< Job 11 >

1 Then answered Zophar the Naamathite, and said,
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Should not the multitude of words be answered? and should a man full of talk be justified?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Should thy lies make men hold their peace? and when thou mockest, shall no man make thee ashamed?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 For thou hast said, My doctrine is pure, and I am clean in thy eyes.
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 But O that God would speak, and open his lips against thee;
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 And that he would show thee the secrets of wisdom, that they are double to that which is! Know therefore that God exacteth of thee less than thy iniquity deserveth.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 Canst thou by searching find out God? canst thou find out the Almighty to perfection?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 It is as high as heaven; what canst thou do? deeper than hell; what canst thou know? (Sheol h7585)
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
9 The measure of it is longer than the earth, and broader than the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If he shall cut off, and shut up, or gather together, then who can hinder him?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For he knoweth vain men: he seeth wickedness also; will he not then consider it?
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 For vain man would be wise, though man is born like a wild donkey’s colt.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 If thou preparest thy heart, and stretchest out thy hands toward him;
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 If iniquity is in thy hand, put it far away, and let not wickedness dwell in thy tents.
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 For then shalt thou lift up thy face without spot; yea, thou shalt be steadfast, and shalt not fear:
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 Because thou shalt forget thy misery, and remember it as waters that pass away:
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 And thy age shall be clearer than the noonday; thou shalt shine forth, thou shalt be as the morning.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 And thou shalt be secure, because there is hope; yea, thou shalt dig about thee, and thou shalt take thy rest in safety.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 Also thou shalt lie down, and none shall make thee afraid; yea, many shall make suit to thee.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 But the eyes of the wicked shall fail, and they shall not escape, and their hope shall be as the giving up of the ghost.
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

< Job 11 >