< 1 Kings 7 >

1 But Solomon was building his own house thirteen years, and he finished all his house.
Ilimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake.
2 He built also the house of the forest of Lebanon; its length was an hundred cubits, and its breadth fifty cubits, and its height thirty cubits, upon four rows of cedar pillars, with cedar beams upon the pillars.
Aliijenga ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni. Urefu wake ulikuwa mita 46, na upanawake ulikuwa mita 23, na kimo chake kilikuwa mita 14. Nayo ilikuwa na safu nne ya nguzo za mierezi na mithili ya mwerezi juu ya nguzo.
3 And it was covered with cedar above upon the beams, that lay on forty five pillars, fifteen in a row.
Paa la ikulu lilikuwa la mwerezi ambalo lilikaa juu ya mihimili. Mihili hiyo ilikuwa imeshikiliwa na nguzo. Kulikuwa na mihimili arobaini na tano, ambayo ilikuwa katika safu kumi na tano.
4 And there were windows in three rows, and light was against light in three rows.
Nayo mihimili ilikuwa safu tatu, na kila dirisha lilikabili dirisha lingine katika madaraja matatu.
5 And all the doors and posts were square, with the windows: and light was against light in three rows.
Milango yote na miimo ilitengenezwa kwa mraba, na madirisha yalikuwa yakikabiliana katika madaraja matatu
6 And he made a porch of pillars; its length was fifty cubits, and its breadth thirty cubits: and the porch was before them: and the other pillars and the thick beams were before them.
Akatengeneza baraza lenye uerfu wa mita 23 na upana wa mita 14. Mbele yake kulikuwa na ukumbi ulioezekwa.
7 Then he made a porch for the throne where he might judge, even the porch of judgment: and it was covered with cedar from one side of the floor to the other.
Sulemani akajenga baraza yenye kiti cha enzi ambacho alitolea hukumu ya haki. Nayo ilikuwa imeezekwa kwa mwerezi kutoka sakafu moja hadi nyingine.
8 And his house where he dwelt had another court within the porch, which was of the like work. Solomon made also an house for Pharaoh’s daughter, whom he had married, like this porch.
Nyumba ya Sulemani ambayo alikusudia kuishi, katika behewa nyingine ndani ya sehemu ya chini ya ikulu, ilitengenezwa kwa kazi hiyo hiyo. Pia alimjengea binti wa Farao nyumba kama hii, ambaye alikuwa mke wake
9 All these were of costly stones, according to the measures of hewn stones, sawed with saws, within and without, even from the foundation to the coping, and so on the outside toward the great court.
Majengo haya yalipmbwa kwa vitu vya thamaini, mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa pande zote. Mawe ya namna hii ndiyo yale yaliyotumika kuanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza.
10 And the foundation was of costly stones, even great stones, stones of ten cubits, and stones of eight cubits.
Msingi ulijengwa kwa mawe makubwa sana na ya thamani yenye urefu wa mita 3. 7 na mengine mita 4. 8.
11 And above were costly stones, after the measures of hewn stones, and cedars.
Kwa juu ilipambwa kwa, mawe ya thamani yaliyochongwa sawa sawa kwa msimeno na kwa mihimili ya mierezi.
12 And the great court all around was with three rows of hewn stones, and a row of cedar beams, both for the inner court of the house of the LORD, and for the porch of the house.
Na behewa kubwa iliyokuwa ikizunguka ikulu ilikuwa na safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi kama ilivyo kwenye baraza la ndani la hekalu la BWANA na ule ukumbi wa hekalu.
13 And king Solomon sent and brought Hiram out of Tyre.
Mfalme Sulemani alituma watu kumleta Huramu kutoka Tiro.
14 He was a widow’s son of the tribe of Naphtali, and his father was a man of Tyre, a worker in brass: and he was filled with wisdom, and understanding, and skill in working all works in brass. And he came to king Solomon, and wrought all his work.
Huramu alikuwa mwana wa mjane wa kabila ya Naftali; baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mfua shaba. Huramu alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi za kufanya kazi kubwa za shaba. Aliletwa kwa mfalme ili kufanya kazi zilizohusiana na shaba kwa mfalme.
15 For he cast two pillars of brass, each of eighteen cubits high: and a line of twelve cubits did surround each of them.
Huramu alizilemba zile nguzo mbili za shaba, kila moja ilikuwa na kimo cha mita 8. 3 na mzingo wa mita 5. 5.
16 And he made two capitals of molten brass, to set upon the tops of the pillars: the height of the one capital was five cubits, and the height of the other capital was five cubits:
Akatengeneza taji mbili za shaba za kuwekwa juu ya zile nguzo. Kimo cha kila taji ilikuwa mita 2. 3.
17 And nets of checker work, and wreaths of chain work, for the capitals which were upon the top of the pillars; seven for the one capital, and seven for the other capital.
Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kazi ya kusuka, na masongo ya mikufu, kwa ajili ya kuvipamba vile vichwa vya nguzo, nayo yailikuwa saba kwa kila kichwa.
18 And he made the pillars, and two rows all around upon the one network, to cover the capitals that were upon the top, with pomegranates: and so he did for the other capital.
