< Psalms 143 >

1 A Psalm by David. Hear my prayer, LORD. Listen to my petitions. In your faithfulness and righteousness, relieve me.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
2 Don’t enter into judgement with your servant, for in your sight no man living is righteous.
Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
3 For the enemy pursues my soul. He has struck my life down to the ground. He has made me live in dark places, as those who have been long dead.
Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
4 Therefore my spirit is overwhelmed within me. My heart within me is desolate.
Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
5 I remember the days of old. I meditate on all your doings. I contemplate the work of your hands.
Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
6 I spread out my hands to you. My soul thirsts for you, like a parched land. (Selah)
Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
7 Hurry to answer me, LORD. My spirit fails. Don’t hide your face from me, so that I don’t become like those who go down into the pit.
Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
8 Cause me to hear your loving kindness in the morning, for I trust in you. Cause me to know the way in which I should walk, for I lift up my soul to you.
Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
9 Deliver me, LORD, from my enemies. I flee to you to hide me.
Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
10 Teach me to do your will, for you are my God. Your Spirit is good. Lead me in the land of uprightness.
Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
11 Revive me, LORD, for your name’s sake. In your righteousness, bring my soul out of trouble.
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
12 In your loving kindness, cut off my enemies, and destroy all those who afflict my soul, for I am your servant.
Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

< Psalms 143 >