< Exodus 35 >

1 And Moses gathered all the congregation of the children of Israel together, and said to them, These are the words which the LORD hath commanded, that ye should do them.
Musa akawakusanya jamii yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndio mambo Yahweh aliyo waamuru mfanye.
2 Six days shall work be done, but on the seventh day there shall be to you an holy day, a sabbath of rest to the LORD: whoever doth work in it shall be put to death.
Kwa siku sita kazi ya weza fanywa, lakini kwako, siku ya saba lazima iwe siku takatifu, siku ya Sabato ya mapumziko, takatifu kwa Yahweh. Yeyote atakaye fanya kazi hiyo siku lazima auawe.
3 Ye shall kindle no fire throughout your habitations upon the sabbath day.
Haupaswi kuwasha moto kwenye nyumba zenu siku ya Sabato.”
4 And Moses spoke to all the congregation of the children of Israel, saying, This is the thing which the LORD commanded, saying,
Musa akasema na jamii yote ya Waisraeli, kwa kusema, “Hichi ndicho kitu Yahweh alicho amuru.
5 Take ye from among you an offering to the LORD: whoever is of a willing heart, let him bring it, an offering of the LORD; gold, and silver, and brass,
Chukuwa sadaka kwa ajili ya Yahweh, wote wenye moyo mkunjufu. Leta sadaka kwa Yahweh - dhahabu, fedha, shaba,
6 And blue, and purple, and scarlet, and fine linen, and goats’ hair,
buluu, zambarau, sufu nyekundu na kitambaa kizuri; nywele za mbuzi;
7 And rams’ skins dyed red, and badgers’ skins, and shittim wood,
ngozi za kondoo zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za pomboo; na mbao za mshita;
8 And oil for the light, and spices for anointing oil, and for the sweet incense,
mafuta ya taa kwa pahali patakatifu, viungo vya manukato kwa hayo mafuta ya kutiwa,
9 And onyx stones, and stones to be set for the ephod, and for the breastplate.
kwa uvumba mzuri na vito vya shohamu na vito vya kutiwa kwa hiyo naivera, na kwa hicho kifuko cha kifuani.
10 And every wise hearted among you shall come, and make all that the LORD hath commanded;
Kila mwanaume mwenye ustadi kati yenu aje na afanye kila kitu ambacho Yahweh aliyaamuru —
11 The tabernacle, its tent, and its covering, its clasps, and its boards, its bars, its pillars, and its sockets,
hema la kuabudia, na kifuniko chake, na vifungo vyake, na mbao zake, nguzo, na sakafu;
12 The ark, and its staffs, with the mercy seat, and the veil of the covering,
pia sanduku na nguzo zake, kiti cha rehema, na pazia la kusitiri.
13 The table, and its staffs, and all its vessels, and the showbread,
Walileta meza na miguu yake, vyombo vyake vyote, na mkate wa wonyesho;
14 The lampstand also for the light, and its furniture, and its lamps, with the oil for the light,
kinara cha taa, vyombo vyake, taa, na mafuta ya zile taa;
15 And the incense altar, and its staffs, and the anointing oil, and the sweet incense, and the hanging for the door at the entrance of the tabernacle,
ile madhabahu ya uvumba na nguzo zake, mafuta ya upako na uvumba ulitiwa maukato; kishikizo cha mwingilio wa hema ya kuabudia;
16 The altar of burnt offering, with its brasen grate, its staffs, and all its vessels, the laver and its foot,
madhabahu ya sadaka ya kuteketeza na kitunzi cha shaba na nguzo na vyombo; na ile beseni kubwa na sakafu yake.
17 The hangings of the court, its pillars, and their sockets, and the hanging for the door of the court,
Walileta vishikizo kwa ajili ya nyuani na nguzo zake na sakafu yake, na pazia kwa ajili mwingilio wa nyauni;
18 The pins of the tabernacle, and the pins of the court, and their cords,
na ile misumari ya hema la kuabudia na nyuani, pamoja na kamba zake.
19 The cloths of service, to do service in the holy place, the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest’s office.
Walileta mavazi yaliyofumwa kutumikia sehemu takatifu, mavazi takatifu ya Aruni kuhani na wanae, kwa wao kutumika kama makuhani.”
20 And all the congregation of the children of Israel departed from the presence of Moses.
Kisha makabila yote ya Israeli yakaondoka na kwenda kutoka uweponi mwa Musa.
21 And they came, every one whose heart was stirred, and every one whom his spirit made willing, and they brought the LORD’S offering to the work of the tabernacle of the congregation, and for all his service, and for the holy garments.
