< Ezekiel 27 >

1 The word of the LORD came again to me, saying,
Tena neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Now, thou son of man, take up a lamentation for Tyre;
“Sasa wewe, mwanadamu, anza kuomboleza kuhusiana na Tiro,
3 And say to Tyre, O thou that dwelleth at the entrance of the sea, which art a merchant of the people for many isles, Thus saith the Lord GOD; O Tyre, thou hast said, I am of perfect beauty.
na mwambie Tiro, aishiye kwenye malango ya bahari, manahodha wa watu hata visiwa vingi, Bwana Yahwe asema hivi kwako: Tiro, umesema, mimi ni ukamilifu katika uzuri.'
4 Thy borders are in the midst of the seas, thy builders have perfected thy beauty.
Mipaka yako iko kwenye moyo wa bahari; majengo yako yamekamilisha uzuri wako.
5 They have made all thy ship planks of fir trees of Senir: they have taken cedars from Lebanon to make masts for thee.
Wametengeneza mbao nene na pana kwa mvinje kutoka Mlima Hermoni; wamechukua mkangazi kutoka Lebanoni kuufanya mlingoti.
6 Of the oaks of Bashan have they made thy oars; the company of the Ashurites have made thy benches of ivory, brought out of the isles of Chittim.
Wametengeneza makasia yako kutoka kwenye mialo ya Bashani; wametengeza sitaha zako kwa mbao za mvinje kutoka Kitimu, na wametengeneza kwa pembe.
7 Fine linen with embroidered work from Egypt was that which thou spreadest forth to be thy sail; blue and purple from the isles of Elishah was that which covered thee.
Tanga zako zilikuwa za rangi za kitani kutoka Misri ambazo zilikuwa kama beramu!
8 The inhabitants of Zidon and Arvad were thy mariners: thy wise men, O Tyre, that were in thee, were thy pilots.
Wale waliokuwa wakiishi Sidoni na Arvadi walikuwa wavuta makasia wako; wenye busara wa Tire walikuwa ndani yenu; walikuwa marubani wako.
9 The ancients of Gebal and her wise men were in thee thy calkers: all the ships of the sea with their mariners were in thee to exchange thy merchandise.
Mafundistadi wenye uzoefu wa hali ya juu kutoka Gabeli walijaza mishono; meli zote za bahari na mabaharia wao miongoni mwenu walikuwa wakiwabeba manahodha kwaajili ya biashara.
10 They of Persia and of Lud and of Phut were in thy army, thy men of war: they hung the shield and helmet in thee; they set forth thy comeliness.
Uajemi, Ludi, na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walining'iniza ngao na chapeo ndani yako; walionyesha uzuri wako.
11 The men of Arvad with thy army were upon thy walls on all sides, and the Gammadims were in thy towers: they hung their shields upon thy walls on every side; they have made thy beauty perfect.
Watu wa Arvadi na Heleki katika jeshi lako walikuwa juu ya kuta zako wamekuzunguka, na watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walinin'giniza juu ngao zao juu ya kuta zako zote zilizokuzunguka! Wakaukamilisha uzuri wako.
12 Tarshish was thy merchant by reason of the multitude of all kind of riches; with silver, iron, tin, and lead, they traded in thy fairs.
Tarshishi alikuwa mdau wa biashara pamoja nawe kwa sababu ya wingi wa utajiri wako wa kuuza mizigo: fedha, chuma, bati, na risasi. Walinunua na kuuza bidhaa za biashara!
13 Javan, Tubal, and Meshech, they were thy merchants: they traded in the persons of men and vessels of brass in thy market.
Yavani, Tubali, na Mesheki-waliwauza watumwa na katika vitu kutengeneza shaba. Walibeba bidhaa zako.
14 They of the house of Togarmah traded in thy fairs with horses and horsemen and mules.
Beth Togarma waliandaa farasi, farasi dume, na nyumbu kama kama bidhaa zako.
15 The men of Dedan were thy merchants; many isles were the merchandise of thy hand: they brought thee for a present horns of ivory and ebony.
Watu wa Dedani walikuwa wafanya biashara wako kwenye pwani nyingi. Bidhaa zilikuwa mkononi mwako; walikutumia pembe, pembe za ndovu, na mpingo kama ushuru!
16 Syria was thy merchant by reason of the multitude of the wares of thy making: they traded in thy fairs with emeralds, purple, and embroidered work, and fine linen, and coral, and agate.
Shamu alikuwa mchuuzi katika bidhaa zako nyingi; waliandaa zumaridi, zambarau, nguo zenye rangi mbali mbali, kitambaa kizuri, lulu, na kito chekundu cha thamani kama bidhaa zako.
17 Judah, and the land of Israel, they were thy merchants: they traded in thy market in wheat of Minnith, and Pannag, and honey, and oil, and balm.
Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe. Waliandaa ngano kutoka Minithi, keki, asali, mafuta, na lihamu kama bidhaa zako.
18 Damascus was thy merchant in the multitude of the wares of thy making, for the multitude of all riches; in the wine of Helbon, and white wool.
