< Ezekiel 27 >

1 The word of the LORD came again to me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 Now, thou son of man, take up a lamentation for Tyre;
“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
3 And say to Tyre, O thou that dwelleth at the entrance of the sea, which art a merchant of the people for many isles, Thus saith the Lord GOD; O Tyre, thou hast said, I am of perfect beauty.
Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
4 Thy borders are in the midst of the seas, thy builders have perfected thy beauty.
Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
5 They have made all thy ship planks of fir trees of Senir: they have taken cedars from Lebanon to make masts for thee.
Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
6 Of the oaks of Bashan have they made thy oars; the company of the Ashurites have made thy benches of ivory, brought out of the isles of Chittim.
Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
7 Fine linen with embroidered work from Egypt was that which thou spreadest forth to be thy sail; blue and purple from the isles of Elishah was that which covered thee.
Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
8 The inhabitants of Zidon and Arvad were thy mariners: thy wise men, O Tyre, that were in thee, were thy pilots.
Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
9 The ancients of Gebal and her wise men were in thee thy calkers: all the ships of the sea with their mariners were in thee to exchange thy merchandise.
Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
10 They of Persia and of Lud and of Phut were in thy army, thy men of war: they hung the shield and helmet in thee; they set forth thy comeliness.
“‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
11 The men of Arvad with thy army were upon thy walls on all sides, and the Gammadims were in thy towers: they hung their shields upon thy walls on every side; they have made thy beauty perfect.
Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
12 Tarshish was thy merchant by reason of the multitude of all kind of riches; with silver, iron, tin, and lead, they traded in thy fairs.
“‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
13 Javan, Tubal, and Meshech, they were thy merchants: they traded in the persons of men and vessels of brass in thy market.
“‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
14 They of the house of Togarmah traded in thy fairs with horses and horsemen and mules.
“‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
15 The men of Dedan were thy merchants; many isles were the merchandise of thy hand: they brought thee for a present horns of ivory and ebony.
“‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
16 Syria was thy merchant by reason of the multitude of the wares of thy making: they traded in thy fairs with emeralds, purple, and embroidered work, and fine linen, and coral, and agate.
“‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
17 Judah, and the land of Israel, they were thy merchants: they traded in thy market in wheat of Minnith, and Pannag, and honey, and oil, and balm.
“‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
18 Damascus was thy merchant in the multitude of the wares of thy making, for the multitude of all riches; in the wine of Helbon, and white wool.
“‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
19 Dan also and Javan going to and fro traded in thy fairs: bright iron, cassia, and calamus, were in thy market.
“‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
20 Dedan was thy merchant in precious clothes for chariots.
“‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
21 Arabia, and all the princes of Kedar, they traded with thee in lambs, and rams, and goats: in these were they thy merchants.
“‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
22 The merchants of Sheba and Raamah, they were thy merchants: they traded in thy fairs with the best of all spices, and with all precious stones, and gold.
“‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
23 Haran, and Canneh, and Eden, the merchants of Sheba, Asshur, and Chilmad, were thy merchants.
“‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
24 These were thy merchants in all sorts of things, in blue clothes, and embroidered work, and in chests of rich apparel, bound with cords, and made of cedar, among thy merchandise.
Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
25 The ships of Tarshish did sing of thee in thy market: and thou wast replenished, and made very glorious in the midst of the seas.
“‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
26 Thy rowers have brought thee into great waters: the east wind hath broken thee in the midst of the seas.
Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
27 Thy riches, and thy fairs, thy merchandise, thy mariners, and thy pilots, thy calkers, and the traders of thy merchandise, and all thy men of war, that are in thee, and in all thy company which is in the midst of thee, shall fall into the midst of the seas in the day of thy ruin.
Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
28 The waves shall shake at the sound of the cry of thy pilots.
Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
29 And all that handle the oar, the mariners, and all the pilots of the sea, shall come down from their ships, they shall stand upon the land;
Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
30 And shall cause their voice to be heard against thee, and shall cry bitterly, and shall cast up dust upon their heads, they shall wallow themselves in the ashes:
Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
31 And they shall make themselves utterly bald for thee, and gird themselves with sackcloth, and they shall weep for thee with bitterness of heart and bitter wailing.
Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
32 And in their wailing they shall take up a lamentation for thee, and lament over thee, saying, What city is like Tyre, like the destroyed in the midst of the sea?
Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
33 When thy wares went forth out of the seas, thou didst fill many people; thou didst enrich the kings of the earth with the multitude of thy riches and of thy merchandise.
Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
34 In the time when thou shalt be broken by the seas in the depths of the waters thy merchandise and all thy company in the midst of thee shall fall.
Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
35 All the inhabitants of the isles shall be astonished at thee, and their kings shall be terribly afraid, they shall be troubled in their countenance.
Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
36 The merchants among the people shall hiss at thee; thou shalt be a terror, and never shalt be any more.
Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”

< Ezekiel 27 >