< Psalms 110 >

1 A psalm of David. Yahweh says to my master, “Sit at my right hand until I make your enemies your footstool.”
Yahwe humwambia bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”
2 Yahweh will hold out the scepter of your strength from Zion; rule among your enemies.
Yahwe atainyosha fimbo ya nguvu yako toka Sayuni; utawale kati ya adui zako.
3 Your people will follow you in holy garments of their own free will on the day of your power; from the womb of the dawn your youth will be to you like the dew.
Siku ile ya uweza wako watu wako watakufuata wakiwa katika mavazi matakatifu ya hiari yao wenyewe; tokea tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande.
4 Yahweh has sworn, and will not change: “You are a priest forever, after the manner of Melchizedek.”
Yahwe ameapa, na hatabadilika: “Wewe ni kuhani milele, baada ya namna ya Melkizedeki.”
5 The Lord is at your right hand. He will kill kings on the day of his anger.
Bwana yuko mkono wako wa kuume. Siku ile ya hasira yake atawaua wafalme.
6 He will judge the nations; he will fill the battlegrounds with dead bodies; he will kill the leaders in many countries.
Yeye atahukumu matifa; ataujaza uwanja wa vita kwa maiti; atawauwa viongozi kaitka nchi nyingi.
7 He will drink of the brook along the road, and then he will lift his head up high after victory.
Atakunywa maji ya kijito njiani, kisha baada ya ushindi atainua kichwa chake juu.

< Psalms 110 >