< Psalms 45 >

1 To the chief Musician upon Shoshannim, for the sons of Korah, Maschil, A Song of loves. My heart is overflowing with a good matter: I speak of the things which I have made concerning the king: my tongue is the pen of a skilful writer.
Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
2 Thou art fairer than the children of men: grace is poured into thy lips: therefore God hath blessed thee for ever.
Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Gird thy sword upon thy thigh, O most mighty, with thy glory and thy majesty.
Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
4 And in thy majesty ride prosperously because of truth and meekness and righteousness; and thy right hand shall teach thee terrible things.
Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
5 Thy arrows are sharp in the heart of the king’s enemies; by which the people fall under thee.
Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
6 Thy throne, O God, is for ever and ever: the sceptre of thy kingdom is a sceptre of justice.
Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
7 Thou lovest righteousness, and hatest wickedness: therefore God, thy God, hath anointed thee with the oil of gladness above thy companions.
Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8 All thy garments smell of myrrh, and aloes, and cassia, out of the ivory palaces, by which they have made thee glad.
Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
9 Kings’ daughters were among thy honourable women: upon thy right hand stood the queen in gold of Ophir.
Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
10 Hearken, O daughter, and consider, and incline thy ear; forget also thy own people, and thy father’s house;
Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
11 So shall the king greatly desire thy beauty: for he is thy Lord; and worship thou him.
Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
12 And the daughter of Tyre shall be there with a gift; even the rich among the people shall entreat thy favour.
Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
13 The king’s daughter is all glorious within: her clothing is of wrought gold.
Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
14 She shall be brought to the king in raiment of needlework: the virgins her companions that follow her shall be brought to thee.
Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
15 With gladness and rejoicing shall they be brought: they shall enter into the king’s palace.
Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
16 Instead of thy fathers shall be thy children, whom thou mayest make princes in all the earth.
Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
17 I will make thy name to be remembered in all generations: therefore shall the people praise thee for ever and ever.
Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.

< Psalms 45 >