< Proverbs 27 >

1 Boast not thyself of to morrow; for thou knowest not what a day may bring forth.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
2 Let another man praise thee, and not thy own mouth; a stranger, and not thy own lips.
Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
3 A stone is heavy, and the sand weighty; but a fool’s wrath is heavier than both.
Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
4 Wrath is cruel, and anger is outrageous; but who is able to stand before envy?
Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
5 Open rebuke is better than secret love.
Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
6 Faithful are the wounds of a friend; but the kisses of an enemy are deceitful.
Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
7 The full soul loatheth an honeycomb; but to the hungry soul every bitter thing is sweet.
Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
8 As a bird that wandereth from her nest, so is a man that wandereth from his place.
Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
9 Ointment and perfume rejoice the heart: so doth the sweetness of a man’s friend by hearty counsel.
Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
10 Thy own friend, and thy father’s friend, forsake not; neither go into thy brother’s house in the day of thy calamity: for better is a neighbour that is near than a brother far off.
Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
11 My son, be wise, and make my heart glad, that I may answer him that reproacheth me.
Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
12 A prudent man foreseeth the evil, and hideth himself; but the simple pass on, and are punished.
Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
13 Take his garment that is surety for a stranger, and take a pledge of him for adulteress.
vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
14 He that blesseth his friend with a loud voice, rising early in the morning, it shall be counted a curse to him.
Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
15 A continual dropping in a very rainy day and a contentious woman are alike.
Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
16 Whoever hideth her hideth the wind, and the ointment of his right hand, which betrayeth itself.
kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
17 Iron sharpeneth iron; so a man sharpeneth the countenance of his friend.
Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
18 He that keepeth the fig tree shall eat the fruit of it: so he that waiteth on his master shall be honoured.
Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
19 As in water face answereth to face, so the heart of man to man.
Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
20 Hell and destruction are never full; so the eyes of man are never satisfied. (Sheol h7585)
Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
21 As the refining pot for silver, and the furnace for gold; so is a man to his praise.
Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
22 Though thou shouldest crush a fool in a mortar among grain with a pestle, yet his foolishness will not depart from him.
Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
23 Be thou diligent to know the state of thy flocks, and look well to thy herds.
Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
24 For riches are not for ever: and doth the crown endure to every generation?
maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
25 The plant appeareth, and the tender grass showeth itself, and herbs of the mountains are gathered.
Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
26 The lambs are for thy clothing, and the goats are the price of the field.
Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
27 And thou shalt have goats’ milk enough for thy food, for the food of thy household, and for maintenance for thy maidens.
Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.

< Proverbs 27 >