< Genesis 7 >

1 And the LORD said to Noah, Come thou and all thy house into the ark; for thee have I seen righteous before me in this generation.
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2 Of every clean beast thou shalt take to thee by sevens, the male and his female: and of beasts that are not clean by two, the male and his female.
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3 Of fowls of the air also by sevens, the male and the female; to keep seed alive on the face of all the earth.
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4 For yet seven days, and I will cause it to rain upon the earth forty days and forty nights; and every living thing that I have made will I destroy from the face of the earth.
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
5 And Noah did according to all that the LORD commanded him.
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
6 And Noah was six hundred years old when the flood of waters was upon the earth.
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7 And Noah went in, and his sons, and his wife, and his sons’ wives with him, into the ark, because of the waters of the flood.
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8 Of clean beasts, and of beasts that are not clean, and of fowls, and of every thing that creepeth upon the earth,
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9 There went in two and two to Noah into the ark, the male and the female, as God had commanded Noah.
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
10 And it came to pass after seven days, that the waters of the flood were upon the earth.
Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
11 In the six hundredth year of Noah’s life, in the second month, the seventeenth day of the month, the same day were all the fountains of the great deep broken up, and the windows of heaven were opened.
Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
12 And the rain was upon the earth forty days and forty nights.
Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
13 In the same day entered Noah, and Shem, and Ham, and Japheth, the sons of Noah, and Noah’s wife, and the three wives of his sons with them, into the ark;
Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
14 They, and every beast after his kind, and all the cattle after their kind, and every creeping thing that creepeth upon the earth after his kind, and every fowl after his kind, every bird of every sort.
Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
15 And they went in to Noah into the ark, two and two of all flesh, in which is the breath of life.
Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
16 And they that entered, went in male and female of all flesh, as God had commanded him: and the LORD shut him in.
Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
17 And the flood was forty days upon the earth; and the waters increased, and bore up the ark, and it was lifted above the earth.
Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
18 And the waters prevailed, and were increased greatly upon the earth; and the ark moved upon the face of the waters.
Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
19 And the waters prevailed exceedingly upon the earth; and all the high hills, that were under the whole heaven, were covered.
Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
20 Fifteen cubits upward did the waters prevail; and the mountains were covered.
Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
21 And all flesh died that moved upon the earth, both of fowl, and of cattle, and of beast, and of every creeping thing that creepeth upon the earth, and every man:
Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
22 All in whose nostrils was the breath of life, of all that was on the dry land, died.
Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
23 And every living thing was destroyed which was upon the face of the ground, both man, and cattle, and the creeping things, and the fowl of heaven; and they were destroyed from the earth: and Noah only remained alive, and they that were with him in the ark.
Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
24 And the waters prevailed upon the earth an hundred and fifty days.
Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.

< Genesis 7 >

The Great Flood
The Great Flood