< Luke 19 >

1 So He entered Jericho and was passing through the town.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 There was a man there called Zacchaeus, who was the local surveyor of taxes, and was wealthy.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 He was anxious to see what sort of man Jesus was; but he could not because of the crowd, for he was short in stature.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 So he ran on in front and climbed up a mulberry tree to see Him; for He was about to pass that way.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 As soon as Jesus came to the place, He looked up and said to him, "Zacchaeus, come down quickly, for I must stay at your house to-day."
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 So he came down in haste, and welcomed Him joyfully.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 When they all saw this, they began to complain with indignation. "He has gone in to be the guest of a notorious sinner!" they said.
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 Zacchaeus however stood up, and addressing the Lord said, "Here and now, Master, I give half my property to the poor, and if I have unjustly exacted money from any man, I pledge myself to repay to him four times the amount."
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Turning towards him, Jesus replied, "To-day salvation has come to this house, seeing that he too is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 For the Son of Man has come to seek and to save that which was lost."
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 As they were listening to His words, He went on to teach them by a parable, because He was near to Jerusalem and they supposed that the Kingdom of God was going to appear immediately.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 So He said to them, "A man of noble family travelled to a distant country to obtain the rank of king, and to return.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 And he called ten of his servants and gave each of them a pound, instructing them to trade with the money during his absence.
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 "Now his countrymen hated him, and sent a deputation after him to say, 'We are not willing that he should become our king.'
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 And upon his return, after he had obtained the sovereignty, he ordered those servants to whom he had given the money to be summoned before him, that he might learn their success in trading.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 "So the first came and said, "'Sir, your pound has produced ten pounds more.'
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 "'Well done, good servant,' he replied; 'because you have been faithful in a very small matter, be in authority over ten towns.'
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 "The second came, and said, "'Your pound, Sir, has produced five pounds.'
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 "So he said to this one also, "'And you, be the governor of five towns.'
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 "The next came. "'Sir,' he said, 'here is your pound, which I have kept wrapt up in a cloth.
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 For I was afraid of you, because you are a severe man: you take up what you did not lay down, and you reap what you did not sow.'
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 "'By your own words,' he replied, 'I will judge you, you bad servant. You knew me to be a severe man, taking up what I did not lay down, and reaping what I did not sow:
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 why then did you not put my money into a bank, that when I came I might have received it back with interest?
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 "And he said to those who stood by, "'Take the pound from him and give it to him who has the ten pounds.'
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 ("They said to him, "'Sir, he already has ten pounds.')
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 "'I tell you that to every one who has anything, more shall be given; and from him who has not anything, even what he has shall be taken away.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But as for those enemies of mine who were unwilling that I should become their king, bring them here, and cut them to pieces in my presence.'"
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 After thus speaking, He journeyed onward, proceeding up to Jerusalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 And when he was come near Bethphage and Bethany, at the Mount called the Oliveyard, He sent two of the disciples on in front,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 saying to them, "Go into the village facing you. On entering it you will find an ass's foal tied up which no one has ever yet ridden: untie it, and bring it here.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 And if any one asks you, 'Why are you untying the colt?' simply say, 'The Master needs it.'"
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 So those who were sent went and found things as He had told them.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 And while they were untying the colt the owners called out, "Why are you untying the colt?"
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 and they replied, "The Master needs it."
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 Then they brought it to Jesus, and after throwing their outer garments on the colt they placed Jesus on it.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 So He rode on, while they carpeted the road with their garments.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 And when He was now getting near Jerusalem, and descending the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began in their joy to praise God in loud voices for all the mighty deeds they had witnessed.
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 "Blessed is the King," they cried, "who comes in the name of the Lord: in Heaven peace, and glory in the highest realms."
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 Thereupon some of the Pharisees in the crowd appealed to Him, saying, "Rabbi, reprove your disciples."
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 "I tell you," He replied, "that if they became silent, the very stones would cry out."
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 When He came into full view of the city, He wept aloud over it, and exclaimed,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 "O that at this time thou hadst known--yes even thou--what makes peace possible! But now it is hid from thine eyes.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For the time is coming upon thee when thy foes will throw up around thee earthworks and a wall, investing thee and hemming thee in on every side.
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 And they will dash thee to the ground and thy children within thee, and will not leave one stone upon another within thee; because thou hast not recognized the time of thy visitation."
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 Then Jesus entered the Temple and proceeded to drive out the dealers.
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 "It is written," He said, "'And My house shall be the House of Prayer,' but you have made it a robbers' cave."
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 And day after day He taught in the Temple, while the High Priests and the Scribes were devising some means of destroying Him, as were also the leading men of the people.
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 But they could not find any way of doing it, for the people all hung upon His lips.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >