< Psalms 50 >

1 A Psalm of Asaph. The mighty God, even the LORD, hath spoken, and called the earth from the rising to the setting of the sun.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 Out of Zion, the perfection of beauty, God hath shined.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Our God shall come, and shall not keep silence: a fire shall devour before him, and it shall be very tempestuous around him.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 He shall call to the heavens from above, and to the earth, that he may judge his people.
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Gather my saints together to me; those that have made a covenant with me by sacrifice.
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 And the heavens shall declare his righteousness: for God is judge himself. (Selah)
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 Hear, O my people, and I will speak; O Israel, and I will testify against thee: I am God, even thy God.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 I will not reprove thee for thy sacrifices or thy burnt offerings, to have been continually before me.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 I will take no bull out of thy house, nor male goats out of thy folds.
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 For every beast of the forest is mine, and the cattle upon a thousand hills.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 I know all the fowls of the mountains: and the wild beasts of the field are mine.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 If I were hungry, I would not tell thee: for the world is mine, and all it containeth.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Will I eat the flesh of bulls, or drink the blood of goats?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Offer to God thanksgiving; and pay thy vows to the most High:
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 And call upon me in the day of trouble: I will deliver thee, and thou shalt glorify me.
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 But to the wicked God saith, What hast thou to do to declare my statutes, or that thou shouldest take my covenant in thy mouth?
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 Seeing thou hatest instruction, and castest my words behind thee.
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 When thou sawest a thief, then thou didst consent with him, and hast been partaker with adulterers.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 Thou givest thy mouth to evil, and thy tongue frameth deceit.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 Thou sittest and speakest against thy brother; thou slanderest thy own mother’s son.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 These things hast thou done, and I kept silence; thou thoughtest that I was altogether such an one as thyself: but I will reprove thee, and set them in order before thine eyes.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 Now consider this, ye that forget God, lest I tear you in pieces, and there be none to deliver.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 Whoever offereth praise glorifieth me: and to him that ordereth his conduct aright will I show the salvation of God.
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Psalms 50 >