< Luke 8 >

1 And it fortuned after that that he him sylfe went throughout cities and tounes preachynge and shewinge ye kyngdom of God and the twelve with him.
Baada ya hayo, Yesu alipitia katika miji na vijiji akitangaza Habari Njema za Ufalme wa Mungu. Wale kumi na wawili waliandamana naye.
2 And also certayne wemen which wer healed of evell spretes and infirmities: Mary called Magdalen out of whom went seven devyls
Pia wanawake kadhaa ambao Yesu alikuwa amewatoa pepo wabaya na kuwaponya magonjwa, waliandamana naye. Hao ndio akina Maria (aitwaye Magdalene), ambaye alitolewa pepo wabaya saba;
3 and Ioanna ye wyfe of Chusa Herodees stewarde and Susanna and many other: which ministred vnto the of their substaunce.
Yoana, mke wa Kuza, mfanyakazi mkuu wa Herode; Susana na wengine kadhaa. Hao wanawake walikuwa wakiwatumikia kwa mali yao wenyewe.
4 When moch people were gadred to gether and were come to him out of all cities he spake by a similitude.
Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu:
5 A sower went out to sowe his seede: and as he sowed some fell by the waye syde and it was troden vnder fete and the foules of the ayre devoured it vp.
“Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
6 And some fell on ston and assone as it was spronge vp it widdred awaye because it lacked moystnes.
Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji.
7 And some fell amonge thornes and ye thornes spronge vp with it and choked it.
Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.
8 And some fell on good grounde and sproge vp and bare frute an hondred foolde. And as he sayde these thinges he cryed: He that hath eares to heare let him heare.
Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia.” Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, “Mwenye masikio na asikie!”
9 And his disciples axed him sayinge: what maner similitude is this?
Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
10 And he sayde: vnto you is it geven to knowe the secretes of the kyngdom of God: but to other in similitudes that when they se they shuld not se: and when they heare they shuld not vnderstonde.
Naye akajibu, “Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
11 The similitude is this. The seede is ye worde of God.
“Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.
12 Thoose yt are besyde the waye are they that heare and afterwarde cometh ye devyll and taketh awaye the worde out of their hertes lest they shuld beleve and be saved.
Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.
13 They on the stonnes are they which when they heare receave the worde with ioye. But these have noo rootes which for a whyle beleve and in tyme of temtacio goo awaye.
Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.
14 And yt which fell amonge thornes are they which heare and goo forth and are choked wt cares and wt riches and volupteous lyvinge and bringe forth noo frute.
Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.
15 That in ye good grounde are they which with a good and pure hert heare the worde and kepe it and bringe forth frute with pacience.
Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.
16 No man lyghteth a candell and covereth it vnder a vessell nether putteth it vnder ye table: but setteth it on a candelsticke that they that enter in maye se ye lyght.
“Watu hawawashi taa na kuifunika kwa chombo au kuiweka mvunguni. Lakini huiweka juu ya kinara ili watu wanapoingia ndani wapate kuona mwanga.
17 No thinge is in secret yt shall not come abroode: Nether eny thinge hyd that shall not be knowen and come to lyght.
“Chochote kilichofichwa kitafichuliwa na siri yoyote itagunduliwa na kujulikana hadharani.
18 Take hede therfore how ye heare. For whosoever hath to him shalbe geve: And whosoever hath not fro him shalbe take even that same which he supposeth that he hath.
“Kwa hiyo, jihadharini jinsi mnavyosikia; maana aliye na kitu ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani kuwa anacho, kitachukuliwa.”
19 Then came to him his mother and his brethren and coulde not come at him for prease.
Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
20 And they tolde him sayinge: Thy mother and thy brethren stonde with out and wolde se the.
Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.
21 He answered and sayd vnto them: my mother and my brethren are these which heare the worde of God and do it.
Lakini Yesu akawaambia watu wote, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika.”
22 And it chaunsed on a certayne daye that he went into a shippe and his disciples also and he sayde vnto them: Let vs goo over vnto the other syde of the lake. And they Lanched forthe.
Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvuke ziwa twende mpaka ng'ambo.” Basi, wakaanza safari.