Kwa hiyo Huramu akafanya safu mbili za komamanga kuzunguka vile vichwa vya nguzo ili kuvipamba vile vichwa.
19 And the capitals that were upon the top of the pillars were of lily work in the porch, four cubits.
Zile taji kwenye vile vichwa vya nguzo za ukumbi zilikuwa zimepambwa kwa maua, yenye vimo vya mita 1. 8.
20 And the capitals upon the two pillars had pomegranates also above, close to the enlargement which was by the network: and the pomegranates were two hundred in rows all around upon the other capital.
Hizo taji kwenye hizo nguzo mbili kwenye vichwa vyake, karibu yake kulikuwa na makomamanga mia mbili yote yakiwa kwenye safu.
21 And he set up the pillars in the porch of the temple: and he set up the right pillar, and called its name Jachin: and he set up the left pillar, and called its name Boaz.
Alisimamisha nguzo kwenye ukumbi wa hekalu. Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini, na ile ya kushoto akaipa jina la Boazi.
22 And upon the top of the pillars was lily work: so was the work of the pillars finished.
Na juu ya zile nguzo kulikuwa na mapambo kama maua. Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa.
23 And he made a molten sea, ten cubits from the one brim to the other: it was round in form, and its height was five cubits: and a line of thirty cubits surrounded it.
Tena akafanya bahari ya kusubu ya, yenye mita 2. 3 kutoka ukingo hadi ukingo, kimo chake kilikuwa mita 4. 6, mziingo wake ulikuwa mita 13. 7.
24 And under the brim of it all around there were gourds surrounding it, ten in a cubit, all the way around the sea: the gourds were cast in two rows, when it was cast.
Na chini ya ile bahari kulikuwa na vibuyu vilivyoizunguka, vilikuwa vibuyu kumi na nane katika kila mita, vilivyowekwa katika kila hicho kipande wakati bahari inapokuwa kalibu.
25 It stood upon twelve oxen, three looking toward the north, and three looking toward the west, and three looking toward the south, and three looking toward the east: and the sea was set above upon them, and all their hinder parts were inward.
Bahari ikakaa juu ya makisai kumi na mbili, tatu, zilitazama kaskazini, tatu zikitazama magharibi, tatu zikitazama kusini na tatu zikitazama kaskazini. Ile bahari iliwekwa juu yao, na pande zao zote za nyuma zilikuwa ndani.
26 And it was an hand breadth thick, and its brim was wrought like the brim of a cup, with flowers of lilies: it contained two thousand baths.
Bahari ilikuwa nene kama upana wa mkono, na ukingo wake ulikuwakama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi huingia bathi elfu mbili za maji.
27 And he made ten bases of brass; four cubits was the length of one base, and four cubits the breadth of it, and three cubits the height of it.
Huramu akatengeneza makalio kumi ya shaba. Kila kalio lilkuwa na urefu wa mita 1. 8, upana wa mita 1. 8, na kimo cha mita 1. 3.
28 And the work of the bases was in this manner: they had borders, and the borders were between the frames:
Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa. Yalikuwa na papi ambazo zilikaa kati kati ya vipandio,
29 And on the borders that were between the frames were lions, oxen, and cherubim: and upon the frames there was a base above: and beneath the lions and oxen were certain additions made of thin work.
na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi. Chini na juu simba kulikuwa na masongo ya kazi ya kufuliwa.
30 And every base had four brasen wheels, and axles of brass: and its four corners had supports: under the laver were molten supports at the side of every addition.
Kila kalio lilikuwa na magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne na miguu yake minne ilikuwa na mataruma chini ya birika. Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo katika kila upande.
31 And the mouth of it within the capital and above was a cubit: but the mouth of it was round after the work of the base, a cubit and an half: and also upon the mouth of it were carvings with their borders, foursquare, not round.
Na kinywa chake kilikuwa cha kuviringana, chenye upana wa sentimita araobaini na sita, na ile taji ilikuwa na sentimita ishirini na tatu. Na kinywa chake kilikuwa na nakshi, na papi zake zilikuwa za mraba, na wala siyo za mvringo.
32 And under the borders were four wheels; and the axles of the wheels were joined to the base: and the height of a wheel was a cubit and half a cubit.
Yale magurudumu mawili yalikuwa chini ya papi, na mikono ya magurudumu yalikuwa ndani ya makalio. Kimo cha yale magurudumu kilikuwa sentimeta sitini na tisa.
33 And the work of the wheels was like the work of a chariot wheel: their axles, and their hubs, and their rims, and their spokes, were all cast.
Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari. Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani vyote vilikuwa vya kusubu.
34 And there were four supports to the four corners of one base: and the supports were of the very base itself.
Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makalio, yaliyokuwa yameshikamanishwa na kalio lenyewe.
35 And in the top of the base it was perfectly round at a height of half a cubit: and on the top of the base its frames and its borders were of the same.
Juu ya makalio kulikuwa na duara yenye kina cha sentimita ishirini na tatu, na juu ya makalio mashikio yake na papi zake zikiwa zimeshikamanishwa.
