< Revelation 22 +

1 And he shewed me a pure ryver of water of lyfe clere as cristall: procedynge oute of the seate of God and of the lambe.
Kisha malaika akanionyesha mto wa maji ya uzima maangavu kama kioo yakitoka kwenye kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo.
2 In the myddes of the strete of it and of ether syde of ye ryver was there wode of lyfe: which bare xii maner of frutes: and gave frute every moneth: and the leves of the wodde served to heale the people with all.
Mto huo ulitiririka kupitia katikati ya barabara kuu ya mji. Kandokando ya mto huo kulikuwa na mti wa uzima unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa.
3 And there shalbe no more cursse but the seate of god and the lambe shalbe in it: and his servauntes shall serve him:
Hapana kitu chochote kilicholaaniwa kitakachokuwa katika mji huo. Kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwanakondoo kitakuwa katika mji huo, na watumishi wake watamwabudu.
4 And shall se his face and his name shalbe in their forheddes.
Watauona uso wake, na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.
5 And there shall be no nyght there and they nede no candle nether light of the sunne: for the lorde God geveth them light and they shall raygne for evermore. (aiōn g165)
Usiku hautakuwako tena, wala hawatahitaji mwanga wa taa au wa jua, maana Bwana Mungu atawaangazia, nao watatawala milele na milele. (aiōn g165)
6 And he sayde vnto me: these sayinges are faythfull and true. And the lorde god of saynctes and prophetes sent his angell to shewe vnto his servauntes the thynges which muste shortly be fulfylled.
Kisha malaika akaniambia, “Maneno haya ni ya kweli na ya kuaminika. Bwana Mungu ambaye huwapa manabii Roho wake, alimtuma malaika wake awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo lazima yatukie punde.
7 Beholde I come shortly. Happy is he that kepeth the sayinge of ye prophesy of this boke.
“Sikiliza! Naja upesi. Heri yake anayeyazingatia maneno ya unabii yaliyo katika kitabu hiki.”
8 I am Ihon which sawe these thynges and herde them. And when I had herde and sene I fell doune to worshippe before the fete of the angell which shewed me these thynges.
Mimi Yohane, niliyaona na kusikia mambo haya. Nilipokwisha sikia na kuona nikajitupa chini mbele ya miguu ya huyo malaika aliyenionyesha mambo hayo, nikataka kumwabudu.
9 And he sayd vnto me: se thou do it not for I am thy feloweservaunt and the feloweservaunt of thy brethren the prophettes and of them which kepe the sayinges of this boke. But worshippe God.
Lakini yeye akaniambia, “Acha! Mimi ni mtumishi tu kama wewe na ndugu zako manabii na wote wanaoyatii maagizo yaliyomo katika kitabu hiki. Mwabudu Mungu!”
10 And he sayde vnto me: seale not the sayinges of prophesy of this boke. For the tyme is at honde.
Tena akaniambia, “Usiyafiche kama siri maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, maana wakati wa kutimizwa kwake umekaribia.
11 He that doeth evyl let him do evyl still: and he which is fylthy let him be fylthy still: and he that is righteous let him be more righteous: and he that is holy let him be more holy.
Kwa sasa anayetenda mabaya na aendelee kutenda mabaya, na aliye mchafu aendelee kuwa mchafu. Mwenye kutenda mema na azidi kutenda mema, na aliye mtakatifu na azidi kuwa mtakatifu.”
12 And beholde I come shortly and my rewarde with me to geve every man accordinge as his dedes shalbe.
“Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi, pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
13 I am Alpha and Omega the begynninge and the ende: the fyrst and the last.
Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho, wa kwanza na wa mwisho.”
14 Blessed are they that do hys commaundmentes that their power maye be in the tree of lyfe and maye entre in thorow the gates into the cite.
Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, kwani watakuwa na haki ya kula tunda la mti wa uzima, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake.
15 For without shalbe dogges and inchauters and whormongers and mortherers and ydolaters and whosoever loveth or makith lesynges.
Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.
16 I Iesus sent myne angell to testyfye vnto you these thynges in the congregacions. I am the rote and the generacion of David and the bright mornynge starre.
“Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!”
17 And the sprete and the bryde sayde come. And let him that heareth saye also come. And let him that is athyrst come. And let whosoever wyll take of the water of lyfe fre.
Roho na Bibiarusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Kisha, yeyote aliye na kiu na aje; anayetaka maji ya uzima na apokee bila malipo yoyote.
18 I testifye vnto every man that heareth the wordes of prophesy of thys boke. yf eny man shall adde vnto these thynges god shall adde vnto him the plages that are wrytten in this boke.
Mimi Yohane nawapa onyo wote wanaosikia maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki: mtu yeyote akiongeza chochote katika mambo haya, Mungu atamwongezea mabaa yaliyoandikwa katika kitabu hiki.
19 And yf eny man shall mynyshe of the wordes of ye boke of this prophesy god shall take a waye his parte out of the boke of lyfe and oute of ye holy citie and fro thoo thynge which are written in this boke.
Na mtu yeyote akipunguza chochote katika maneno ya unabii yaliyomo katika kitabu hiki, Mungu atamnyang'anya sehemu yake katika ule mti wa uzima, na sehemu yake katika mji mtakatifu, ambavyo vimeelezwa katika kitabu hiki.
20 He which testifyeth these thinges sayth: be it I come quyckly Amen. Even soo: come lorde Iesu.
Naye anayetoa ushahidi wake juu ya mambo haya asema: “Naam! Naja upesi.” Amina. Na iwe hivyo! Njoo Bwana Yesu!
21 The grace of oure lorde Iesu Christ be with you all. Amen.
Nawatakieni nyote neema ya Bwana Yesu. Amen.

< Revelation 22 +