< Mark 1 >

1 The beginning of the Good News of Jesus Christ the Son of God.
Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2 As it is written in Isaiah the Prophet, "See, I am sending My messenger before Thee, Who will prepare Thy way";
Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3 "The voice of one crying aloud: 'In the Desert prepare a road for the Lord: Make His highways straight.'"
Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
4 So John the Baptizer came, and was in the Desert proclaiming a baptism of the penitent for forgiveness of sins.
Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5 There went out to him people of all classes from Judaea, and the inhabitants of Jerusalem of all ranks, and were baptized by him in the river Jordan, making open confession of their sins.
Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6 As for John, his garment was of camel's hair, and he wore a loincloth of leather; and his food was locusts and wild honey.
Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7 His announcement was, "There is One coming after me mightier than I--One whose sandal-strap I am unworthy to stoop down and unfasten.
Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8 I have baptized you with water, but He will baptize you with the Holy Spirit."
Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
9 At that time Jesus came from Nazareth in Galilee and was baptized by John in the Jordan;
Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10 and immediately on His coming up out of the water He saw an opening in the sky, and the Spirit like a dove coming down to Him;
Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11 and a voice came from the sky, saying, "Thou art My Son dearly loved: in Thee is My delight."
Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
12 At once the Spirit impelled Him to go out into the Desert,
Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13 where He remained for forty days, tempted by Satan; and He was among the wild beasts, but the angels waited upon Him.
akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14 Then, after John had been thrown into prison, Jesus came into Galilee proclaiming God's Good News.
Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15 "The time has fully come," He said, "and the Kingdom of God is close at hand: repent, and believe this Good News.
“Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
16 One day, passing along the shore of the Lake of Galilee, He saw Simon and Andrew, Simon's brother, throwing their nets in the Lake; for they were fisherman.
Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17 "Come and follow me," said Jesus, "and I will make you fishers for men."
Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
18 At once they left their nets and followed Him.
Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19 Going on a little further He saw James the son of Zabdi and his brother John: they also were in the boat mending the nets, and He immediately called them.
Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20 They therefore left their father Zabdi in the boat with the hired men, and went and followed Him.
Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21 So they came to Capernaum, and on the next Sabbath He went to the synagogue and began to teach.
Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22 The people listened with amazement to His teaching--for there was authority about it: it was very different from that of the Scribes--
Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23 when all at once, there in their synagogue, a man under the power of a foul spirit screamed out:
Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24 "What have you to do with us, Jesus the Nazarene? Have you come to destroy us? I know who you are--God's Holy One."
akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
25 But Jesus reprimanded him, saying, "Silence! come out of him."
Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
26 So the foul spirit, after throwing the man into convulsions, came out of him with a loud cry.
Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27 And all were amazed and awe-struck, so they began to ask one another, "What does this mean? Here is a new sort of teaching--and a tone of authority! And even to foul spirits he issues orders and they obey him!"
Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
28 And His fame spread at once everywhere in all that part of Galilee.
Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29 Then on leaving the synagogue they came at once, with James and John, to the house of Simon and Andrew.
Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30 Now Simon's mother-in-law was ill in bed with a fever, and without delay they informed Him about her.
Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31 So He went to her, and taking her hand He raised her to her feet: the fever left her, and she began to wait upon them.
Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32 When it was evening, after sunset people came bringing Him all who were sick and the demoniacs;
Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33 and the whole town was assembled at the door.
Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34 Then He cured numbers of people who were ill with various diseases, and He drove out many demons; not allowing the demons to speak, because they knew who He was.
Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35 In the morning He rose early, while it was still quite dark, and leaving the house He went away to a solitary place and there prayed.
Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36 And Simon and the others searched everywhere for Him.
Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37 When they found Him they said, "Every one is looking for you."
Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
38 "Let us go elsewhere, to the neighbouring country towns," He replied, "that I may proclaim my Message there also; because for that purpose I came from God."
Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
39 And He went through all Galilee, preaching in the synagogues and expelling the demons.
Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40 One day there came a leper to Jesus entreating Him, and pleading on his knees. "If you are willing," he said, "you are able to cleanse me."
Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
41 Moved with pity Jesus reached out His hand and touched him. "I am willing," He said; "be cleansed."
Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
42 The leprosy at once left him, and he was cleansed.
Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43 Jesus at once sent him away, strictly charging him,
Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44 and saying, "Be careful not to tell any one, but go and show yourself to the Priest, and for your purification present the offerings that Moses appointed as evidence for them."
“Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
45 But the man, when he went out, began to tell every one and to publish the matter abroad, so that it was no longer possible for Jesus to go openly into any town; but He had to remain outside in unfrequented places, where people came to Him from all parts.
Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.

< Mark 1 >