< Numbers 11 >

1 And when the people complained, it displeased the LORD: and the LORD heard it; and his anger was kindled; and the fire of the LORD burnt among them, and consumed them that were in the uttermost parts of the camp.
Sasa watu wakanung'unika juu ya matatizo yao wakati BWANA alipokuwa akiwasikiliza. BWANA akawasikia watu naye akakasirika. Moto kutoka kwa BWANA ukashuka na ukawaka kati yao na kuteketeza baadhi ya kambi kwenye pembe zake.
2 And the people cried to Moses; and when Moses prayed to the LORD, the fire was quenched.
Ndipo watu wakamwita Musa kwa nguvu, Naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukazimika.
3 And he called the name of the place Taberah: because the fire of the LORD burnt among them.
Mahali pale paliitwa Tabera, kwa sababu moto wa BWANA uliwaka kati yao.
4 And the mixed multitude that was among them fell to lusting: and the children of Israel also wept again, and said, Who shall give us flesh to eat?
Baadhi ya wageni wakaanza kuweka kambi zao pamoja na wana wa wa Israeli. Walitaka kula chakula kizuri. Kisha wana wa Israeli walipoanza kulia wakisema, “Ni nani atakayetupatia nyama za kula?
5 We remember the fish, which we ate in Egypt freely; the cucumbers, and the melons, and the leeks, and the onions, and the garlic:
Tunakumbuka samaki tulizokula bure kule Misri, yale matango, na matikiti maji, na mboga na vitunguu na vitunguu saumu.
6 But now our soul is dried away: there is nothing at all, besides this manna, before our eyes.
Na sasa hatuna hamu ya kula, kwa sababu tunaona mana tu.
7 And the manna was as coriander seed, and the colour of it as the colour of bdellium.
Mana ilifanana na punje ya mtama. ilionekana kama bedola.
8 And the people went about, and gathered it, and ground it in mills, or beat it in a mortar, and baked it in pans, and made cakes of it: and the taste of it was as the taste of fresh oil.
watu wakazunguka kisha wakakusanyika. Wakaisaga, wakaitwanga kwa vinu, wakaitokosa nyunguni, na kuitengeneza mikate. radha yake ilikuwa kama mafuta mapya ya mizeituni.
9 And when the dew fell upon the camp in the night, the manna fell upon it.
Na umande ulipoanguka kambini usiku ule, na mana ilianguka pia.
10 Then Moses heard the people weeping throughout their families, every man in the door of his tent: and the anger of the LORD was kindled greatly; Moses also was displeased.
Musa akawasikia watu wakilia katika familia zao, na kila mtu alikuwa kwenye lango la hema yake. BWANA alikasirika sana, na mbele ya macho ya Musa malalamiko yao yalikuwa mabaya.
11 And Moses said to the LORD, Why hast thou afflicted thy servant? and why have I not found favour in thy sight, that thou layest the burden of all this people upon me?
Musa akasema na BWANA, “Kwa nini umemtendea mtumishi wako vibaya namna hiyo? kwa nini hujapendezwa na mimi? unanifanya kubeba mizigo ya hawa watu.
12 Have I conceived all this people? have I begotten them, that thou shouldest say to me, Carry them in thy bosom, as a nursing father beareth the nursing child, to the land which thou sworest to their fathers?
Je, mimi ndiye niliyewatungia mimba hawa watu? Mimi ndiye niliyewazaa kiasi kwamba unaniambia, “wabebe kwa ukaribu vifuani mwako kama baba abebavyo mtoto wake? Je, nitawabeba mpaka kwenye nchi ambayo uliwaahidi mababu zao kuwapa?
13 Where should I get flesh to give to all this people? for they weep to me, saying, Give us flesh, that we may eat.
Naweza kupata wapi nyama za kuwapa watu wote hawa? Wanalia mbele zangu na wanasema, 'tupe nyama tule.'
14 I am not able to bear all this people alone, because it is too heavy for me.
Mimi peke yangu siwezi kuwabeba watu wote hawa. Ni wengi sana kwangu.
15 And if thou dealest thus with me, kill me, I pray thee, out of hand, if I have found favour in thy sight; and let me not see my wretchedness.
Kwa vile unanitendea hivi, basi uniue, na kama wewe ni mpole kwangu, basi niondolee mzigo huu.”
16 And the LORD said to Moses, Gather to me seventy men of the elders of Israel, whom thou knowest to be the elders of the people, and officers over them; and bring them to the tabernacle of the congregation, that they may stand there with thee.
BWANA akamwambia Musa, “Niletee wazee sabini miongoni mwa Waisraeli. Hakikisha ni wazee na viongozi wa watu. Uwalete kwenye hema ya kukutania wasimame pamoja na wewe.
17 And I will come down and talk with thee there: and I will take of the Spirit who is upon thee, and will put it upon them; and they shall bear the burden of the people with thee, that thou mayest not bear it thyself alone.
Nami nitashuka niseme nawe mahali pale. Nitatoa sehemu ya roho iliyo ndani yako na kuwapatia wao. Nao watabeba mzigo wa watu pamoja nawe. na hautaubeba peke yako.
18 And say thou to the people, Sanctify yourselves for to morrow, and ye shall eat flesh: for ye have wept in the ears of the LORD, saying, Who shall give us flesh to eat? for it was well with us in Egypt: therefore the LORD will give you flesh, and ye shall eat.
