< Ezekiel 16 >

1 Again the word of the LORD came to me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Son of man, cause Jerusalem to know her abominations,
“Mwanadamu, mwambie Yerusalemu kuhusu machukizo yake,
3 And say, Thus saith the Lord GOD to Jerusalem; Thy birth and thy nativity is of the land of Canaan; thy father was an Amorite, and thy mother an Hittite.
na useme, 'Bwana Yahwe asema hivi kwa Yerusalemu: Mwanzo wako na kuzaliwa kwako kulichukua nafasi katika nchi ya Kanaani; baba yako alikuwa Mwamori, na mama yako alikuwa Mhiti.
4 And as for thy nativity, in the day thou wast born thy navel was not cut, neither wast thou washed in water to cleanse thee; thou wast not salted at all, nor swaddled at all.
Katika siku ya kuzaliwa kwako, mama yako hakukata kitovu chako, wala hakukuosha kwenye maji usafishwe au kukuchua kwa chumvi, wala kukusitiri nguo.
5 No eye pitied thee, to do any of these to thee, to have compassion upon thee; but thou wast cast out in the open field, to the lothing of thy person, in the day that thou wast born.
Hakuna jicho lililokuhurumia kufanya haya mambo kwa ajili yako, kukuhurumia wewe. Katika siku uliyozaliwa, kwa kuchukiwa uhai wako, ulitupwa nje uwandani.
6 And when I passed by thee, and saw thee polluted in thy own blood, I said to thee when thou wast in thy blood, Live; yea, I said to thee when thou wast in thy blood, Live.
Lakini nilipita karibu nawe, nalikuona ukijinyonga kwa damu yako mwenyewe, “kubaki hai!”
7 I have caused thee to multiply as the bud of the field, and thou hast increased and become great, and thou art come to excellent ornaments: thy breasts are fashioned, and thy hair is grown, though thou wast naked and bare.
Nimekufanya ukue kama mmea katika shamba. Umeongezeka na kuwa mkubwa, na umekuwa mzuri wa wazuri. Maziwa yako yakawa thabiti, na nywele zako zikawa nyingi, ingawa ulikuwa uchi huna nguo.
8 Now when I passed by thee, and looked upon thee, behold, thy time was the time of love; and I spread my skirt over thee, and covered thy nakedness: yea, I swore to thee, and entered into a covenant with thee, saith the Lord GOD, and thou becamest mine.
Nilipita karibu nawe tena, na nalikuona. Tazama! wakati wa upendo umefika kwako, hivyo nikatandika joho langu juu yako na kufunika uchi wako. Kisha nikaapa kwako na kukuleta kwenye agano-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na ukawa wangu.
9 Then I washed thee with water; yea, I thoroughly washed away thy blood from thee, and I anointed thee with oil.
Basi nilikuosha kwa maji na kukufuta damu yako, na kukupaka mafuta.
10 I clothed thee also with embroidered work, and shod thee with badgers’ skin, and I girded thee with fine linen, and I covered thee with silk.
Nilikuvalisha nguo ya taraza na kukuwekea makuzi ya ngozi kwenye miguu yako. Nilikufungia kwa kitani kizuri na kukufunika kwa hariri.
11 I decked thee also with ornaments, and I put bracelets upon thy hands, and a chain on thy neck.
Kisha nalikupamba kwa vito, na kukuvalisha vikuku kwenye mikono yako, na mkufu kwenye shingo yako.
12 And I put a jewel on thy forehead, and earrings in thy ears, and a beautiful crown upon thy head.
Nalitia hazama katika pua yako na hereni katika masikio yako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
13 Thus wast thou decked with gold and silver; and thy raiment was of fine linen, and silk, and embroidered work; thou didst eat fine flour, and honey, and oil: and thou wast exceeding beautiful, and thou didst prosper into a kingdom.
Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha, na ulivaa kitani safi, hariri, na ngu za taraza; ulikula unga mzuri, asali, na mafuta, na ulikuwa mzuri sana, na ukawa malkia.
14 And thy renown went forth among the heathen for thy beauty: for it was perfect through my comeliness, which I had put upon thee, saith the Lord GOD.
