< Judges 4 >

1 And the children of Israel again did evil in the sight of the LORD, after Ehud was dead.
Baada ya Ehudi kufa, watu wa Israeli walifanya tena yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
2 And the LORD sold them into the hand of Jabin king of Canaan, that reigned in Hazor; the captain of whose host was Sisera, who dwelt in Harosheth of the Gentiles.
Bwana akawatia mkononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyewala huko Hasori. Kamanda wa jeshi lake aitwaye Sisera, naye aliishi Harosheti ya Mataifa.
3 And the children of Israel cried to the LORD: for he had nine hundred chariots of iron; and twenty years he mightily oppressed the children of Israel.
Wana wa Israeli wakamwomba Bwana awasaidie, kwa sababu Sisera alikuwa na magari ya chuma mia tisa na akawashinda wana wa Israeli kwa nguvu kwa miaka ishirini.
4 And Deborah, a prophetess, the wife of Lapidoth, she judged Israel at that time.
Basi Debora, nabii wa kike (mke wa Lapidothi), alikuwa mwamuzi anayeongoza katika Israeli wakati huo.
5 And she dwelt under the palm tree of Deborah between Ramah and Bethel in mount Ephraim: and the children of Israel came up to her for judgment.
Naye aliketi chini ya mtende wa Debora kati ya Rama na Betheli katika nchi ya mlima wa Efraimu, na watu wa Israeli walimwendea ili kutatua migogoro yao.
6 And she sent and called Barak the son of Abinoam from Kedeshnaphtali, and said to him, Hath not the LORD God of Israel commanded, saying, Go and draw toward mount Tabor, and take with thee ten thousand men of the children of Naphtali and of the children of Zebulun?
Akamtuma Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali. Akamwambia, Bwana, Mungu wa Israeli, anakuamuru, Nenda katika mlima wa Tabori, uende pamoja nawe watu elfu kumi kutoka Naftali na Zabuloni.
7 And I will draw to thee to the river Kishon Sisera, the captain of Jabin’s army, with his chariots and his multitude; and I will deliver him into thy hand.
Nitamfukuza Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, akutane nawe karibu na mto Kishoni, pamoja na magari yake na jeshi lake, na nitakupa ushindi juu yake. '
8 And Barak said to her, If thou wilt go with me, then I will go: but if thou wilt not go with me, then I will not go.
Baraka akamwambia, 'Ikiwa utakwenda nami, nitakwenda, lakini ikiwa huendi pamoja nami, sitaenda.'
9 And she said, I will surely go with thee: however the journey that thou takest shall not be for thy honour; for the LORD shall sell Sisera into the hand of a woman. And Deborah arose, and went with Barak to Kedesh.
Alisema, 'Nitakwenda nawe. Hata hivyo, njia unayoienda haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamuuza Sisera mkononi mwa mwanamke. Ndipo Debora akainuka, akaenda pamoja na Baraka Kedeshi.
10 And Barak called Zebulun and Naphtali to Kedesh; and he went up with ten thousand men at his feet: and Deborah went up with him.
Baraki akawaita wana wa Zebuloni na Naftali kusanyika Kedeshi. Watu elfu kumi walimfuata, na Debora akaenda pamoja naye.
11 Now Heber the Kenite, who was of the children of Hobab the father in law of Moses, had separated himself from the Kenites, and pitched his tent to the plain of Zaanaim, which is by Kedesh.
Heberi (Mkeni) alijitenganisha na Wakeni - walikuwa wazao wa Hobabu (mkwe wa Musa) - na akaweka hema yake mwaloni uliopo huko Saanaimu karibu na Kedesh.
12 And they showed Sisera that Barak the son of Abinoam had gone up to mount Tabor.
Walipomwambia Sisera kwamba Baraka, mwana wa Abinoamu, alikuwa amekwenda mlima wa Tabori,
13 And Sisera gathered together all his chariots, even nine hundred chariots of iron, and all the people that were with him, from Harosheth of the Gentiles to the river of Kishon.
Sisera akawaita magari yake yote, magari ya farasi mia tisa, na askari wote waliokuwa pamoja naye, kutoka Haroshethi ya Mataifa mpaka Mto Kishoni.
