< Luke 19 >

1 Jesus entered and was passing through Jericho.
Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
2 Behold, there was a man there named Zacchaeus. He was a chief tax collector and was rich.
Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 He was trying to see who Jesus was, but could not see over the crowd, because he was small in height.
Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
4 So he ran on ahead of the people and climbed up into a sycamore tree to see him, because Jesus was about to pass that way.
Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
5 When Jesus came to the place, he looked up and said to him, “Zacchaeus, come down quickly, for today I must stay at your house.”
Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
6 So he hurried and came down and welcomed him joyfully.
Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
7 When everyone saw this, they all complained, saying, “He has gone in to visit a man who is a sinner.”
Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
8 Zacchaeus stood and said to the Lord, “Look, Lord, the half of my goods I give to the poor, and if I have cheated anyone of anything, I will restore four times the amount.”
Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
9 Jesus said to him, “Today salvation has come to this house, because he too is a son of Abraham.
Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
10 For the Son of Man came to seek and to save the people who are lost.”
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
11 As they heard these things, he continued speaking and told a parable, because he was near to Jerusalem, and they thought that the kingdom of God was about to appear immediately.
Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
12 He said therefore, “A certain nobleman went into a far country to receive for himself a kingdom and then to return.
Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
13 He called ten of his servants, and gave them ten minas, and said to them, 'Conduct business until I come back.'
Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
14 But his citizens hated him and sent a delegation after him, saying, 'We will not have this man rule over us.'
Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
15 It happened when he came back again, having received the kingdom, he commanded the servants to whom he had given the money to be called to him, that he might know what profit they had made by doing business.
Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
16 The first came before him, saying, 'Lord, your mina has made ten minas more.'
Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
17 The nobleman said to him, 'Well done, good servant. Because you were faithful in very little, you will have authority over ten cities.'
Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
18 The second came, saying, 'Your mina, lord, has made five minas.'
Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
19 The nobleman said to him, 'You take charge over five cities.'
Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
20 Another came, saying, 'Lord, here is your mina, which I kept safely in a cloth,
Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
21 for I was afraid of you, because you are a demanding person. You take up what you did not put in, and you reap what you did not sow.'
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
22 The nobleman said to him, 'By your own words I will judge you, you wicked servant. You knew that I am a demanding person, that I take up what I did not put in, and that I reaped what I did not sow.
Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
23 Then why did you not put my money in the bank, so that when I returned I would have collected it with interest?'
Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
24 The nobleman said to them that stood by, 'Take away from him the mina, and give it to him that has the ten minas.'
Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
25 They said to him, 'Lord, he has ten minas.'
Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
26 'I say to you, that everyone who has will be given more, but from him that has not, even that which he has will be taken away.
'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 But these enemies of mine, those who did not want me to reign over them, bring them here and kill them before me.'”
Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
28 When he had said these things, he went on ahead, going up to Jerusalem.
Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
29 It came about that when he came near to Bethphage and Bethany, to the hill that is called Olivet, he sent two of the disciples,
Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 saying, “Go into the next village. As you enter, you will find a colt that has never been ridden. Untie it and bring it to me.
akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
31 If anyone asks you, 'Why are you untying it?' say, 'The Lord has need of it.'”
Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
32 Those who were sent went and found the colt just as Jesus had told them.
Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 As they were untying the colt, the owners said to them, “Why are you untying the colt?”
Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
34 They said, “The Lord has need of it.”
Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
35 They brought it to Jesus, and they threw their cloaks upon the colt and set Jesus on it.
Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
36 As he went, they spread their cloaks on the road.
Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 As he was now approaching the place where the Mount of Olives descends, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the mighty works which they had seen,
Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
38 saying, “Blessed is the king who comes in the name of the Lord! Peace in heaven and glory in the highest!”
wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
39 Some of the Pharisees in the multitude said to him, “Teacher, rebuke your disciples.”
Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
40 Jesus answered and said, “I tell you, if these were silent, the stones would cry out.”
Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
41 When Jesus approached the city, he wept over it,
Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
42 saying, “If only you had known in this day, even you, the things which bring you peace! But now they are hidden from your eyes.
akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 For the days will come upon you when your enemies will build a barricade around you, and surround you, and press in on you from every side.
Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
44 They will strike you down to the ground and your children with you. They will not leave one stone upon another, because you did not recognize it when God was trying to save you.”
Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
45 Jesus entered the temple and began to cast out those who were selling,
Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
46 saying to them, “It is written, 'My house will be a house of prayer,' but you have made it a den of robbers.”
akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
47 So Jesus was teaching daily in the temple. The chief priests and the scribes and the leaders of the people wanted to kill him,
Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
48 but they could not find a way to do it, because all the people were listening to him intently.
lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.

< Luke 19 >