< Proverbs 15 >

1 A soft answer turneth away wrath: but grievous words stir up anger.
Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
2 The tongue of the wise useth knowledge aright: but the mouth of fools poureth out foolishness.
Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
3 The eyes of the LORD are in every place, beholding the evil and the good.
Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
4 A wholesome tongue is a tree of life: but perverseness in it is a breach in the spirit.
Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
5 A fool despiseth his father’s instruction: but he that regardeth reproof is prudent.
Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
6 In the house of the righteous is much treasure: but in the revenues of the wicked is trouble.
Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
7 The lips of the wise disperse knowledge: but the heart of the foolish doeth not so.
Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
8 The sacrifice of the wicked is an abomination to the LORD: but the prayer of the upright is his delight.
Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
9 The way of the wicked is an abomination to the LORD: but he loveth him that followeth after righteousness.
Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
10 Correction is grievous to him that forsaketh the way: and he that hateth reproof shall die.
Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
11 Hell and destruction are before the LORD: how much more then the hearts of the children of men? (Sheol h7585)
Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
12 A scorner loveth not one that reproveth him: neither will he go to the wise.
Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
13 A merry heart maketh a cheerful countenance: but by sorrow of the heart the spirit is broken.
Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
14 The heart of him that hath understanding seeketh knowledge: but the mouth of fools feedeth on foolishness.
Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
15 All the days of the afflicted are evil: but he that is of a merry heart hath a continual feast.
Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
16 Better is little with the fear of the LORD than great treasure and trouble with it.
Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
17 Better is a dinner of herbs where love is, than a stalled ox and hatred with it.
Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
18 A wrathful man stirreth up strife: but he that is slow to anger appeaseth strife.
Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
19 The way of the slothful man is as an hedge of thorns: but the way of the righteous is made plain.
Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
20 A wise son maketh a glad father: but a foolish man despiseth his mother.
Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
21 Folly is joy to him that is destitute of wisdom: but a man of understanding walketh uprightly.
Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
22 Without counsel purposes are disappointed: but in the multitude of counsellors they are established.
Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
23 A man hath joy by the answer of his mouth: and a word spoken in due season, how good it is!
Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
24 The way of life is above to the wise, that he may depart from hell beneath. (Sheol h7585)
Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
25 The LORD will destroy the house of the proud: but he will establish the border of the widow.
Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
26 The thoughts of the wicked are an abomination to the LORD: but the words of the pure are pleasant words.
Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
27 He that is greedy of gain troubleth his own house; but he that hateth bribes shall live.
Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
28 The heart of the righteous studieth to answer: but the mouth of the wicked poureth out evil things.
Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
29 The LORD is far from the wicked: but he heareth the prayer of the righteous.
Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
30 The light of the eyes rejoiceth the heart: and a good report maketh the bones fat.
Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
31 The ear that heareth the reproof of life abideth among the wise.
Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
32 He that refuseth instruction despiseth his own soul: but he that heareth reproof getteth understanding.
Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
33 The fear of the LORD is the instruction of wisdom; and before honour is humility.
Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.

< Proverbs 15 >