< Revelation 18 >

1 And after that I sawe another angell come from heven havinge gret power and the erth was lyghtned with hys bryghtnes.
Baada ya vitu hivi nilimwona malaika mwingine akishuka chini kutoka mbinguni. Yeye alikuwa na mamlaka kuu, na nchi iliangazwa kwa utukufu wake.
2 And he cryed myghtyly with a stronge voyce sayinge: Great Babilon is fallen ys fallen and ys become the habitation of devels and the holde of all fowle sprettes and a cage of all vnclene and hatefull byrdes
Alilia kwa sauti kuu, akisema, “Umeanguka, umeanguka, ule mji mkuu Babeli! Umekuwa sehemu yakaapo mapepo, na sehemu ikaapo kila roho chafu, na sehemu akaapo kila mchafu na ndege achukizaye.
3 for all nacions have dronken of the wyne of the wrath of her fornycacion. And the kynges of the erth have committed fornicacion with her and her marchauntes are wexed ryche of the abundance of her pleasures.
Kwa kuwa mataifa yote yamekunywa mvinyo ya tamaa ya uasherati wake ambayo humletea ghadhabu. Wafalme wa nchi wamezini naye. Wafanyabiashara wa nchi wamekuwa matajiri kwa nguvu ya maisha yake ya anasa.”
4 And I herde another voyce from heven saye: come a waye from her my people that ye be not parttakers in her synnes that ye receave not of her plages.
Kisha nilisikia sauti nyingine kutoka mbinguni iikisema, “Tokeni kwake watu wangu, ili msije mkashiriki katika dhambi zake, na ili msije mkapokea mapigo yake yoyote.
5 For her synnes are gon vp to heven and God hath remembred her wyckednes.
Dhambi zake zimerundikana juu kama mbingu, na Mungu ameyakumbuka matendo yake maovu.
6 Rewarde her even as she rewarded you and geve her dubble accordynge to her workes. And poure in dubble to her in the same cuppe which she fylled vnto you.
Mlipeni kama alivyowalipa wengine, na mkamlipe mara mbili kwa jinsi alivyotenda; katika kikombe alichokichanganya, mchanganyishieni mara mbili kwa ajili yake.
7 And as moche as she gloryfied her silfe and lyved wantanly so moche poure ye in for her of punysshment and sorowe for she sayde in her herte: I sytt beinge a quene and am no wyddowe and shall se no sorowe.
Kama alivyojitukuza yeye mwenyewe, na aliishi kwa anasa, mpeni mateso mengi na huzuni. Kwa kuwa husema moyoni mwake, 'Nimekaa kama malkia; wala siyo mjane, na wala sitaona maombolezo.'
8 Therfore shall her plages come at one daye deeth and sorowe and honger and she shallbe brent with fyre: for stronge ys the lorde god which iudgeth her.
Kwa hiyo ndani ya siku moja mapigo yake yatamlemea: kifo, maombolezo, na njaa. Atateketezwa kwa moto, kwa kuwa Bwana Mungu ni mwenye nguvu, na ni mhukumu wake.”
9 And the kynges of the erth shalbe wepe her and wayle over her which have committed fornicacion with her and have lyved wantanly with her when they shall se the smoke of her burnynge
Wafalme wa nchi waliozini na kuchanganyikiwa pamoja naye watalia na kumwombolezea watakapouona moshi wa kuungua kwake.
10 and shall stonde a farre of for feare of her punnysshment sayinge: Alas Alas that gret cite Babilon that myghty cite: For at won houre is her iudgment come.
Watasimama mbali naye, kwa hofu ya maumivu yake wakisema, “Ole, ole kwa mji mkuu, Babeli, mji wenye nguvu! Kwa saa moja hukumu yako imekuja.”
11 And the marchauntes of the erth shall wepe and wayle in them selves for no man wyll bye their ware eny more
Wafanyabiashara wa nchi lieni na kuomboleza kwa ajili yake, kwa kuwa hakuna hata mmoja anunuaye bidhaa zake tena -
12 the ware of golde and silver and precious stones nether of pearle and raynes and purple and skarlet and all thyne wodde and almanner vessels of yvery and almanner vessels of most precious wodde and of brasse and of yron
bidhaa za dhahabu, fedha, mawe ya thamani, lulu, kitani nzuri, zambarau, hariri, nyekundu, aina zote za miti ya harufu nzuri, kila chombo cha pembe za ndovu, kila chombo kilichotengenezwa kwa miti ya thamani, shaba, chuma, jiwe,
13 and synamon and odours and oyntmentes and frankynsence and wyne and oyle and fyne floure and wheate bestes and shepe and horsys and charrettes and boddyes and soules of men.
mdalasini, viungo, uvumba, manemane, ubani, mvinyo, mafuta, unga mzuri, ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari, na watumwa, na roho za watu.
