< Numbers 2 >

1 And the LORD spoke to Moses and to Aaron, saying,
BWANA akasema na Musa na Haruni tena. Akamwambia,
2 Every man of the children of Israel shall encamp by his own standard, with the banner of their father’s house: far off from the tabernacle of the congregation shall they encamp.
Kila mtu atapanga kulingana na mahali pake, pamoja na mabango ya baba zao. Watapanga kuzunguka hema ya kukutania kila upande.
3 And on the east side toward the rising of the sun shall they of the standard of the camp of Judah encamp throughout their armies: and Nahshon the son of Amminadab shall be captain of the children of Judah.
Wale watakaopanga mashariki mwa hema ya kukutania, mahali ambapo juu huonekana wakati wa jua kuchomoza, ni makambi ya Yuda nao watakuwa katika kundi lao. Nashoni mwana wa Aminadabu ni kiongozi wa watu wa Yuda.
4 And his host, and those that were numbered of them, were seventy and four thousand and six hundred.
Idadi ya watu wa Yuda ni 74, 600.
5 And those that shall encamp next to him shall be the tribe of Issachar: and Nethaneel the son of Zuar shall be captain of the children of Issachar.
Kabila la Isakari litapanga mbele ya Yuda. Nethaneli mwana wa Zuari ataliongoza jeshi la Isakari.
6 And his host, and those that were numbered of them, were fifty and four thousand and four hundred.
Idadi ya kikosi chake ni wanaume 54, 000.
7 Then the tribe of Zebulun: and Eliab the son of Helon shall be captain of the children of Zebulun.
Kabila la Zabuloni litapanga mbele ya Isakari. Eliabu mwana wa Heloni ndiye atakayeliongoza jeshi la Zabuloni.
8 And his host, and those that were numbered of them, were fifty and seven thousand and four hundred.
Idadi ya kikosi chake ni 57, 400.
9 All that were numbered in the camp of Judah were an hundred thousand and eighty thousand and six thousand and four hundred, throughout their armies. These shall first move forward.
Idadi yote ya kambi y a Yuda ni 186, 400. Watakuwa wa kwanza kuondoka.
10 On the south side shall be the standard of the camp of Reuben according to their armies: and the captain of the children of Reuben shall be Elizur the son of Shedeur.
Upande wa kusini kutakuwa na kambi ya Reubeni katika kundi lao. Kiongozi wa kundi la Reubeni ni Elizuri mwana wa Shedeuri.
11 And his host, and those that were numbered of them, were forty and six thousand and five hundred.
Idadi ya kikosi chake ni 46, 500.
12 And those who encamp by him shall be the tribe of Simeon: and the captain of the children of Simeon shall be Shelumiel the son of Zurishaddai.
Simeoni atapanga mbele ya Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Zurishadai.
13 And his host, and those that were numbered of them, were fifty and nine thousand and three hundred.
Waliohesabiwa kwenye kikosi chake ni 59, 300.
14 Then the tribe of Gad: and the captain of the sons of Gad shall be Eliasaph the son of Reuel.
Kabila la Gadi litafuatia. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deuli.
15 And his host, and those that were numbered of them, were forty and five thousand and six hundred and fifty.
Idadi ya kikosi chake ni 45, 650.
16 All that were numbered in the camp of Reuben were an hundred thousand and fifty and one thousand and four hundred and fifty, throughout their armies. And they shall move forward in the second rank.
Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na kikosi chake, ni 151, 450. Watakuwa wa pili kuondoka.
17 Then the tabernacle of the congregation shall move forward with the camp of the Levites in the midst of the camp: as they encamp, so shall they move forward, every man in his place by their standards.
Kifuatacho, ni hema la kukutania kuondoka kambini pamoja na Walawi likiwa katikati ya kambi zote. Lazima waondoke hapo kambini kwa mpangilio huo kama walivyoingia kwenye kambi. Kila mwanamume lazima awe mahali pake kwa kufuata bango lake.
18 On the west side shall be the standard of the camp of Ephraim according to their armies: and the captain of the sons of Ephraim shall be Elishama the son of Ammihud.
Migawanyiko ya kambi y Efraimu kufuata mahali pake. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
19 And his host, and those that were numbered of them, were forty thousand and five hundred.
Hesabu ya kikosi hiki ni 40, 500.
20 And by him shall be the tribe of Manasseh: and the captain of the children of Manasseh shall be Gamaliel the son of Pedahzur.
Baada ya hao lilifuata kabila la Manase. Kiongozi wa Manase ni Gamaliel mwana wa Pedazuri.
21 And his host, and those that were numbered of them, were thirty and two thousand and two hundred.
Hesabu ya kikosi hiki ni 32, 200.
22 Then the tribe of Benjamin: and the captain of the sons of Benjamin shall be Abidan the son of Gideoni.
Kabila litakalofuata ni la Benjamini. Kiongozi wa Benjamini n Abidani mwana wa Gidioni.
23 And his host, and those that were numbered of them, were thirty and five thousand and four hundred.
Hesabu ya kikosi hiki ni 35, 000
24 All that were numbered of the camp of Ephraim were an hundred thousand and eight thousand and an hundred, throughout their armies. And they shall go forward in the third rank.
Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108, 100. Watakuwa wa tatu kuondoka.
25 The standard of the camp of Dan shall be on the north side by their armies: and the captain of the children of Dan shall be Ahiezer the son of Ammishaddai.
Upande wa kaskazini kutakuwa na kambi ya kikosi cha Dani. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
26 And his host, and those that were numbered of them, were sixty and two thousand and seven hundred.
Hesabu ya kikosi hiki ni 62, 700.
27 And those that encamp by him shall be the tribe of Asher: and the captain of the children of Asher shall be Pagiel the son of Ocran.
Watu wa kabila ya Asheri watapanga mbele ya Dani. Kiongozi wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okirani.
28 And his host, and those that were numbered of them, were forty and one thousand and five hundred.
Hesabu ya Kikosi hiki ni 41, 500.
29 Then the tribe of Naphtali: and the captain of the children of Naphtali shall be Ahira the son of Enan.
Kabila la Naftali ndilo litakalofuatia. Kiongozi wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
30 And his host, and those that were numbered of them, were fifty and three thousand and four hundred.
Hesabu ya kikosi hiki ni 53, 400.
31 All they that were numbered in the camp of Dan were an hundred thousand and fifty and seven thousand and six hundred. They shall go last with their standards.
Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157, 600. Hawa watakuwa wa mwisho kuondoka kambini, wakifuata bango lao.
32 These are those who were numbered of the children of Israel by the house of their fathers: all those that were numbered of the camps throughout their hosts were six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
Hawa ndio Waisraeli, waliohesabiwa kufuata familia zao. Wote waliohesabiwa kwenye kambi zao, kwa kufuata vikosi vyao ni 603, 550.
33 But the Levites were not numbered among the children of Israel; as the LORD commanded Moses.
Lakini Musa na Haruni hawakujumuisha Walawi kwenye Hesabu ya Waisrael. Ilikuwa kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa.
34 And the children of Israel did according to all that the LORD commanded Moses: so they encamped by their standards, and so they moved forward, every one after their families, according to the house of their fathers.
Watu wa Israel walifanya yote ambayo BWANA alimwagiza Musa. Walipanga kwa kufuata mabango yao. Walisafiri kutoka kambini kwa kufuata jamaa zao, kwa mpangilio wa familia za koo zao.

< Numbers 2 >