36 For on the plates of its frames, and on its borders, he engraved cherubim, lions, and palm trees, according to the proportion of every one, and additions all around.
Juu ya mabamba na papi zake Huramu akachora makerubi, simba, na mitende ambayo ilifunika nafasi ya juu, nayo ilikuwa imezungukwa na masongo.
37 After this manner he made the ten bases: all of them had one casting, one measure, and one size.
Alitengeneza makalio kumi kwa jinsi hii. Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana, na yalikuwa ya vipimo sawa, na sura inayofanana.
38 Then he made ten lavers of brass: one laver contained forty baths: and every laver was four cubits: and upon every one of the ten bases one laver.
Huramu akatengeneza birika kumi za shaba. Birika moja liliweza kubeba bathi arobaini za maji. Kila birika lilikuwa mita 1. 8 toka birika moja hadi jingine na kulikuwa na birika moja katika kila kalio kati ya yale kumi.
39 And he put five bases on the right side of the house, and five on the left side of the house: and he set the sea on the right side of the house eastward toward the south.
Alitengeneza makalio tano upande wa kusini unaoelekea upande wa hekalu. Akatengeneza bahari katika upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu.
40 And Hiram made the lavers, and the shovels, and the basins. So Hiram finished doing all the work that he made for king Solomon for the house of the LORD:
Huramu akatengeneza birika na koleo na besini la kunyunyizia. Kisha akamaliza kazi yote aliyofanya kwa mfalme Sulemani katika hekalu la BWANA:
41 The two pillars, and the two bowls of the capitals that were on the top of the two pillars; and the two networks, to cover the two bowls of the capitals which were upon the top of the pillars;
Zile nguzo mbili, na lile besini lakawa kama taji ambalo lilikuwa juu ya zile nguzo, na nyavu mbili za mapambo za kufunika zile besini mbili za kuwa kama taji zilizokuwa juu ya nguzo.
42 And four hundred pomegranates for the two networks, even two rows of pomegranates for one network, to cover the two bowls of the capitals that were upon the pillars;
Kisha akatengeneza makomamanga mia nne kwa ajili ya zile nyavu mbili za mapambo: safu mbili za makomamamanga kwa kila kazi ya nyavu kwa ajili ya kufunikia zile besini mbili kama taji iliyo juu ya nguzo,
43 And the ten bases, and ten lavers on the bases;
yale makalio kumi, na birika kumi kwenye makalio.
44 And one sea, and twelve oxen under the sea;
Akatengeneza bahari na makisai kumi chini yake;
45 And the pots, and the shovels, and the basins: and all these vessels, which Hiram made to king Solomon for the house of the LORD, were of bright brass.
na masufuria, koleo, birika na vyombo vingine vyote. Huramu akivitengeneza kwa shaba iliyosuguliwa, kwa ajili ya mfalme Sulemani, na kawa ajili ya hekalu la BWANA.
46 In the plain of Jordan did the king cast them, in the clay ground between Succoth and Zarthan.
Mfalme alivisubu katika uwanda wa Yorodani, katika udongo mfinyanzi kati ya Sukoti na Zarethani.
47 And Solomon left all the vessels unweighed, because they were very many: neither was the weight of the brass known.
Sulemani hakuvipima vyombo vyote kwa sababu vilikuwa vingi mno kuvipima, na kwa sababu uzito wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa.
48 And Solomon made all the vessels that pertained to the house of the LORD: the altar of gold, and the table of gold, upon which was the showbread,
Sulemani akatengeneza mapambo yote yaliyokuwa kwenye hekalu la BWANA kwa kutumia dhahabu: Ile madhabahu ya dhahabu na ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho.
49 And the lampstands of pure gold, five on the right side, and five on the left, before the inner sanctuary, with the flowers, and the lamps, and the tongs of gold,
Vile vinara vya dhahabu, ambavyo vitano vilikuwa upande wa kulia na vitano mkono wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani, vilikuwa vya dhahabu safi, na maua, na taa na koleo zilikuwa za dhahabu.
50 And the bowls, and the snuffers, and the basins, and the spoons, and the censers of pure gold; and the hinges of gold, both for the doors of the inner house, the most holy place, and for the doors of the house, that is, of the temple.
Vile vikombe, na makasi, mabakuri, na vijiko, na vyetezo vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi. na bawaba za dhahabu za milango ya ndani, ambazoo ndio mahali patakatifu sana, na milango ya ukumbi mkubwa, vyote vilitengenezwa kwa dhahabu.
51 So was ended all the work that king Solomon made for the house of the LORD. And Solomon brought in the things which David his father had dedicated; even the silver, and the gold, and the vessels, he placed among the treasures of the house of the LORD.
Kwa njia hii, kazi yote ambayo mfalme Sulemani alifanya kwa ajili ya hekalu ilimalizika. Kwa Sulemani akaviingiza ndani yake vitu vile vilivyokuwa vimewekwa wakfu na Daudi, baba yake, na fedha na dhahabu, na mapambo, na vile vya ndani ya hazina ya BWANA.

< 1 Kings 7 >