< Romans 13 >

1 Let every soule submit him selfe vnto the auctorite of ye hyer powers. For there is no power but of God.
Kila mtu anapaswa kuwatii wenye mamlaka katika serikali; maana mamlaka yote hutoka kwa Mungu; nao wenye mamlaka wamewekwa na Mungu.
2 The powers that be are ordeyned of God. Whosoever therfore resysteth power resisteth the ordinaunce of God. And they that resist shall receave to the selfe damnacio.
Anayepinga mamlaka ya viongozi anapinga agizo la Mungu; nao wafanyao hivyo wanajiletea hukumu wenyewe,
3 For rulars are not to be feared for good workes but for evyll Wilt thou be with out feare of the power? Do well then: and so shalt thou be praysed of the same.
Maana, watawala hawasababishi hofu kwa watu wema, ila kwa watu wabaya. Basi, wataka usimwogope mtu mwenye mamlaka? Fanya mema naye atakusifu;
4 For he is the minister of God for thy welth. But and yf thou do evyll then feare: for he beareth not a swearde for nought: but is the minister of God to take vengeaunce on them that do evyll.
maana yeye ni mtumishi wa Mungu anayefanya kazi kwa faida yako. Lakini ukifanya mabaya, basi, huna budi kumwogopa, maana anao kweli uwezo wa kutoa adhabu. Yeye ni mtumishi wa Mungu na huitekeleza ghadhabu ya Mungu kwao watendao maovu.
5 Wherfore ye must nedes obeye not for feare of vengeaunce only: but also because of conscience.
Kwa hiyo ni lazima kuwatii wenye mamlaka, si tu kwa sababu ya kuogopa ghadhabu ya Mungu, bali pia kwa sababu dhamiri inadai hivyo.
6 And even for this cause paye ye tribute. For they are goddes ministers servynge for the same purpose.
Kwa sababu hiyohiyo ninyi hulipa kodi; maana viongozi hao humtumikia Mungu ikiwa wanatimiza wajibu wao.
7 Geve to every man therfore his duetie: Tribute to whom tribute belongeth: Custome to whom custome is due: feare to whom feare belongeth: Honoure to who honoure pertayneth
Mpeni kila mtu haki yake; mtu wa ushuru, ushuru; wa kodi, kodi; na astahiliye heshima, heshima.
8 Owe nothinge to eny man: but to love one another. For he that loveth another fulfylleth the lawe.
Msiwe na deni kwa mtu yeyote, isipokuwa tu deni la kupendana. Ampendaye jirani yake ameitekeleza Sheria.
9 For these commaundementes: Thou shalt not comit advoutry: Thou shalt not kyll: Thou shalt not steale: Thou shalt not beare false witnes: Thou shalt not desyre and so forth (yf there be eny other comaundement) they are all comprehended in this sayinge: Love thyne neghbour as thy selfe.
Maana, amri hizi: “Usizini; Usiue; Usitamani;” na nyingine zote, zimo katika amri hii moja: “Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
10 Love hurteth not his neghbour. Therfore is love the fulfillynge of the lawe.
Ampendaye jirani yake hamtendei vibaya. Basi, kwa mapendo Sheria yote hutimizwa.
11 This also we knowe I mean the season howe that it is tyme that we shuld now awake oute of slepe. For now is oure salvacion nearer then when we beleved.
Zaidi ya hayo, ninyi mnajua tumo katika wakati gani: sasa ndio wakati wa kuamka usingizini; naam, wokovu wetu u karibu zaidi sasa kuliko wakati ule tulipoanza kuamini.
12 The nyght is passed and the daye is come nye. Let us therfore cast awaye the dedes of darcknes and let vs put on the (Armoure) of lyght.
Usiku unakwisha na mchana unakaribia. Basi, tutupilie mbali mambo yote ya giza, tukajitwalie silaha za mwanga.
13 Let vs walke honestly as it were in the daye lyght: not in eatynge and drinkynge: nether in chamburynge and wantannes: nether in stryfe and envyinge:
Mwenendo wetu uwe wa adabu kama inavyostahili wakati wa mchana; tusiwe na ulafi na ulevi, uchafu na uasherati, ugomvi na wivu.
14 but put ye on the Lorde Iesus Christ. And make not provision for the flesshe to fulfyll ye lustes of it.
Bwana Yesu Kristo awe vazi lenu; msishughulikie tena tamaa zenu za maumbile na kuziridhisha.

< Romans 13 >