Dameski alikuwa mfanya biashara wa bidhaa zako zote, za utajiri mkubwa mno, na ya divai ya Helboni na sufu ya Zahari.
19 Dan also and Javan going to and fro traded in thy fairs: bright iron, cassia, and calamus, were in thy market.
Dani na Yavani kutoka Uzali walikwandalia bidhaa ya chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai. Hivi vikawa bidhaa yako.
20 Dedan was thy merchant in precious clothes for chariots.
Dedani alikuwa mchuuzi katika nguo nzuri za kutandika.
21 Arabia, and all the princes of Kedar, they traded with thee in lambs, and rams, and goats: in these were they thy merchants.
Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe; walikuandalia wanakondoo, kondoo dume na mbuzi.
22 The merchants of Sheba and Raamah, they were thy merchants: they traded in thy fairs with the best of all spices, and with all precious stones, and gold.
Wafanya biashara wa Sheba na Raama walikuja kukuuzia kila aina ya viungo vizuri katika vito vyote vya thamani; waliuza dhahabu kwa ajili ya bidhaa.
23 Haran, and Canneh, and Eden, the merchants of Sheba, Asshur, and Chilmad, were thy merchants.
Harani, Kane, na Adina walikuwa wafanya biashara pamoja nawe, karibu na Sheba, Ashuru, na Kilmadi.
24 These were thy merchants in all sorts of things, in blue clothes, and embroidered work, and in chests of rich apparel, bound with cords, and made of cedar, among thy merchandise.
Hawa walikuwa wachuuzi wako mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi zilibuniwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri katika sehemu zako za soko.
25 The ships of Tarshish did sing of thee in thy market: and thou wast replenished, and made very glorious in the midst of the seas.
Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara ya bidhaa yako! Hivyo ulijaa, shehena nzito katika moyo wa bahari!
26 Thy rowers have brought thee into great waters: the east wind hath broken thee in the midst of the seas.
Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno; upepo wa mashariki umekuvunja kati yao.
27 Thy riches, and thy fairs, thy merchandise, thy mariners, and thy pilots, thy calkers, and the traders of thy merchandise, and all thy men of war, that are in thee, and in all thy company which is in the midst of thee, shall fall into the midst of the seas in the day of thy ruin.
Utajiri wako, bidhaa, na mizigo ya biashara; wapiga makasia wako na marubani, na waunzi wa meli; wafanya biashara wako wa bidhaa na watu wote wa vita walio ndani yako, na jeshi lako-watazama kwenye kina cha bahari siku ya kuangamia kwako.
28 The waves shall shake at the sound of the cry of thy pilots.
Miji iliyopo kwenye bahari sauti itatetemeka kulia kwa rubani zako;
29 And all that handle the oar, the mariners, and all the pilots of the sea, shall come down from their ships, they shall stand upon the land;
Wote wavutao kasia watashuka chini kutoka meli katika zao; wanamaji na marubani wote juu ya bahari watasimama juu ya nchi.
30 And shall cause their voice to be heard against thee, and shall cry bitterly, and shall cast up dust upon their heads, they shall wallow themselves in the ashes:
Kisha watakufanya kusikiliza sauti yao na kulia kwa uchungu; watarusha vumbi juu ya vichwa vyao. Watabingirika katika majivu.
31 And they shall make themselves utterly bald for thee, and gird themselves with sackcloth, and they shall weep for thee with bitterness of heart and bitter wailing.
Watanyo vichwa vyao upara kwa ajili yako na kujifunga wenyewe kwa nguo za magunia, na watalia kwa sauti.
32 And in their wailing they shall take up a lamentation for thee, and lament over thee, saying, What city is like Tyre, like the destroyed in the midst of the sea?
Watakuinulia maombolezo ya kuomboleza kwa ajili yako na kuimba nyimbo za maombolezo juu yako, ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa kati ya bahari?
33 When thy wares went forth out of the seas, thou didst fill many people; thou didst enrich the kings of the earth with the multitude of thy riches and of thy merchandise.
Wakati bidhaa yako ilipoenda ufukweni kutoka kwenye bahari, imewarithisha watu wengi; uliwatajirisha wafalme wa dunia kwa wingi wa utajiri wako mkubwa na bidhaa!
34 In the time when thou shalt be broken by the seas in the depths of the waters thy merchandise and all thy company in the midst of thee shall fall.
Lakini wakati ulipo vunjwavunjwa kwa bahari, kwa vilindi vya maji, bidhaa yako na wafanya kazi wako wote kuzama!
35 All the inhabitants of the isles shall be astonished at thee, and their kings shall be terribly afraid, they shall be troubled in their countenance.
Wote wakaao pwani walikuogopa, na wafalme wao kuvunjwa vunjwa katika kitisho! Nyuso zao zimetetemeka!
36 The merchants among the people shall hiss at thee; thou shalt be a terror, and never shalt be any more.
Wafanya biashara wa meli wa watu wakuzomea; umekuwa tishio, na hutakuwepo tena milele.”

< Ezekiel 27 >