< Psalms 132 >

1 A Song of degrees. LORD, remember David, and all his afflictions:
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 How he swore to the LORD, and vowed to the mighty God of Jacob;
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 Surely I will not come into the tabernacle of my house, nor go up into my bed;
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 I will not give sleep to my eyes, or slumber to my eyelids,
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 Until I find a place for the LORD, an habitation for the mighty God of Jacob.
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Lo, we heard of it at Ephratah: we found it in the fields of the wood.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 We will go into his tabernacles: we will worship at his footstool.
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Arise, O LORD, into thy rest; thou, and the ark of thy strength.
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Let thy priests be clothed with righteousness; and let thy saints shout for joy.
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 For thy servant David’s sake turn not away the face of thy anointed.
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 The LORD hath sworn in truth to David; he will not turn from it; Of the fruit of thy body will I set upon thy throne.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 If thy children will keep my covenant and my testimony that I shall teach them, their children also shall sit upon thy throne for evermore.
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 For the LORD hath chosen Zion; he hath desired it for his habitation.
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 This is my rest for ever: here will I dwell; for I have desired it.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 I will abundantly bless her provision: I will satisfy her poor with bread.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 I will also clothe her priests with salvation: and her saints shall shout aloud for joy.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 There will I make the horn of David to bud: I have ordained a lamp for my anointed.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 His enemies will I clothe with shame: but upon himself shall his crown flourish.
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Psalms 132 >