< Revelation 5 >

1 And I sawe in the right honde of him that sat in ye trone a boke written with in and on the backside sealyd with vii. seales.
Kisha katika mkono wa kulia wa huyo aliyeketi juu ya kiti cha enzi, nikaona kitabu; nacho kilikuwa kimeandikwa ndani na nje na kufungwa na mihuri saba.
2 And I sawe a stronge angell which cryed with a loude voyce: Who is worthy to open the boke and to loose the seales therof.
Tena nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: “Nani anayestahili kuvunja hiyo mihuri na kukifungua kitabu hicho?”
3 And no man in heven ner in erth nether vnder the erth was able to open the boke nether to loke thereon.
Lakini hakupatikana mtu yeyote mbinguni, wala duniani, wala chini Kuzimu, aliyeweza kukifungua hicho kitabu au kukitazama ndani. (questioned)
4 And I wepte moche because no man was founde worthy to open and to rede the boke nether to loke thereon.
Basi, mimi nikalia sana kwa sababu hakupatikana mtu aliyestahili kukifungua, au kukitazama ndani.
5 And one of the elders sayde unto me: wepe not: Beholde a lion beinge of the tribe of Iuda the rote of Dauid hath obtayned to open the boke and to lose the vii. seales therof.
Kisha mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama! Simba wa kabila la Yuda, mjukuu maarufu wa Daudi, ameshinda. Yeye anaweza kuivunja mihuri yake saba na kukifungua hicho kitabu.”
6 And I behelde and loo in the myddes of the seate and of the. iiii. bestes and in the myddes of the elders stode a lambe as though he had bene kylled which had vii. hornes and vii. eyes which are the spretes of God sent into all the worlde.
Kisha nikaona pale katikati ya kiti cha enzi Mwana kondoo amesimama, akizungukwa kila upande na vile viumbe hai vinne, na wale wazee. Huyo Mwanakondoo alionekana kana kwamba amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba ambayo ni roho saba za Mungu zilizokuwa zimepelekwa kila mahali duniani.
7 And he cam and toke the boke oute of the right honde of him that sate apon the seate.
Mwanakondoo akaenda, akakitwaa hicho kitabu kutoka mkono wa kulia wa yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi.
8 And when he had take the boke the. iiii. bestes and xxiiii. elders fell doune before the labe havynge harpes and golden vialles full of odoures which are the prayers of saynctes
Mara tu alipokwisha twaa hicho kitabu, vile viumbe hai vinne pamoja na wale wazee ishirini na wanne walianguka kifudifudi mbele ya Mwanakondoo. Kila mmoja, alikuwa na kinubi na bakuli za dhahabu zilizojaa ubani, ambao ni sala za watu wa Mungu.
9 and they songe a newe songe saynge: thou art worthy to take ye boke and to ope ye seales therof: for thou waste kylled and haste redemed vs by thy bloud out of all kynreddes and tonges and people and nacions
Basi, wakaimba wimbo huu mpya: “Wewe unastahili kukitwaa hicho kitabu na kuivunja mihuri yake. Kwa sababu wewe umechinjwa, na kwa damu yako umemnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
10 and haste made vs vnto oure god kynges and prestes and we shall raygne on the erth.
Wewe umewafanya wawe ufalme wa makuhani wamtumikie Mungu wetu nao watatawala duniani.”
11 And I behelde and I herd the voyce of many angylles aboute the trone and about the bestes and the elders and I herde thousand thousandes
Kisha nikatazama, nikasikia sauti ya malaika wengi sana, idadi isiyohesabika, maelfu na maelfu. Walikuwa wamekaa kuzunguka kiti cha enzi, vile viumbe hai vinne na wale wazee;
12 saynge wt a lowde voyce: Worthy is the lambe that was killed to receave power and riches and wisdom and strenghte and honoure and glory and blyssynge.
wakasema kwa sauti kuu: “Mwanakondoo aliyechinjwa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, utukufu na sifa.”
13 And all creatures which are in heven and on the erth and vnder the erth and in the see and all that are in them herd I sayinge: blyssinge honour glory and power be vnto hym that sytteth apon the seate and vnto the lambe for ever more. (aiōn g165)
Nikasikia viumbe vyote mbinguni, duniani, chini kuzimuni na baharini—viumbe vyote ulimwenguni—vikisema: “Kwake yeye aketiye katika kiti cha enzi, na kwa Mwanakondoo, iwe sifa na heshima na utukufu na enzi milele na milele.” (aiōn g165, questioned)
14 And the. iiii. bestes sayd: Ame. And the. xxiiii. elders fell apon their faces and worshypped him that lyveth for ever more.
Na vile viumbe vinne hai vikasema, “Amina!” Na wale wazee wakaanguka kifudifudi, wakaabudu.

< Revelation 5 >