Umaarufu wako ukaenda miongoni mwa mataifa kwa sababu ya uzuri wako, kwa kuwa ulikuwa mkamili katika ukuu niliokuwa nimekupa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 But thou didst trust in thy own beauty, and didst play the harlot because of thy renown, and didst pour out thy harlotries on every one that passed by; his it was.
Lakini ulitumaini uzuri wako, na ukafanya kama kahaba kwa sababu ya umaarufu wako; umeyamwaga matendo yako ya kikahaba kwa kila aliyepita karibu, ili kwamba uzuri wako uwe wake.
16 And of thy garments thou didst take, and didst deck thy high places with various colours, and didst play the harlot upon them: the like things shall not come, neither shall it be so.
Kisha ulichukua nguo zako na pamoja nao umepatengeneza mahali pa juu kwa ajili yako palipambwa kwa rangi tofauti tofauti, na hapo ulifanya kama kahaba. Hii haitatokea. Wala haitatokea.
17 Thou hast also taken thy fair jewels of my gold and of my silver, which I had given thee, and hast made to thyself images of men, and hast committed harlotry with them,
Umevichukua vito vizuri vya dhahabu na fedha nilizowapatia, na umejitengenezea sanamu za wanaume, na umefanya pamoja nao ukahaba afanyao.
18 And hast taken thy embroidered garments, and didst cover them: and thou hast set my oil and my incense before them.
Ulichukua nguo zako za tarizi na kuwafunika, na kuwawekea mafuta yangu na manukato mbele yao.
19 My food also which I gave thee, fine flour, and oil, and honey, with which I fed thee, thou hast even set before them for a sweet savour: and thus it was, saith the Lord GOD.
Mkate wangu niliokupatia-ulitengenezwa kwa unga mzuri, mafuta, na asali-umeviweka mbele yao kwa ajili ya kunukia harufu nzuri, kwa kuwa hivi ndivyo ilivyotokea-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
20 Moreover thou hast taken thy sons and thy daughters, whom thou hast borne to me, and these hast thou sacrificed to them to be devoured. Is this of thy harlotries a small matter,
Kisha uliwachukua watoto wako ulionizalia, na kuwatoa sadaka kwa picha ili waliwe kama chakula. Je! matendo yako ya kikahaba ni kitu kidogo?
21 That thou hast slain my children, and delivered them to cause them to pass through the fire for them?
Umewachinja watoto wangu na kuwatupia kwenye moto.
22 And in all thy abominations and thy harlotries thou hast not remembered the days of thy youth, when thou wast naked and bare, and wast polluted in thy blood.
Katika machukizo yako yote na matendo yako ya kikahaba hukutafakari kuhusu siku za ujana wako, wakati ulipokuwa uchi na bila nguo kama kama umepigwa katika damu.
23 And it came to pass after all thy wickedness, woe, ( woe to thee! saith the Lord GOD; )
Ole! Ole wako! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwahiyo, zaidi ya hapo kwa haya maovu yote,
24 That thou hast also built to thee an eminent place, and hast made thee an high place in every street.
umejijengea chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi.
25 Thou hast built thy high place at every head of the way, and hast made thy beauty to be abhorred, and hast offered thyself to every one that passed by, and multiplied thy harlotries.
Umepajenga mahali pako palipoinuka kwenye kichwa cha kila njia na kuunajisi uzuri wako, kwa kuwa umeutoa mwili wako kwa kila mtu apitaye karibu na umefanya matendo mengi zaidi ya ukahaba.
26 Thou hast also committed harlotry with the Egyptians thy neighbours, great of flesh; and hast multiplied thy harlotry, to provoke me to anger.
Umetenda kama kahaba pamoja na Wamisri, tamaa ya jirani zako, na umetenda matendo mengi zaidi ya kikahaba, ili kuchochea hasira yangu.
27 Behold, therefore I have stretched out my hand over thee, and have diminished thy ordinary food, and delivered thee to the will of them that hate thee, the daughters of the Philistines, who are ashamed of thy lewd way.
