< Revelation 7 >

1 And after that I sawe. iiii. angels stonde on the iiii. corners of ye erth holdynge ye iiii. wyndes of the erth that ye wyndes shulde not blowe on the erthe nether on the see nether on eny tree.
Baada ya hayo nikawaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za dunia wakishika pepo nne za dunia ili upepo usivume hata kidogo: wala katika nchi, wala baharini, wala kwenye miti.
2 And I sawe another angell ascende from the rysynge of the sunne: which had the seale of the lyvynge god and he cryed with a loude voyce to the iiii angelles (to whom power was geven to hurt the erth and the see)
Kisha nikamwona malaika mwingine akipanda juu kutoka mashariki akiwa na mhuri wa Mungu aliye hai. Akapaaza sauti na kuwaambia hao malaika wanne waliokabidhiwa jukumu la kuiharibu nchi na bahari,
3 saying: Hurt not the erth nether the see nether the trees tyll we have sealed ye servauntes of oure god in their forheddes.
“Msiharibu nchi, wala bahari, wala miti, mpaka tutakapokwisha wapiga mhuri watumishi wa Mungu wetu katika paji la uso.”
4 And I herde the nombre of them which were sealed and there were sealed an C. and xliiii. M. of all the trybes of the chyldren of Israhell.
Kisha nikasikia idadi ya hao waliopigwa mhuri: Watu mia moja arobaini na nne elfu wa makabila yote ya watu wa Israeli.
5 Of the trybe of Iuda were sealed xii. M Of the trybe of Ruben were sealed xii. M. of the trybe of Gad were sealed xii. M.
Kabila la Yuda walikuwa watu kumi na mbili elfu; kabila la Reubeni, kumi na mbili elfu, kabila la Gadi, kumi na mbili elfu;
6 Of the trybe of Asser were sealed xii. M. Of the trybe of Neptalym were sealed xii. M. Of the trybe of Manasses were sealed xii. M.
Kabila la Asheri, kumi na mbili elfu; kabila la Naftali, kumi na mbili elfu; kabila la Manase, kumi na mbili elfu;
7 Of ye trybe of Symeo were sealed xii. M. Of ye tribe of Leuy were sealed xii. M. Of ye trybe of Isacar were sealed xii. M.
kabila la Simeoni, kumi na mbili elfu, kabila la Lawi, kumi na mbili elfu, kabila la Isakari, kumi na mbili elfu;
8 Of the trybe of zabulon weee sealed xii. M. Of the tribe of Ioseph were sealed xii. M. Of the trybe of Beniamin were sealed xii. thowsande.
kabila la Zabuloni, kumi na mbili elfu; kabila la Yosefu, kumi na mbili elfu, na kabila la Benyamini, kumi na mbili elfu.
9 After this I behelde and lo a gret multitude (which noma coulde nombre) of all nacios and people and tonges stode before the seate and before the lambe clothed with longe whyte garmentes and palmes in there hondes
Kisha nikatazama, nikaona umati mkubwa wa watu wasiohesabika: watu wa kila taifa, ukoo, jamaa na lugha. Nao walikuwa wamesimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwanakondoo, wakiwa wamevaa mavazi meupe na kushika matawi ya mitende mikononi mwao.
10 and cryed with a lowde voyce sayinge: salvacion be asscribed to him that syttith apon the seate of oure god and vnto the lambe.
Wakapaaza sauti: “Ukombozi wetu watoka kwa Mungu wetu aketiye juu ya kiti cha enzi, na kutoka kwa Mwanakondoo!”
11 And all the angelles stode in the compase of the seate and of the elders and of the iiii. bestes and fel before the seat on their faces and worshipped god
Malaika wote wakasimama kukizunguka kiti cha enzi, wazee na vile viumbe hai vinne. Wakaanguka kifudifudi mbele ya kiti cha enzi, wakamwabudu Mungu,
12 sayinge amen: Blessynge and glory wisdome and thankes and honour and power and myght be vnto oure god for evermore Amen. (aiōn g165)
wakisema, “Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukrani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu, milele na milele! Amina!” (aiōn g165)
13 And one of the elders answered sayinge vnto me: what are these which are arayed in longe whyte garmentes and whence cam they?
Mmoja wa hao wazee akaniuliza, “Hawa waliovaa mavazi meupe ni watu gani? Na wametoka wapi?”
14 And I sayde vnto him: lorde thou wottest. And he sayde vnto me: these are they which cam oute of gret tribulacion and made their garmetes large and made them whyte in the bloud of the lambe:
Nami nikamjibu, “Mheshimiwa, wewe wajua!” Naye akaniambia, “Hawa ni wale waliopita salama katika ule udhalimu mkuu. Waliyaosha mavazi yao katika damu ya Mwanakondoo, yakawa meupe kabisa.
15 therfore are they in the presence of the seate of God and serve him daye and nyght in hys temple and he that sytteth in the seate wyll dwell amonge them.
Ndiyo maana wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Humtumikia Mungu mchana na usiku katika Hekalu lake; naye aketiye juu ya kiti cha enzi atatandaza hema lake juu yao kuwalinda.
16 They shalt honger no more nether thyrst nether shall the sunne lyght on them nether eny heate:
Hawataona tena njaa wala kiu; jua wala joto kali halitawachoma tena,
17 For the lambe which ys in the myddes of the seate shall fede them and shall ledde them vnto fountaynes of lyuynge water and god shall wype awaye all teares from their eyes.
kwa sababu Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchungaji wao, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji ya uzima. Naye Mungu atayafuta machozi yote machoni mwao.”

< Revelation 7 >