< Esther 4 >

1 When Mordecai perceived all that was done, Mordecai tore his clothes, and put on sackcloth with ashes, and went out into the midst of the city, and cried with a loud and a bitter cry;
Modeka aliposikia kilichokuwa kimepangwa dhidi yao, alirarua mavazi yake na kuvaa maguni na majivu. Akaenda katikati mwa mji na kulia kwa sauti na uchungu mwingi.
2 And came even before the king’s gate: for none might enter into the king’s gate clothed with sackcloth.
Akaenda hadi langoni mwa mfalme; kwa sababu hakuna aliye ruhusiwa kuingia akiwa amevaa magunia.
3 And in every province, wherever the king’s commandment and his decree came, there was great mourning among the Jews, and fasting, and weeping, and wailing; and many lay in sackcloth and ashes.
Amri hii ilipofika katika kila jimbo, kulikuwa na kilio kikubwa kwa Wayahudi, na kufunga, kulia na maombolezo. Wengi wao walilala katika magunia na majivu.
4 So Esther’s maids and her chamberlains came and told it to her. Then was the queen exceedingly grieved; and she sent raiment to clothe Mordecai, and to take away his sackcloth from him: but he accepted it not.
Malkia Esta alipopata habari kutoka kwa wahudumu wake, alipatwa na majonzi. Akatuma watu wampelekee nguo Modekai ili avue magunia na kuvaa nguo nzuri, lakini Modekai hakukubali.
5 Then called Esther for Hatach, one of the king’s chamberlains, whom he had appointed to attend upon her, and gave him a commandment to Mordecai, to learn what it was, and why it was.
kisha Esta akamwita Hathaki, mmoja wa wasimamizi wa mfalme, ambaye alikuwa amepewa wajibu wa kumuhudumia. Akamwagiza kwenda kwa Modekai ili afahamu kwa nini Modekai ameamua kufanya hivyo.
6 So Hatach went forth to Mordecai to the street of the city, which was before the king’s gate.
Hivyo Hathaki akaenda kwa Modekai katika mji mbele ya lango la mfalme.
7 And Mordecai told him all that had happened to him, and of the sum of the money that Haman had promised to pay to the king’s treasuries for the Jews, to destroy them.
Modekai akamweleza Hathaki mambo yote kuhusu maangamizi ya Wayahudi yaliyo pangwa na kiasi cha fedha ambacho Hamani ameahidi kuwapa wahazini wa mfalme, ili kuwaua Wayahudi.
8 Also he gave him the copy of the writing of the decree that was given at Shushan to destroy them, to show it to Esther, and to tell it to her, and to charge her that she should go in to the king, to make supplication to him, and to make request before him for her people.
Na kisha akampa nakala ya mbiu ambayo ilitolewa Shushani kwa uangamivu wa Wayahudi. Alifanya hiivyo ili kwamba Hathaki amwambie Esta achukue jukumu la kwenda na kumuomba mfalme na kumsihi kwa niaba ya Wayahudi.
9 And Hatach came and told Esther the words of Mordecai.
Hivyo, Hathaki akaenda na kumweleza Esta kile alicho ambiwa na Modekai.
10 Again Esther spoke to Hatach, and gave him commandment to Mordecai;
Esta akaongea na Hathaki na akamwambia arudi kwa Modekai.
11 All the king’s servants, and the people of the king’s provinces, do know, that whoever, whether man or woman, shall come to the king into the inner court, who is not called, there is one law of his to put him to death, except him to whom the king shall hold out the golden sceptre, that he may live: but I have not been called to come in to the king these thirty days.
Esta akamwambia Hathaki, “Watumishi wote wa mfalme na watu wote katika majimbo yote wanafahamu kuwa mtu yeyote aingiae kwa mfalme bila kibali anapaswa kufa isipokuwa yule ambaye mfalme atamunyoshea fimbo yake ya dhahabu. Ni siku thelathini sasa sijaenda mbele ya mfalme.
12 And they told to Mordecai Esther’s words.
Hathaki akamwambia Modekai maneno aliyoambiwa na Esta.
13 Then Mordecai commanded to answer Esther, Think not with thyself that thou shalt escape in the king’s house, more than all the Jews.
Modekai akarudisha ujumbe: “usifikiri kwamba wewe utasalimika kuliko Wayahudi wote.
14 For if thou shalt altogether hold thy peace at this time, then shall there relief and deliverance arise to the Jews from another place; but thou and thy father’s house shall be destroyed: and who knoweth whether thou hast come to the kingdom for such a time as this?
Kama ukikaa kimya kwa wakati huu, Mungu ataleta wokovu kwa njia nyingine, lakini wewe na nyumba ya baba yako mtaangamia. Ni nani ajuaye umekuja katika nafasi hii kwa wakati muafaka kama huu.
15 Then Esther told them return Mordecai this answer,
Kisha Esta akatuma ujumbe kwa Modekai,
16 Go, gather all the Jews that are present in Shushan, and fast ye for me, and neither eat nor drink three days, night or day: I also and my maidens will fast likewise; and so will I go in to the king, which is not according to the law: and if I perish, I perish.
“Nenda, uwakusanyea Wayahudi wote wanaoishi katika mji wa Shushani, na wafunge kwa ajili yangu. Wasile wala kunywa kwa muda wa siku tatu. Mimi na watumishi watumishi wangu wa kike tutafunga kwa siku hizo. Na kisha nitaenda mbele ya mfalme kinyume cha sheria. Na kama nitakufa na nife.
17 So Mordecai went his way, and did according to all that Esther had commanded him.
Modekai akaenda na akafanya yote ambayo Esta aliyo mwagiza kufanya.

< Esther 4 >