Tazama! Nitakunyooshea mkono wangu na kupunguza chakula chako. Nitauchukua uhai wako juu ya adui zako, binti za Wafilisti, ambao walikuwa na haya ya tabia yako ya uchafu.
28 Thou hast played the harlot also with the Assyrians, because thou wast not satisfied; yea, thou hast played the harlot with them, and yet couldest not be satisfied.
Umetenda kama kahaba pamoja na Waashuru kwa sababu hukuweza kuridhika. Umetenda kama kahaba na bado hukuridhika.
29 Thou hast moreover multiplied thy harlotry in the land of Canaan to Chaldea; and yet with this thou wast not satisfied.
Umefanya matendo mengi zaidi ya kikahaba katika nchi ya jamii ya wana maji wa Ukaldayo, na wala hukuridhika kwa hayo.
30 How weak is thy heart, saith the Lord GOD, seeing thou doest all these things, the work of an imperious harlot;
Jinsi moyo wako ulivyo dhaifu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwamba utaweza kuyafanya haya mambo yote, matendo ya aibu ya kikahaba?
31 In that thou buildest thy eminent place in the head of every way, and makest thy high place in every street; and hast not been as an harlot, in that thou scornest hire;
Mmepajenga mahali penu pa juu kwenye kichwa cha kila mtaa na kufanya chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi. Bado hukuwa kama kahaba kwa sababu ulikataa kulipwa ujira.
32 But as a wife that committeth adultery, who taketh strangers instead of her husband!
Wewe mwanamke mzinifu, wewe upokeaye wageni badala ya mume wako.
33 They give gifts to all harlots: but thou givest thy gifts to all thy lovers, and hirest them, that they may come to thee on every side for thy harlotry.
Watu hulipa kwa kila kahaba, lakini wewe huwapa mshara wako wapenzi wako wote na kuwapa rushwa ili waje kwako pande zote kwa matendo yako ya kikahaba.
34 And thou art the opposite from other women in thy harlotries, though none followeth thee to commit harlotries: and in that thou givest a reward, and no reward is given to thee, therefore thou art the opposite.
Hivyo kuna tofauti kati yako na hao wanawake wengine, kwa kuwa hakuna hata mmoja ajaye kwako kukuuliza kulala pamoja nao. Badala yake, unawalipa. Hakuna akulipaye.
35 Therefore, O harlot, hear the word of the LORD:
Kwa hiyo, wewe kahaba, lisikilize neno la Yahwe.
36 Thus saith the Lord GOD; Because thy filthiness was poured out, and thy nakedness uncovered through thy harlotries with thy lovers, and with all the idols of thy abominations, and by the blood of thy children, which thou didst give to them;
Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umemwaga tamaa yako na kuonyesha sehemu zako za siri kupitia matendo yako ya ukahaba pamoja na wapenzi wako wote pamoja na sanamu zako za chukizo, na kwa sababu ya damu ya watoto wako uliyowapatia sanamu zako,
37 Behold, therefore I will gather all thy lovers, with whom thou hast taken pleasure, and all them that thou hast loved, with all them that thou hast hated; I will even gather them on every side against thee, and will uncover thy nakedness to them, that they may see all thy nakedness.
kwa hiyo, tazama! Nitawakusanya wapenzi wako wote uliokutana nao, wote ambao uliowapenda na wote uliowachukia, na nitawakusanya juu yako kila upande. Nitawaonyesha wazi sehemu zako za siri hivyo wanaweza kuona uchi wako wote.
38 And I will judge thee, as women that break wedlock and shed blood are judged; and I will give thee blood in fury and jealousy.
Kwa kuwa nitakuadhibu kwa uasherati na kumwaga damu, na nitaleta juu yako damu ya hasira yangu na hasira kali.
39 And I will also give thee into their hand, and they shall throw down thy eminent place, and shall break down thy high places: they shall strip thee also of thy clothes, and shall take thy fair jewels, and leave thee naked and bare.
Nitakutia kwenye mikono yao hivyo watakutupa chini kwenye chumba cha chini kwa chini na kupavunja mahali pako pa juu na watakuvua nguo zako na kuchukua vito vyako vyote. watakuacha uchi bila nguo.