14 And the apples that thy soule lusted after are departed fro the. And all thynges which were deyntie and had in pryce ar departed fro the and thou shalt fynde them no more.
Matunda uliyoyatamani kwa nguvu zako yameondoka kutoka kwako. Anasa zako zote na mapambo yametoweka, hayatapatikana tena.
15 The marchauntes of these thynges which were wexed ryche shall stonde a farre of from her for feare of the punyshment of her wepynge and waylynge
Wafanyabiashara wa vitu hivi waliopata utajiri kwa mapenzi yake watasimama mbali kutoka kwake kwa sababu ya hofu ya maumivu yake, wakilia na sauti ya maombolezo.
16 and saying: alas alas that grett cite that was clothed in raynes and purple and scarlett and decked with golde and precious stone and pearles:
Wakisema, “Ole, ole mji ule mkuu uliovikwa kitani nzuri, zambarau, na nyekundu, na kupambwa kwa dhahabu, na vito vya thamani na lulu!”
17 for at one houre so great ryches ys come to nought And every shippe governer and all they that occupied shippes and shippmen which worke in the see stode a farre of
Ndani ya saa moja utajiri wote huo ulitoweka. Kila nahodha wa meli, kila baharia, na wote wanamaji, na wote wafanyao kazi baharini, walisimama mbali.
18 and cryed when they sawe the smoke of her burnynge sayinge what cite is lyke vnto this grett cite?
Walilia walipouona moshi wa kuungua kwake. Walisema, “Ni mji gani unafanana na mji huu mkubwa?”
19 And they cast dust on their heddes and cryed wepynge and waylinge and sayed: Alas Alas yt greate cite wherin were made ryche all that had shyppes in the see by the reason of her costlynes for atone houre is she made desolate
Walitupa mavumbi juu ya vichwa vyao, na walilia, wakitokwa machozi na kuomboleza, “Ole, ole mji mkubwa mahali wote waliokuwa na meli zao baharini walikuwa matajiri kutokana na mali zake. Ndani ya saa moja umeangamizwa.”
20 Reioyce over her thou heven and ye holy Apostles and prophetes: for god hath geven youre iudgment on her.
“Furahini juu yake, mbingu, ninyi waumini, mitume, na manabii, kwa maana Mungu ameleta hukumu yenu juu yake!”
21 And a myghty angell toke vp a stone lyke a grett mylstone and cast it into the see sayinge: with suche violence shall that gret cite Babilon be cast and shallbe founde no more.
Malaika mwenye nguvu aliinua jiwe kama jiwe kuu la kusagia na alilitupa baharini, akisema, “Kwa njia hii, Babeli, ule mji mkuu, utatupwa chini kwa ukatili na hautaonekana tena.
22 And the voyce of harpers and musicions and of pypers and trompetters shalbe herde no more in the: and no craftes man of whatsoever craft he be shalbe founde eny more in the. and the soude of a myll shalbe herde no more in the
Sauti ya vinanda, wanamuziki, wacheza filimbi, na tarumbeta hawatasikika tena kwenu. Wala fundi wa aina yoyote hataonekana kwenu. Wala sauti ya kinu haitasikika tena kwenu.
23 and the voyce of the brydegrome and of the bryde shalbe herde no more in the: for thy marchauntes were ye grett men of ye erth. And with thyne inchantment were deceaved all nacions:
Mwanga wa taa hautaangaza ndani yako. Sauti ya bwana harusi na bibi harusi hazitasikiwa tena ndani yako, maana wafanyabiashara wako walikuwa wakuu wa nchi, na wa mataifa, wamedanganywa kwa uchawi wako.
24 and in her was founde the bloude of the prophettes and of ye saynctes and of all that were slayne apon ye erth.
Ndani yake damu ya manabii na waamini ilionekana, na damu ya wote waliouawa juu ya nchi.”

< Revelation 18 >