< Job 8 >

1 Then answered Bildad the Shuhite, and said,
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 How long wilt thou speak these things? and how long shall the words of thy mouth be like a strong wind?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Doth God pervert judgment? or doth the Almighty pervert justice?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 If thy children have sinned against him, and he hath cast them away for their transgression;
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 If thou wouldest seek to God early, and make thy supplication to the Almighty;
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 If thou wert pure and upright; surely now he would awake for thee, and make the habitation of thy righteousness prosperous.
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 Though thy beginning was small, yet thy latter end should greatly increase.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 For enquire, I pray thee, of the former age, and prepare thyself to the search of their fathers:
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 (For we are but of yesterday, and know nothing, because our days upon earth are a shadow: )
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 Shall they not teach thee, and tell thee, and utter words out of their heart?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Can the rush grow without mire? can the flag grow without water?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 While it is still green, and not cut down, it withereth before any other herb.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 So are the paths of all that forget God; and the hypocrite’s hope shall perish:
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 Whose confidence shall be cut off, and whose trust shall be a spider’s web.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 He shall lean upon his house, but it shall not stand: he shall hold it fast, but it shall not endure.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 He is green before the sun, and his branch shooteth forth in his garden.
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 His roots are wrapped about the heap, and seeth the place of stones.
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 If he shall be destroyed from his place, then it shall deny him, saying, I have not seen thee.
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Behold, this is the joy of his way, and out of the earth shall others grow.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Behold, God will not cast away a perfect man, neither will he help the evildoers:
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 Till he shall fill thy mouth with laughing, and thy lips with rejoicing.
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 They that hate thee shall be clothed with shame; and the dwelling place of the wicked shall come to nought.
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.

< Job 8 >