40 They shall also bring up a company against thee, and they shall stone thee with stones, and thrust thee through with their swords.
Kisha wataleta kundi la watu juu yako na kukupiga kwa mawe, na kukukata kwa panga zao.
41 And they shall burn thy houses with fire, and execute judgments upon thee in the sight of many women: and I will cause thee to cease from playing the harlot, and thou also shalt give no hire any more.
Watachoma nyumba zako na kufanya matendo mengi ya adhabu juu yako kwenye uso wa wanawake wengi, kwa kuwa nitakusimamisha ukahaba wako, na hutawalipa tena wapenzi wako.
42 So will I make my fury toward thee to rest, and my jealousy shall depart from thee, and I will be quiet, and will be no more angry.
Kisha nitatuliza ghadhabu yangu juu yako; hasira yangu itakuacha, kwa kuwa nitaridhika, na sitakuwa na hasira tena.
43 Because thou hast not remembered the days of thy youth, but hast provoked me in all these things; behold, therefore I also will recompense thy way upon thy head, saith the Lord GOD: and thou shalt not commit this lewdness above all thy abominations.
Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako na kunifanya nitetemeke kwa hasira kwa sababu ya haya mambo yote, kwa hiyo, tazama! Mimi mwenyewe nitashusha kwa kichwa chako mwenyewe adhabu kwa kile ulichokifanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Hutaongeza ukahaba kwa matendo yako yote ya machukizo?
44 Behold, every one that useth proverbs shall use this proverb against thee, saying, As is the mother, so is her daughter.
Tazama! Kila mtu azungumzaye Mithali kuhusu wewe atasema, “Kama alivyo, hivyo pia ni binti yake.”
45 Thou art thy mother’s daughter, that lotheth her husband and her children; and thou art the sister of thy sisters, who lothed their husbands and their children: your mother was an Hittite, and your father an Amorite.
Wewe ni binti wa mama yako, amchukiaye mume wake na mtoto wake, na wewe ni dada wa dada zako aliyewachukia waume zao na watoto wao. Mama yako alikuwa Mhiti, na baba yako alikuwa Mwamori.
46 And thy elder sister is Samaria, she and her daughters that dwell at thy left hand: and thy younger sister, that dwelleth at thy right hand, is Sodom and her daughters.
Dada yako mkubwa alikuwa Samaria na binti zake walikuwa wale waliokuwa wakiishi kaskazini, wakati dada yako mdogo alikuwa ni yule aliyekuwa akiishi kusini mwako, ambaye ni, Sodoma na binti zake.
47 Yet hast thou not walked after their ways, nor done after their abominations: but, as if that were a very little thing, thou wast corrupted more than they in all thy ways.
Hukuenenda katika njia zao na kuchukua tabia zao na matendo yao, lakini katika njia zako zote ulikuwa mbaya zaidi kuliko walivyokuwa wao.
48 As I live, saith the Lord GOD, Sodom thy sister hath not done, she nor her daughters, as thou hast done, thou and thy daughters.
Kama niishivyo- hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-dada yako Sodoma na binti zake, hawajafanya uovu mwingi kama wewe ulivyofanya na binti zako walivyofanya.
49 Behold, this was the iniquity of thy sister Sodom, pride, fulness of bread, and abundance of idleness was in her and in her daughters, neither did she strengthen the hand of the poor and needy.
Tazama! Hii ilikuwa dhambi ya dada yako Sodoma: Alikuwa na kiburi katika mafanikio yake, uzembe na kutojali kuhusu chochote. Hakuitia nguvu mikono ya maskini na watu wahitaji.
50 And they were haughty, and committed abomination before me: therefore I took them away as I saw good.
Alikuwa na kiburi na kufanya machukizo mbele yangu, hivyo niliwatoa kama nilivyoona.
51 Neither hath Samaria committed half of thy sins; but thou hast multiplied thy abominations more than they, and hast justified thy sisters in all thy abominations which thou hast done.
