truth.
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 I have not sat with deceitful men, neither will I go in with hypocrites.
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 I hate the assembly of evildoers, and will not sit with the wicked.
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 I will wash my hands in innocence, so I will go about your altar, LORD,
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 that I may make the voice of thanksgiving to be heard and tell of all your wondrous deeds.
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 LORD, I love the habitation of your house, the place where your glory dwells.
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 Don’t gather my soul with sinners, nor my life with bloodthirsty men
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 in whose hands is wickedness; their right hand is full of bribes.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 But as for me, I will walk in my integrity. Redeem me, and be merciful to me.
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 My foot stands in an even place. In the congregations I will bless the LORD.
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.

< Psalms 26 >