14 And Deborah said to Barak, Arise; for this is the day when the LORD hath delivered Sisera into thy hand: hath not the LORD gone out before thee? So Barak went down from mount Tabor, and ten thousand men after him.
Debora akamwambia Baraka, Nenda! Kwa maana hii ndiyo siku ambayo Bwana amekupa ushindi juu ya Sisera. Je! si Bwana anayekuongoza? Basi Baraka akashuka kutoka mlima wa Tabori na watu kumi elfu wakamfuata.
15 And the LORD destroyed Sisera, and all his chariots, and all his host, with the edge of the sword before Barak; so that Sisera came down from his chariot, and fled away on his feet.
Bwana alifanya jeshi la Sisera kuchanganyikiwa, magari yake yote, na jeshi lake lote. Watu wa Baraka waliwashinda na Sisera akaanguka kutoka kwenye gari lake na kukimbia kwa miguu.
16 But Barak pursued the chariots, and the host, to Harosheth of the Gentiles: and all the host of Sisera fell upon the edge of the sword; and there was not a man left.
Lakini Baraka akayafuata magari na jeshi mpaka Haroshethi ya Mataifa, na jeshi lote la Sisera likauawa kwa upanga, wala hakuna mtu aliyeokoka.
17 However Sisera fled away on his feet to the tent of Jael the wife of Heber the Kenite: for there was peace between Jabin the king of Hazor and the house of Heber the Kenite.
Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mpaka hema ya Yaeli, mkewe Heberi Mkeni; kwa sababu kulikuwa na amani kati ya Yabini mfalme wa Hazori, na nyumba ya Heberi Mkeni.
18 And Jael went out to meet Sisera, and said to him, Turn in, my lord, turn in to me; fear not. And when he had turned in to her into the tent, she covered him with a mantle.
Jaeli akatoka kumlaki Sisera, akamwambia, karibu, bwana wangu; karibu kwangu, wala usiogope. Basi akakaribia kwake, akaingia hemani kwake, naye akamvika bushuti.
19 And he said to her, Give me, I pray thee, a little water to drink; for I am thirsty. And she opened a bottle of milk, and gave him a drink, and covered him.
Akamwambia, Tafadhali nipe maji kidogo ninywe, kwa maana nina kiu. Alifungua mfuko wa ngozi ya maziwa akampa anywe, kisha akamfunika tena.
20 Again he said to her, Stand in the door of the tent, and it shall be, when any man doth come and enquire of thee, and say, Is there any man here? that thou shalt say, No.
Akamwambia, “Simama mlangoni pa hema. Ikiwa mtu atakuja na kukuuliza, 'Je, kuna mtu hapa?', Sema 'Hapana'.”
21 Then Jael Heber’s wife took a nail of the tent, and took an hammer in her hand, and went softly to him, and smote the nail into his temples, and fastened it into the ground: for he was fast asleep and weary. So he died.
Kisha Jaeli (mke wa Heberi) akachukua kigingi cha hema na nyundo mkononi mwake akamwendea kwa siri, kwa sababu alikuwa amelala usingizi mzito, naye akakitia kigingi cha hema upande wa kichwa chake akamchoma na kikapenya kushuka chini. Hivyo akafa.
22 And, behold, as Barak pursued Sisera, Jael came out to meet him, and said to him, Come, and I will show thee the man whom thou seekest. And when he came into her tent, behold, Sisera lay dead, and the nail was in his temples.
Baraka alipokuwa akimfuata Sisera, Jaeli alitoka kukutana naye akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Basi akaingia pamoja naye, tazama Sisera amekufa, na kigingi cha hema kando ya kichwa chake.
23 So God subdued on that day Jabin the king of Canaan before the children of Israel.
Basi siku hiyo Mungu alimshinda Jabin, mfalme wa Kanaani, mbele ya watu wa Israeli.
24 And the hand of the children of Israel prospered, and prevailed against Jabin the king of Canaan, until they had destroyed Jabin king of Canaan.
Uwezo wa watu wa Israeli ulikua na nguvu zaidi dhidi ya Jabin mfalme wa Kanaani, hata walipomwangamiza.

< Judges 4 >