Samaria hakufanya hata nusu ya dhambi zako; badala yake, umefanya machukizo mengi kuliko walivyofanya, na umewonyesha hayo dada zako walikuwa bora kuliko wewe kwa sababu ya machukizo yako uyafanyayo!
52 Thou also, who hast judged thy sisters, bear thy own shame for thy sins that thou hast committed more abominable than they: they are more righteous than thou: yea, be thou confounded also, and bear thy shame, in that thou hast justified thy sisters.
Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe; kwa njia hii umewaonyesha dada zako walikuwa bora kuliko wewe, kwa sababu ya dhambi ulizozifanya katika hayo machukizo yako yote. Dada zako sasa wanaonekana bora kuliko wewe. Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe, kwa njia hii umewaonyesha kwamba dada zako walikuwa bora kuliko wewe.
53 When I shall bring again their captivity, the captivity of Sodom and her daughters, and the captivity of Samaria and her daughters, then will I bring again the captivity of thy captives in the midst of them:
Kwa kuwa nitarudisha masalia wao-masalia ya Sodoma na binti zake, na masalia ya Samaria na binti zake; lakini masalia yako yatakuwa miongoni mwao.
54 That thou mayest bear thy own shame, and mayest be confounded in all that thou hast done, in that thou art a comfort to them.
Kwa kufikiria haya mambo utaonyesha aibu yako; utakuwa mnyenyekevu kwa sababu ya kila kitu ulichokifanya, na kwa njia hii utakuwa faraja kwao.
55 When thy sisters, Sodom and her daughters, shall return to their former state, and Samaria and her daughters shall return to their former state, then thou and thy daughters shall return to your former state.
Hivyo dada yako Sodoma na binti zake watarudishwa kwenye hali yao ya zamani, na Samaria na binti zake watarudishwa kwenye mashamba yao ya zamani. Kisha wewe na binti zako watarudishwa kwenye hali yako ya kawaida.
56 For thy sister Sodom was not mentioned by thy mouth in the day of thy pride,
Sodoma dada yako hakutajwa hata kwa kinywa chako katika siku ulipojiinua,
57 Before thy wickedness was discovered, as at the time of thy reproach of the daughters of Syria, and all that are around her, the daughters of the Philistines, who despise thee on every side.
kabla uovu wako haujafunuliwa. Lakini sasa wewe ni kitu cha dharau kwa binti za Edomu na binti wote wa Wafilisti waliomzunguka. Watu wote wanakudharau wewe.
58 Thou hast borne thy lewdness and thy abominations, saith the LORD.
Utaonyesha aibu yako na matendo yako ya machukizo! -hivi ndivyo Yahwe asemavyo!
59 For thus saith the Lord GOD; I will even deal with thee as thou hast done, who hast despised the oath in breaking the covenant.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitashughulika na wewe kama unavyostahili, wewe uliyedharau kiapo chako kwa kulivunja agano.
60 Nevertheless I will remember my covenant with thee in the days of thy youth, and I will establish to thee an everlasting covenant.
Lakini mimi mwenyewe nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe katika siku za ujana wako, nitaliimarisha agano la milele pamoja na wewe.
61 Then thou shalt remember thy ways, and be ashamed, when thou shalt receive thy sisters, thy elder and thy younger: and I will give them to thee for daughters, but not by thy covenant.
Kisha utazikumbuka njia zako na kuona aibu utakapo wapokea dada zako wakubwa na dada zako wadogo. Nitakupatia wao kama binti zako, lakini kwa sababu ya agano lako.
62 And I will establish my covenant with thee; and thou shalt know that I am the LORD:
Mimi nitaweka imara agano lango pamoja nawe, nawe utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
63 That thou mayest remember, and be confounded, and never open thy mouth any more because of thy shame, when I am pacified toward thee for all that thou hast done, saith the Lord GOD.
Kwa sababu ya haya mambo, utakumbuka kila kitu na kuona aibu, hutafungua mdomo wako tena kuongea kwa sababu ya aibu yako, wakati nitakapokusamehe kwa yale yote uliyoyafanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'

< Ezekiel 16 >