23 And as they sayled he fell a slepe and there arose a storme of wynde in ye lake and they were fylled with water and were in ieopardy.
Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.
24 And they went to him and awoke him sayinge: Master Master we are loost. Then he arose and rebuked the wynde and the tempest of water and they ceased and it wexed calme.
Wale wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwamsha wakisema, “Bwana, Bwana! Tunaangamia!” Yesu akaamka, akaikemea dhoruba na mawimbi, navyo vikatulia, kukawa shwari.
25 And he sayd vnto the: where is youre faith? They feared and wondred sayinge one to another: what felowe is this? for he comaundeth bothe the wyndes and water and they obey him?
Kisha akawaambia, “Iko wapi imani yenu?” Lakini wao walishangaa na kuogopa huku wakiambiana, “Huyu ni nani basi, hata anaamuru dhoruba na mawimbi, navyo vinamtii?”
26 And they sayled vnto the region of ye Gaderenites which is over agaynst Galile.
Wakaendelea na safari, wakafika pwani ya nchi ya Wagerase inayokabiliana na Galilaya, ng'ambo ya ziwa.
27 And as he went out to londe ther met him a certayne man out of ye cite which had a devyll longe tyme and ware noo clothes nether aboode in eny housse: but amonge graves.
Alipokuwa anashuka pwani, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo alimjia kutoka mjini. Kwa muda mrefu mtu huyo, hakuwa anavaa nguo, wala hakuwa anaishi nyumbani bali makaburini.
28 When he sawe Iesus he cryed and fell doune before him and with a loude voyce sayde: What have I to do with the Iesus the sonne of the God moost hyest? I beseche the torment me not.
Alipomwona Yesu, alipiga kelele na kujitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa “We, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu una shauri gani nami? Ninakusihi usinitese!”
29 Then he comaunded ye foule sprete to come out of the man. For ofte tymes he caught him and he was bounde with chaynes and kept with fetters: and he brake the bondes and was caryed of the fende into wyldernes.
Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikwishamwambia huyo pepo mchafu amtoke mtu huyo. Pepo huyo mchafu alikuwa anamvamia mtu huyo mara nyingi, na ingawa watu walimweka ndani na kumfunga kwa minyororo na pingu, lakini kila mara alivivunja vifungo hivyo, akakimbizwa na pepo huyo mchafu hadi jangwani.
30 And Iesus axed him sayinge: what is thy name? And he sayde: Legion because many devyls were entred into him.
Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Yeye akajibu, “Jina langu ni Jeshi” —kwa sababu pepo wengi walikuwa wamempagaa.
31 And they besought him yt he wolde not comaunde the to goo out into ye depe. (Abyssos g12)
Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
32 And ther was there by an heerde of many swyne fedynge on an hyll: and they besought him yt he wolde soffre the to enter into the. And he soffred the.
Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani. Basi, hao pepo wakamsihi awaruhusu wawaingie. Naye Yesu akawapa ruhusa.
33 Then went the devyls out of the man and entred into the swyne: And the heerd toke their course and ran heedlynge into the lake and were choked.
Kwa hiyo pepo hao wakamtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nao wakaporomoka kwenye ule mteremko mkali, wakatumbukia ziwani, wakazama majini.
34 When the herdmen sawe what had chaunsed they fleed and tolde it in the cite and in the villages.
Wale wachungaji walipoona yote yaliyotokea walikimbia, wakaenda kuwapa watu habari, mjini na mashambani.
35 And they came out to se what was done: and came to Iesus and founde ye man out of who the devyls were departed sittynge at the fete of Iesus clothed and in his right mynde and they were afrayde.
Watu wakaja kuona yaliyotokea. Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo ameketi karibu na Yesu, amevaa nguo, ana akili zake, wakaogopa.
36 They also wich sawe it tolde the by what meanes he yt was possessed of ye devyll was healed.
Wale watu walioshuhudia tukio hilo waliwaeleza hao jinsi yule mtu alivyoponywa.
37 And all the whole multitude of ye cotrye of the Gaderenites besought him yt he wolde departe from the: for they were taken wt greate feare. And he gate him into the shippe and returned backe agayne.
