< Luke 20 >

1 And it came to pass, [that] on one of those days, as he was teaching the people in the temple, and preaching the gospel, the chief priests and the scribes came upon [him], with the elders,
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 And spoke to him, saying, Tell us, By what authority doest thou these things? or who is he that gave thee this authority?
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 And he answered and said to them, I will also ask you one thing; and answer me:
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 The baptism of John, was it from heaven, or from men?
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 And they reasoned with themselves, saying, If we shall say, From heaven; he will say, Why then believed ye him not?
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 But if we say, From men; all the people will stone us: for they are persuaded that John was a prophet.
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 And they answered, that they could not tell whence [it was].
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 And Jesus said to them, Neither do I tell you by what authority I do these things.
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 Then he began to speak to the people this parable; A certain man planted a vineyard, and let it to husbandmen, and went into a far country for a long time.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 And at the season he sent a servant to the husbandmen, that they should give him of the fruit of the vineyard: but the husbandmen beat him, and sent [him] away empty.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 And again he sent another servant: and they beat him also, and treated [him] shamefully, and sent [him] away empty.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 And again he sent the third: and they wounded him also, and cast [him] out.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 Then said the lord of the vineyard, What shall I do? I will send my beloved son: it may be when they see him they will reverence him.
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 But when the husbandmen saw him, they reasoned among themselves, saying, This is the heir; come, let us kill him, that the inheritance may be ours.
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 So they cast him out of the vineyard, and killed [him]. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 He will come and destroy these husbandmen, and will give the vineyard to others. And when they heard [it], they said, may that never be.
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 And he beheld them, and said, What is this then that is written, The stone which the builders rejected, the same is become the head of the corner?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 Whoever shall fall upon that stone, shall be broken: but on whomsoever it shall fall, it will grind him to powder.
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 And the chief priests and the scribes the same hour sought to lay hands on him; and they feared the people: for they perceived that he had spoken this parable against them.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 And they watched [him], and sent forth spies, who should feign themselves just men, that they might take hold of his words, that so they might deliver him to the power and authority of the governor.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 And they asked him, saying, Master, we know that thou sayest and teachest rightly, neither acceptest thou the person [of any], but teachest the way of God truly:
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Is it lawful for us to give tribute to Cesar, or not?
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 But he perceived their craftiness, and said to them, Why tempt ye me?
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Show me a penny. Whose image and superscription hath it? They answered and said, Cesar's.
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 And he said to them, Render therefore to Cesar the things which are Cesar's, and to God the things which are God's.
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 And they could not take hold of his words before the people: and they marveled at his answer, and held their peace.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 Then came to [him] certain of the Sadducees (who deny that there is any resurrection) and they asked him,
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 Saying, Master, Moses wrote to us, If any man's brother should die, having a wife, and he should die without children, that his brother should take his wife, and raise up seed to his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 There were therefore seven brothers: and the first took a wife, and died without children.
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 And the second took her for a wife, and he died childless.
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 And the third took her; and in like manner the seven also: And they left no children, and died.
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 Last of all the woman died also.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 Therefore in the resurrection, whose wife of them is she? for seven had her to wife.
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 And Jesus answering, said to them, The children of this world marry, and are given in marriage: (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn g165)
35 But they who shall be accounted worthy to obtain that world, and the resurrection from the dead, neither marry, nor are given in marriage. (aiōn g165)
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn g165)
36 Neither can they die any more: for they are equal to the angels; and are the children of God, being the children of the resurrection.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 Now that the dead are raised, even Moses showed at the bush, when he calleth the Lord the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob.
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 For he is not a God of the dead, but of the living: for all live to him.
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 Then certain of the scribes answering, said, Master, thou hast well said.
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 And after that, they durst not ask him any question at all.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 And he said to them, How say they that Christ is David's son?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 And David himself saith in the book of Psalms, The LORD said to my Lord, Sit thou on my right hand,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 Till I make thy enemies thy footstool.
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 David therefore calleth him Lord, how is he then his son?
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 Then in the audience of all the people, he said to his disciples,
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 Beware of the scribes, who desire to walk in long robes, and love greetings in the markets, and the highest seats in the synagogues, and the chief rooms at feasts;
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 Who devour widows' houses, and for a show make long prayers: the same shall receive greater damnation.
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”

< Luke 20 >