< Psalms 146 >

1 Praise ye the LORD. Praise the LORD, O my soul.
Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
2 While I live will I praise the LORD: I will sing praises to my God while I have any being.
Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
3 Put not your trust in princes, nor in the son of man, in whom there is no help.
Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
4 His breath goeth forth, he returneth to his earth; in that very day his thoughts perish.
Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
5 Happy is he that hath the God of Jacob for his help, whose hope is in the LORD his God:
Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
6 Who made heaven, and earth, the sea, and all that is in them: who keepeth truth for ever:
Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
7 Who executeth judgment for the oppressed: who giveth food to the hungry. The LORD looseth the prisoners:
Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
8 The LORD openeth the eyes of the blind: the LORD raiseth them that are bowed down: the LORD loveth the righteous:
Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
9 The LORD preserveth the strangers; he relieveth the fatherless and widow: but the way of the wicked he turneth upside down.
Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
10 The LORD shall reign for ever, even thy God, O Zion, to all generations. Praise ye the LORD.
Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.

< Psalms 146 >