< Psalms 138 >

1 A Psalm of David. I will praise thee with my whole heart: before the gods will I sing praise to thee.
Nitakushukuru kwa moyo wangu wote; mbele ya miungu nitakuimbia sifa.
2 I will worship toward thy holy temple, and praise thy name for thy lovingkindness and for thy truth: for thou hast magnified thy word above all thy name.
Nitasujundu mbele ya hekalu lako takatifu na kulishukuru jina lako kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na kwa uaminifu wako. Umelifanya muhimu zaidi neno lako na jina lako kuliko kitu chochote.
3 In the day when I cried thou didst answer me, and strengthen me with strength in my soul.
Siku ile niliyo kuita, ulinijibu; ulinitia moyo na kuitia nguvu nafsi yangu.
4 All the kings of the earth shall praise thee, O LORD, when they hear the words of thy mouth.
Wafalme wote wa nchi watakushukuru wewe, Yahwe, maana watasikia maneno kutoka kinywani mwako.
5 Yea, they shall sing in the ways of the LORD: for great is the glory of the LORD.
Hakika, wataimba kuhusu matendo ya Yahwe, kwa kuwa utukufu wa Yahwe ni mkuu.
6 Though the LORD is high, yet hath he respect to the lowly: but the proud he knoweth afar off.
Maana ingawa Yahwe yuko juu, lakini anawajali wanyenyekevu, lakini hawatambui wenye majivuno.
7 Though I walk in the midst of trouble, thou wilt revive me: thou shalt stretch forth thy hand against the wrath of my enemies, and thy right hand shall save me.
Nijapopita katikati ya hatari, wewe utauhifadhi uhai wangu; utanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, na mkono wako wa kuume utaniokoa.
8 The LORD will perfect that which concerneth me: thy mercy, O LORD, endureth for ever: forsake not the works of thy own hands.
Yahwe yuko pamoja nami hadi mwisho; uaminifu wa agano lako, Yahwe, wadumu milele. Usiwaache wale ambao mikono yako imewaumba.

< Psalms 138 >