< Psalms 36 >

1 To the chief Musician, A Psalm of David the servant of the LORD. The transgression of the wicked saith within my heart, that there is no fear of God before his eyes.
Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
2 For he flattereth himself in his own eyes, until his iniquity is found to be hateful.
Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
3 The words of his mouth are iniquity and deceit: he hath ceased to be wise, and to do good.
Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 He deviseth mischief upon his bed; he setteth himself in a way that is not good; he abhorreth not evil.
Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
5 Thy mercy, O LORD, is in the heavens; and thy faithfulness reacheth to the clouds.
Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
6 Thy righteousness is like the great mountains; thy judgments are a great deep: O LORD, thou preservest man and beast.
Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
7 How excellent is thy lovingkindness, O God! therefore the children of men put their trust under the shadow of thy wings.
Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
8 They shall be abundantly satisfied with the fatness of thy house; and thou shalt make them drink of the river of thy pleasures.
Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
9 For with thee is the fountain of life: in thy light shall we see light.
Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
10 O continue thy lovingkindness to them that know thee; and thy righteousness to the upright in heart.
Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
11 Let not the foot of pride come against me, and let not the hand of the wicked remove me.
Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
12 There are the workers of iniquity fallen: they are cast down, and shall not be able to rise.
Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.

< Psalms 36 >