< Numbers 17 >

1 And the LORD spoke to Moses, saying,
BWANA akanena na Musa, akasema,
2 Speak to the children of Israel, and take of every one of them a rod according to the house of their fathers, of all their princes according to the house of their fathers twelve rods: write thou every man’s name upon his rod.
“Waambie wana wa Israeli wakuletee fimbo za kutembelea moja kwa kila jamaa, fimbo kumi na mbili. Uandika jina la kila mmoja kwenye hizo fimbo.
3 And thou shalt write Aaron’s name upon the rod of Levi: for one rod shall be for the head of the house of their fathers.
Utaandika jina la Haruni kwenye jina la Lawi. Kutakuwa na fimbo moja kwa kila kiongozi kutoka kwenye kabila la mababu zake.
4 And thou shalt lay them in the tabernacle of the congregation before the testimony, where I will meet with you.
Utaziweka hizo fimbo kwenye hema ya kukutania mbele ya amri za agano, ambapo Mimi hukutana na wewe. Itakuwa hivi,
5 And it shall come to pass, that the man’s rod, whom I shall choose, shall blossom: and I will make to cease from me the murmurings of the children of Israel, by which they murmur against you.
fimbo ya mtu yule ninayemchagua itachipua. Nitazuia watu wa Israeli walalamikao, ambao wanaongea kinyume na wewe.”
6 And Moses spoke to the children of Israel, and every one of their princes gave him a rod apiece, for each prince one, according to their fathers’ houses, even twelve rods: and the rod of Aaron was among their rods.
Kwa hiyo Musa akawaambia wana wa Israeli. Viongozi wote wa kabila wakampatia fimbo, fimbo moja kutoka kwa kila kiongozi, aliyechaguliwa kutoka kwenye kila kabila ya babu zao, jumla yake fimbo kumi na mbili. Fimbo ya Haruni ilikuwa miongoni mwa fimbo hizo.
7 And Moses laid the rods before the LORD in the tabernacle of witness.
Ndipo Musa alipoziweka zile fimbo mbele ya BWANA katika hema ya amri ya agano.
8 And it came to pass, that on the next day Moses went into the tabernacle of witness; and, behold, the rod of Aaron for the house of Levi had budded, and brought forth buds, and bloomed blossoms, and yielded almonds.
Siku iliyofuata Musa aliingia kwenye hema ya amri ya agano, na tazama, fimbo ya Haruni kwa ajili ya Kabila la Lawi ilikuwa imetoa machipukizi. Machipukizi yalikuwa hadi kuchanua maua na kuzaa malozi mabivu!
9 And Moses brought out all the rods from before the LORD to all the children of Israel: and they looked, and took every man his rod.
Musa akazitoa fimbo zote kutoka kwa BWANA kwa watu wote wa Israeli, na kila mtu akachukua fimbo yake.
10 And the LORD said to Moses, Bring Aaron’s rod again before the testimony, to be kept for a sign against the rebels; and thou shalt quite take away their murmurings from me, that they die not.
BWANA akamwambua Musa, “Iweke fimbo ya Haruni mbele ya amri za agano. Iweke iwe ishara ya hatia mbele ya watu waliopinga ili ukomeshe malalamiko dhidi yangu, vinginevyo watakufa.”
11 And Moses did so: as the LORD commanded him, so did he.
Musa akafanya kama BWANA alivyoagiza.
12 And the children of Israel spoke to Moses, saying, Behold, we die, we perish, we all perish.
Wana wa Israeli wakanena na Musa wakisema, “tutakufa hapa! Wote tutaangamia!
13 Whoever approacheth the tabernacle of the LORD shall die: shall we be consumed with dying?
Kila mmoja anayekuja hapa, anayekaribia masikani ya BWANA, atakufa. Je, ni lazima wote tuangamie?”

< Numbers 17 >