< Numbers 1 >

1 And the LORD spoke to Moses in the wilderness of Sinai, in the tabernacle of the congregation, on the first day of the second month, in the second year after they had come out of the land of Egypt, saying,
Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
2 Take ye the sum of all the congregation of the children of Israel, after their families, by the house of their fathers, with the number of their names, every male by their polls;
'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
3 From twenty years old and upward, all that are able to go forth to war in Israel: thou and Aaron shall number them by their armies.
kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
4 And with you there shall be a man of every tribe; every one head of the house of his fathers.
Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
5 And these are the names of the men that shall stand with you: of the tribe of Reuben; Elizur the son of Shedeur.
Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
6 Of Simeon; Shelumiel the son of Zurishaddai.
kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
7 Of Judah; Nahshon the son of Amminadab.
Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 Of Issachar; Nethaneel the son of Zuar.
Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
9 Of Zebulun; Eliab the son of Helon.
kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
10 Of the children of Joseph: of Ephraim; Elishama the son of Ammihud: of Manasseh; Gamaliel the son of Pedahzur.
kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
11 Of Benjamin; Abidan the son of Gideoni.
kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
12 Of Dan; Ahiezer the son of Ammishaddai.
Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
13 Of Asher; Pagiel the son of Ocran.
kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
14 Of Gad; Eliasaph the son of Deuel.
kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
15 Of Naphtali; Ahira the son of Enan.
na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
16 These were the renowned of the congregation, princes of the tribes of their fathers, heads of thousands in Israel.
Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
17 And Moses and Aaron took these men who are mentioned by their names:
Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
18 And they assembled all the congregation on the first day of the second month, and they declared their genealogies after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, by their polls.
na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
19 As the LORD commanded Moses, so he numbered them in the wilderness of Sinai.
Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
20 And the children of Reuben, Israel’s eldest son, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, by their polls, every male from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
21 Those that were numbered of them, even of the tribe of Reuben, were forty and six thousand and five hundred.
Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
22 Of the children of Simeon, by their generations, after their families, by the house of their fathers, those that were numbered of them, according to the number of the names, by their polls, every male from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
23 Those that were numbered of them, even of the tribe of Simeon, were fifty and nine thousand and three hundred.
Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
24 Of the children of Gad, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
25 Those that were numbered of them, even of the tribe of Gad, were forty and five thousand six hundred and fifty.
Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
26 Of the children of Judah, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
27 Those that were numbered of them, even of the tribe of Judah, were seventy and four thousand and six hundred.
walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
28 Of the children of Issachar, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
29 Those that were numbered of them, even of the tribe of Issachar, were fifty and four thousand and four hundred.
Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
30 Of the children of Zebulun, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
31 Those that were numbered of them, even of the tribe of Zebulun, were fifty and seven thousand and four hundred.
Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
32 Of the children of Joseph, namely, of the children of Ephraim, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
33 Those that were numbered of them, even of the tribe of Ephraim, were forty thousand and five hundred.
Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
34 Of the children of Manasseh, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
35 Those that were numbered of them, even of the tribe of Manasseh, were thirty and two thousand and two hundred.
Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
36 Of the children of Benjamin, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
37 Those that were numbered of them, even of the tribe of Benjamin, were thirty and five thousand and four hundred.
Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
38 Of the children of Dan, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
39 Those that were numbered of them, even of the tribe of Dan, were sixty and two thousand and seven hundred.
Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
40 Of the children of Asher, by their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
41 Those that were numbered of them, even of the tribe of Asher, were forty and one thousand and five hundred.
Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
42 Of the children of Naphtali, throughout their generations, after their families, by the house of their fathers, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war;
Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
43 Those that were numbered of them, even of the tribe of Naphtali, were fifty and three thousand and four hundred.
Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
44 These are those that were numbered, which Moses and Aaron numbered, and the princes of Israel, being twelve men: each one was for the house of his fathers.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
45 So were all those that were numbered of the children of Israel, by the house of their fathers, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war in Israel;
Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
46 Even all they that were numbered were six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
Walihesabu wanaume 603, 550.
47 But the Levites after the tribe of their fathers were not numbered among them.
Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
48 For the LORD had spoken to Moses, saying,
Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
49 Only thou shalt not number the tribe of Levi, neither take the sum of them among the children of Israel:
“usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
50 But thou shalt appoint the Levites over the tabernacle of testimony, and over all its vessels, and over all things that belong to it: they shall bear the tabernacle, and all its vessels; and they shall minister to it, and shall encamp around the tabernacle.
Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
51 And when the tabernacle moveth forward, the Levites shall take it down: and when the tabernacle is to be pitched, the Levites shall set it up: and the stranger that cometh near shall be put to death.
Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
52 And the children of Israel shall pitch their tents, every man by his own camp, and every man by his own standard, throughout their hosts.
Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
53 But the Levites shall encamp around the tabernacle of testimony, that there may be no wrath upon the congregation of the children of Israel: and the Levites shall keep the charge of the tabernacle of testimony.
Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
54 And the children of Israel did according to all that the LORD commanded Moses, so did they.
Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.

< Numbers 1 >