Wakazi wa nchi ya Gerase walishikwa na hofu kubwa. Kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke, aende zake. Hivyo Yesu alipanda tena mashua, akaondoka.
38 Then the man out of whom the devyls were departed besought him yt he myght be wt him: But Iesus sent him awaye sayinge:
Yule mtu aliyetokwa na wale pepo akamsihi aende pamoja naye. Lakini Yesu hakumruhusu, bali akamwambia,
39 Goo home agayne into thyne awne housse and shewe what great thinges God hath done to ye. And he went his waye and preached thorow out all the cite what great thinges Iesus had done vnto him.
“Rudi nyumbani ukaeleze yote Mungu aliyokutendea.” Basi, yule mtu akaenda akitangaza kila mahali katika mji ule mambo yote Yesu aliyomtendea.
40 And it fortuned when Iesus was come agayne that ye people receaved him. For they all wayted for him.
Yesu aliporudi upande mwingine wa ziwa, kundi la watu lilimkaribisha, kwa maana wote walikuwa wanamngojea.
41 And beholde ther came a man named Iairus (and he was a ruler of ye synagoge) and he fell doune at Iesus fete and besought him yt he wolde come into his housse
Hapo akaja mtu mmoja aitwaye Yairo, ofisa wa sunagogi. Alijitupa miguuni pa Yesu, akamwomba aende nyumbani kwake,
42 for he had but a doughter only apon a twelve yere of age and she laye a dyinge. And as he went the people thronged him.
kwa kuwa binti yake wa pekee, mwana wa pekee mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa mahututi. Yesu alipokuwa akienda, watu wakawa wanamsonga kila upande.
43 And a woman havynge an issue of bloud twelve yeres (which had spent all her substance amonge phisicios nether coulde be holpen of eny)
Kulikuwa na mwanamke mmoja kati ya lile kundi la watu, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote kwa waganga, hakuna aliyefaulu kumponya.
44 came behinde him and touched the hem of his garmet and immediatly her issue of bloud staunched.
Huyo mwanamke alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake. Papo hapo akaponywa ugonjwa wake wa kutokwa damu.
45 And Iesus sayde: Who is it that touched me? when every man denyed Peter and they yt were with him sayde: Master the people thrust the and vexe the: and sayest thou who touched me?
Yesu akasema, “Ni nani aliyenigusa?” Wote wakasema kwamba hapakuwa na mtu aliyemgusa. Naye Petro akasema, “Mwalimu, umati wa watu umekuzunguka na kukusonga!”
46 And Iesus sayd: Some body touched me. For I perceave that vertue is gone out of me.
Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, maana nimehisi nguvu imenitoka.”
47 When the woman sawe that she was not hid she came trimblynge and fell at is fete and tolde him before all the people for what cause she had touched him and how she was healed immediatly.
Yule mwanamke alipoona kwamba hawezi kujificha, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa mbele ya Yesu. Hapo akaeleza mbele ya wote kisa cha kumgusa Yesu na jinsi alivyoponyeshwa mara moja.
48 And he sayde vnto hyr: Doughter be of good comforte Thy faith hath made the hoale goo in peace.
Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
49 Whyll he yet spake there came one from ye rulers of the synagogis housse which sayde to him: thy doughter is deed disease not the master.
Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: “Binti yako ameshakufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?”
50 When Iesus hearde that He answered the father sayinge: Feare not beleve only and she shalbe made whole.
Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, “Usiogope; amini tu, naye atapona.”
51 And when he came to ye housse he suffred no man to goo in with him save Peter Iames and Iohn and the father and the mother of the mayden.
Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.
52 Every body weept and sorowed for her. And he sayde: Wepe not: for she is not deed but slepeth.
Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, “Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!”
53 And they lewgh him to scorne. For they knew that she was deed.
Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
54 And he thrust the all out and caught her by the honde and cryed sayinge: Mayde aryse.
Lakini Yesu akamshika mkono akasema, “Mtoto amka!”
55 And hyr sprete came agayne and she roose strayght waye. And he commaunded to geve her meate.
Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
56 And the father and the mother of hyr were astonyed. But he warned the that they shuld tell noo man what was done.
Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.

< Luke 8 >