Kila mtu moyo wake ulimchochea na aliye andaliwa na roho yake alikuja na kuleta sadaka kwa Yahweh kwa matengenezo ya hema ya kuabudia, kwa vitu vyote kwajili ya huduma ndani yake, na kwa vazi takatifu.
22 And they came, both men and women, as many as were willing hearted, and brought bracelets, and earrings, and rings, and necklaces, all jewels of gold: and every man that offered offered an offering of gold to the LORD.
Walikuja, wote wanaume kwa wanawake, wote waliokuwa na moyo wa utayari. Walileta madini, hereni, pete, na vitu vya thamani, vitu vyote tofauti vyenye madini ya dhahabu. Waliwasilisha sadaka za dhahabu kama sadaka ya kupunga kwa Yahweh.
23 And every man, with whom was found blue, and purple, and scarlet, and fine linen, and goats’ hair, and red skins of rams, and badgers’ skins, brought them.
Kila mmoja alikuwa na sufu ya buluu, dhambarau, au nyekundu, nguo nzuri, singa za mbuzi, ngozi za kondoo zilizobadili kuwa nyekundu, na ngozi ya pomboo walivileta.
24 Every one that offered an offering of silver and brass brought the LORD’S offering: and every man, with whom was found shittim wood for any work of the service, brought it.
kila mmoja alitengeneza sadaka ya fedha au shaba walizileta kama sadaka kwa Yahweh, na kila mmoja aliyekuwa na mti wa mshita kwa matumizi ya kazi aliuleta.
25 And all the women that were wise hearted spun with their hands, and brought that which they had spun, both of blue, and of purple, and of scarlet, and of fine linen.
kila mwanamke mwenye ustadi walisokota sufu kwa mikono yao na walileta sufu walizosokota za buluu, dhambarau, au sufu nyekundu, au nguo nzuri.
26 And all the women whose heart moved them in wisdom spun goats’ hair.
Wanawake wote wenye mioyo iliyochochewa na walio na ustadi walisokota singa za mbuzi.
27 And the rulers brought onyx stones, and stones to be set, for the ephod, and for the breastplate;
Viongozi walileta mawe ya shohamu na mawe mengine kwaajili ya kuwekwa kwenye hiyo naivera na hicho kifuko cha kifuani;
28 And spice, and oil for the light, and for the anointing oil, and for the sweet incense.
walileta viungo na mafuta kwaajili ya taa, kwa mafuta ya upako, na kwa uvumba wa manukato.
29 The children of Israel brought a willing offering to the LORD, every man and woman, whose heart made them willing to bring for all manner of work, which the LORD had commanded to be made by the hand of Moses.
Waisraeli walileta sadaka ya hiyari kwa Yahweh; kila mwanaume na mwanamke ambao mioyo yao ilikuwa tayari walileta vifaa kwaajili kazi zote ambazo Yahweh aliamuru kupitia Musa zifanyike.
30 And Moses said to the children of Israel, See, the LORD hath called by name Bezaleel the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah;
Musa alisema kwa waisraeli, “Tazama, Yahweh ameita kwa jina juu ya Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, kutoka kabila la Yuda.
31 And he hath filled him with the spirit of God, in wisdom, in understanding, and in knowledge, and in all manner of workmanship;
Aliijaza Bezaleli kwa Roho yake, kumpa hekima, uwelewa, na maarifa, kwa aina zote za ujenzi,
32 And to make beautifully wrought works, to work in gold, and in silver, and in brass,
kufanya sanaa ya ubunifu na kufanya kazi za dhahabu, shaba, na shaba;
33 And in the cutting of stones, to set them, and in carving of wood, to make any manner of skilful work.
pia kukata na kupanga mawe na mbao iliochongwa- kufanya kazi za aina zote kwa ubunifu na ujenzi.
34 And he hath put in his heart that he may teach, both he, and Aholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan.
Aliiweka kufundisha ndani ya moyo wake, yeye pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, kutoka kabila la Dani.
35 He hath filled them with wisdom of heart, to work all manner of work, of the engraver, and of the skilful workmen, and of the embroiderer, in blue, and in purple, in scarlet, and in fine linen, and of the weaver, even of them that do any work, and of those that make beautifully wrought work.
Aliwajaza kwa ustadi wa kufanya kazi za aina zote, kufanya kazi ya kama kuchora mawe, kama mwerevu, kama mtia taraza katika nyuzi za rangu ya buluu, dhambarau, na nyekundu na nguo nzuri, na kama washonaji. Walikuwa wachonga mawe wa kazi zote, na walikuwa wabunifu wa sanaa.

< Exodus 35 >