< Psalms 142 >

1 Maschil of David; A Prayer when he was in the cave. I cried to the LORD with my voice; with my voice to the LORD I made my supplication.
Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
2 I poured out my complaint before him; I showed before him my trouble.
Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
3 When my spirit was overwhelmed within me, then thou knewest my path. In the way in which I walked have they secretly laid a snare for me.
Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
4 I looked on my right hand, and beheld, but there was no man that would know me: refuge failed me; no man cared for my soul.
Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
5 I cried to thee, O LORD: I said, Thou art my refuge and my portion in the land of the living.
Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 Attend to my cry; for I am brought very low: deliver me from my persecutors; for they are stronger than I.
Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
7 Bring my soul out of prison, that I may praise thy name: the righteous shall surround me; for thou shalt deal bountifully with me.
Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”

< Psalms 142 >