< Psalms 141 >

1 A Psalm of David. LORD, I cry to thee: make haste to me; give ear to my voice, when I cry to thee.
Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
2 Let my prayer be set forth before thee as incense; and the lifting up of my hands as the evening sacrifice.
Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
3 Set a watch, O LORD, before my mouth; keep the door of my lips.
Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
4 Incline not my heart to any evil thing, to practise wicked works with men that work iniquity: and let me not eat of their dainties.
Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
5 Let the righteous smite me; it shall be a kindness: and let him reprove me; it shall be an excellent oil, which shall not break my head: for yet my prayer also shall be in their calamities.
Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
6 When their judges are overthrown in stony places, they shall hear my words; for they are sweet.
Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
7 Our bones are scattered at the grave’s mouth, as when one cutteth and cleaveth wood upon the earth. (Sheol h7585)
Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
8 But my eyes are to thee, O GOD the Lord: in thee is my trust; leave not my soul destitute.
Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
9 Keep me from the traps which they have laid for me, and the snares of the workers of iniquity.
Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
10 Let the wicked fall into their own nets, while I escape.
Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.

< Psalms 141 >