Waambie watu, 'Jitakaseni ninyi wenyewe, kwa kuwa kesho mtakuala nyama, kwa kuwa mmelia na BWANA amesikia, “Mlipokuwa mkisema kuwa nani atakayetupa nyama tule? Kule Misri tulikula chakula kizuri!” Kwa hiyo BWANA atawapeni nyama, nanyi mtakula nyama.
19 Ye shall not eat one day, nor two days, nor five days, neither ten days, nor twenty days;
Hamtakula nyama kwa siku moja tu, au siku mbili, au siku tano, au siku kumi, au siku ishirini,
20 But even a whole month, until it shall come out at your nostrils, and it be loathsome to you: because ye have despised the LORD who is among you, and have wept before him, saying, Why came we forth out of Egypt?
Lakini mtakula nyama kwa mwezi mmoja mpaka zitakapowatokea puani. Mpaka zitawakinai kwa sababu mmemkataa BWANA ambaye yuko kati yenu. Mmelia mbele yake. mmesema, “Kwa nini tulitoka Misri?””
21 And Moses said, The people, among whom I am, are six hundred thousand footmen; and thou hast said, I will give them flesh, that they may eat a whole month.
Kisha Musa akasema, “Mimi nina watu 600, 000, na wewe umesema, “Nitawapa nyama mle kwa mwezi mmoja,'
22 Shall the flocks and the herds be slain for them, to suffice for them? or shall all the fish of the sea be gathered together for them, to suffice for them?
Je, tutayachinja haya makundi ya ng'ombe na kondoo ili kuwatosheleza?”
23 And the LORD said to Moses, Is the LORD’S hand shortened? thou shalt see now whether my word shall come to pass to thee or not.
BWANA akasema na Musa, “Je mkono wangu ni mfupi? Sasa utaona kama maneno yangu ni ya kweli ama sivyo.
24 And Moses went out, and told the people the words of the LORD, and gathered the seventy men of the elders of the people, and set them around the tabernacle.
Musa alitoka nje kwenda kuwaambia watu maneno ya BWANA. Aliwakusanya wazee sabini wa watu na kuwaweka kuizunguka hema.
25 And the LORD came down in a cloud, and spoke to him, and took of the spirit that was upon him, and gave it to the seventy elders: and it came to pass, that, when the spirit rested upon them, they prophesied, and did not cease.
BWANA akashuka chini katika wingu akaongea na Musa. BWANA akachukua sehemu ya roho iliyokuwa kwa Musa na kuiweka kwa wale wazee sabini. Roho alipowashukia, wakaanza kutoa unabii, lakini ilitokea kwenye tukio hilo tu na haikujirudia tena.
26 But there remained two of the men in the camp, the name of the one was Eldad, and the name of the other Medad: and the spirit rested upon them; and they were of them that were recorded, but went not out to the tabernacle: and they prophesied in the camp.
Watu wawili waitwao Elidadi na Medadi walibaki kambini. Lakini Roho aliwashukia pia. Majina yao yalikuwa yameandikwa kwenye orodha lakini walikuwa hawajaenda hemani. Hata hivyo nao walitoa unabii wakiwa kambini.
27 And there ran a young man, and told Moses, and said, Eldad and Medad do prophesy in the camp.
Kijana mmoja huko kambini alikimbia akaenda kumwambia Musa, “Elidadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
28 And Joshua the son of Nun, the servant of Moses, one of his young men, answered and said, My lord Moses, forbid them.
Joshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Musa, ambaye ni miongoni mwa wale aliowachagua akamwambia Musa, “Bwana wangu Musa, wazuie.”
29 And Moses said to him, Enviest thou for my sake? O that all the LORD’S people were prophets, and that the LORD would put his spirit upon them!
Musa akamwambia, “una wivu kwa niaba yangu? Natamani kama watu wote wa BWANA wangekuwa manabii na kwamba angeweka Roho yake juu yao wote!”
30 And Moses withdrew into the camp, he and the elders of Israel.
Kisha Musa na wale wazee wakarudi kambini.
31 And there went forth a wind from the LORD, and brought quails from the sea, and let them fall by the camp, as it were a day’s journey on this side, and as it were a day’s journey on the other side, around the camp, and as it were two cubits high upon the face of the earth.
Kisha upepo ukavuma kutoka kwa BWANA ukaja na kware kutokea baharini. Wakaanguka karibu na kambi, kiasi cha umbali wa safari ya siku moja upande huu na umbali wa siku moja upande mwingine. Wale kware wakaizunguka kambi kiasi cha mita moja toka uso wa dunia.
32 And the people stood up all that day, and all that night, and all the next day, and they gathered the quails: he that gathered least gathered ten homers: and they spread them all abroad for themselves around the camp.
Watu wakawakusanya hao kware kwa bidii mchana huo wote na usiku huo wote, na mchana wote uliofuatia. Hakuna aliyekusanya pungufu ya mita mbili za uajazo. Wakawaanika kweye ardhi yote hapo kambini.
33 And while the flesh was yet between their teeth, before it was chewed, the wrath of the LORD was kindled against the people, and the LORD smote the people with a very great plague.
Wakati ile nyama ikiwa bado iko kwenye meno yao, wakiwa bado wanatafuna, BWANA akawakasirikia. Akwapiga watu wale kwa gonjwa kubwa sana.
34 And he called the name of that place Kibrothhattaavah: because there they buried the people that lusted.
Mahali pale paliitwa Kibroti Hataava, kwa sababu pale walizika watu waliotamani nyama.
35 And the people journeyed from Kibrothhattaavah to Hazeroth; and abode at Hazeroth.
Kutoka Kibroti Hataava watu wakasafiri hadi Hazeroti, ambapo walipumzika.

< Numbers 11 >