< Esther 5 >

1 Now it came to pass on the third day, that Esther put on her royal apparel, and stood in the inner court of the king’s house, opposite the king’s house: and the king sat upon his royal throne in the royal house, opposite the entrance of the house.
Baada ya siku tatu, Esta akajivika mavazi yake ya kimalkia na akasimama sehemu ya ndani ya ua wa ikulu ya mfalme, mbele ya nyumba ya mfalme. mfalme alikuwa ameketi katika kiti chake cha enzi na akitazama mlango wa kuingilia.
2 And it was so, when the king saw Esther the queen standing in the court, that she obtained favour in his sight: and the king held out to Esther the golden sceptre that was in his hand. So Esther drew near, and touched the top of the sceptre.
Mfalme alipomwona malkia Esta alipata kibali kwa mfalme. Alimpa fimbo ya dhahabu mikononi mwa Esta. Hivyo Esta akamsogelea mfalme na kuishika fimbo ya utawala.
3 Then said the king to her, What wilt thou, queen Esther? and what is thy request? it shall be even given thee to the half of the kingdom.
Kisha mfalme akamwambia Malkia Esta, “Unahitaji upewe nini? Ombi lako ni lipi? Hata nusu ya ufalme wangu utapewa.”
4 And Esther answered, If it shall seem good to the king, let the king and Haman come this day to the banquet that I have prepared for him.
Malkia Esta akamwambia mfalme, kama nimepata kibali machoni pako, naomba wewe na Hamani muhudhurie leo katika karamu niliyoiandaa kwa ajili yake.”
5 Then the king said, Cause Haman to make haste, that he may do as Esther hath said. So the king and Haman came to the banquet that Esther had prepared.
Mfalme akasema, “Mleteni haraka Hamani sawa sawa na matakwa ya Malkia Esta.” Mfalme pamoja na Hamani wakahuduria katika karamu aliyoandaa malkia Esta.
6 And the king said to Esther at the banquet of wine, What is thy petition? and it shall be granted thee: and what is thy request? even to the half of the kingdom it shall be performed.
Mvinyo ulipohudumiwa katika karamu, mfalme akamuuliza Malkia Esta hitaji lako ni nini? Na ombi lako ni lipi? Utapewa hata nusu ya ufalme.”
7 Then answered Esther, and said, My petition and my request is;
Esta akajibu mfalme, “Hitaji na ombi langu ni hili,
8 If I have found favour in the sight of the king, and if it shall please the king to grant my petition, and to perform my request, let the king and Haman come to the banquet that I shall prepare for them, and I will do to morrow as the king hath said.
kama ikikupendeza mfalme, kwa kunipa haja yangu na kuheshimu ombi langu, wewe na Hamani muhudhurie tena katika karamu nitakayoiandaa kesho na hapo ndipo nitakapo kuambia haja yangu.
9 Then went Haman forth that day joyful and with a glad heart: but when Haman saw Mordecai in the king’s gate, that he stood not up, nor trembled before him, he was full of indignation against Mordecai.
Hamani akaenda nyumbani kwakwe huku akiwa amejawa na furaha moyoni mwake. Lakini alipomwona Modekai katika lango la mfalme, modekai hasimami wala kutetemeka mbele zake, alijawa na ghadhabu kwa ajili ya Modekai.
10 Nevertheless Haman restrained himself: and when he came home, he sent and called for his friends, and Zeresh his wife.
Lakini akajizuia na akaenda nyumbani kwake. Akawaarika marafiki zake wakakusanyika pamoja na Zereshi, mkewe.
11 And Haman told them of the glory of his riches, and the multitude of his children, and all the things in which the king had promoted him, and how he had advanced him above the princes and servants of the king.
Hamani akawaeleza juu ya utukufu wa mali na idadi ya watoto aliokuwa nao, na vile alivyo juu kuliko wasimamizi na watumishi wote wa mfalme.
12 Haman said moreover, Yea, Esther the queen let no man come in with the king to the banquet that she had prepared but myself; and to morrow I am invited to her also with the king.
Hamani akawambia, “Hata jana Malkia Esta aliandaa karamu kwa ajili ya mfalme na ni mimi tu na mfalme tulio hudhuria katika karamu aliyoiandaa Malkia Esta. Na hata kesho tuna mwaliko mwingine pamoja na mfalme.
13 Yet all this availeth me nothing, so long as I see Mordecai the Jew sitting at the king’s gate.
Lakini haya yote sio kitu kama Modekai ataendelea kukaa katika lango la mfalme.
14 Then said Zeresh his wife and all his friends to him, Let a gallows be made fifty cubits high, and to morrow speak thou to the king that Mordecai may be hanged on it: then go thou in merrily with the king to the banquet. And the thing pleased Haman; and he caused the gallows to be made.
Kisha Zereshi, mkewe Hamani akamwambia Mmewe na rafiki zake wote, “Andaeni mti wenye urefu wa futi hamsini. Na wakati wa ahsubuhi ongea na mfalme ili Modekai atundikwe katika mti huo. Kisha nenda kwa furaha na mfalme katika karamu aliyoiandaa Malkia.

< Esther 5 >