< Luke 8 >

1 And it fortuned after that that he him sylfe went throughout cities and tounes preachynge and shewinge ye kyngdom of God and the twelve with him.
Ilitokea muda mfupi baadaye kwamba Yesu alianza kusafiri katika miji na jiji mbalimbali, akihubiri na kutangaza habari njema ya ufalme wa Mungu na wale kumi wawili walikwenda pamoja naye,
2 And also certayne wemen which wer healed of evell spretes and infirmities: Mary called Magdalen out of whom went seven devyls
vilevile wanawake fulani waliokuwa wameponywa kutoka kwa roho wachafu na magonjwa mbalimbali. Walikuwa ni Mariamu aliyeitwa Magdalena ambaye alikuwa ametolewa pepo saba.
3 and Ioanna ye wyfe of Chusa Herodees stewarde and Susanna and many other: which ministred vnto the of their substaunce.
Yoana mke wa Kuza na meneja wa Herode, Susana, na wanawake wengine wengi, waliotoa mali vyao kwa ajili yao wenyewe.
4 When moch people were gadred to gether and were come to him out of all cities he spake by a similitude.
Nabaada ya umati wa watu kukusanyika pamoja, wakiwemo na watu waliokuja kwake kutoka miji mbalimbali, akazungumza nao kwa kutumia mifano.
5 A sower went out to sowe his seede: and as he sowed some fell by the waye syde and it was troden vnder fete and the foules of the ayre devoured it vp.
“mpandaji alienda kupanda mbegu, alipokuwa apanda, baadhi ya mbegu hizo ziliangukia kando ya njia zikakanyagwa chini ya miguu, na ndege wa angani wakazila.
6 And some fell on ston and assone as it was spronge vp it widdred awaye because it lacked moystnes.
Mbegu zingine zilianguka juu ya udongo wa miamba na zilipoota na kuwa miche zilipooza kwa sababu hakukuwa na unyevunyevu.
7 And some fell amonge thornes and ye thornes spronge vp with it and choked it.
Mbegu zingine ziliangukia kwenye miti ya miiba, nayo hiyo miti ya miiba ikakua pamoja na zile mbegu na zikasongwa.
8 And some fell on good grounde and sproge vp and bare frute an hondred foolde. And as he sayde these thinges he cryed: He that hath eares to heare let him heare.
Lakini mbegu zingine ziliangukia kwenye udongo unaofaa na zikazaa mazao mara mia zaidi. “Baada ya Yesu kusema mambo haya, alipaza sauti,”Yeyote aliye na masikio ya kusikia na asikie.”
9 And his disciples axed him sayinge: what maner similitude is this?
Tena wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo,
10 And he sayde: vnto you is it geven to knowe the secretes of the kyngdom of God: but to other in similitudes that when they se they shuld not se: and when they heare they shuld not vnderstonde.
Yesu akawaambia, “Mmepewa upendeleo wa kujua siri ya ufalme wa Mungu, lakini watu wengine watafundishwa tu kwa mifano, ili kwamba 'wakiona wasione na wakisikia wasielewe.'
11 The similitude is this. The seede is ye worde of God.
Na hii ndiyo maana ya mfano huu. Mbegu ni neno la Mungu.
12 Thoose yt are besyde the waye are they that heare and afterwarde cometh ye devyll and taketh awaye the worde out of their hertes lest they shuld beleve and be saved.
Mbegu zile zilizoanguka kando kando ya njia ndiyo wale watu wanaolisikia neno, na baadaye mwovu shetani hulichukua mbali kutoka moyoni, ili kwamba wasiamini na kuokolewa.
13 They on the stonnes are they which when they heare receave the worde with ioye. But these have noo rootes which for a whyle beleve and in tyme of temtacio goo awaye.
Kisha na zile zilizoangukia kwenye mwamba ni watu wale wanaosikia neno na kulipokea kwa furaha lakini hawana mizizi yeyote, wanaamini tu kwa muda mfupi, na wakati wa majaribu huanguka.
14 And yt which fell amonge thornes are they which heare and goo forth and are choked wt cares and wt riches and volupteous lyvinge and bringe forth noo frute.
Na mbegu zile zilizoangukia kwenye miiba ni watu wanaosikia neno, lakini wanapoendelea kukua husongwa na huduma na utajiri na ubora wa maisha haya na hawazai matunda.
15 That in ye good grounde are they which with a good and pure hert heare the worde and kepe it and bringe forth frute with pacience.
Lakini zile mbegu zilizoangukia kwenye udongo mzuri ni wale watu, ambao ni wanyeyekevu na mioyo mizuri, baada ya kulisikia neno hulishikilia na likawa salama na kuazaa matunda ya uvumilivu.
16 No man lyghteth a candell and covereth it vnder a vessell nether putteth it vnder ye table: but setteth it on a candelsticke that they that enter in maye se ye lyght.
Sasa, hakuna hata mmoja, anayewasha taa na kuifunika kwa bakuli au kuiweka chini ya kitanda. Badala ya kuiweka kwenye kinara cha taa ili kwamba kila mmoja anayeingia apate kuiona.
17 No thinge is in secret yt shall not come abroode: Nether eny thinge hyd that shall not be knowen and come to lyght.
Kwa kuwa hakuna kitakachojificha ambacho hakitajulikana, au chochote kilicho sirini ambacho hakitajulikana kikiwa kwenye mwanga.
18 Take hede therfore how ye heare. For whosoever hath to him shalbe geve: And whosoever hath not fro him shalbe take even that same which he supposeth that he hath.
kwa hiyo kuwa makini unapokuwa unasikiliza. Kwa sababu aliye nacho, kwake ataongezewa zaidi, lakini asiye nacho hata kile kidogo alicho nacho kitachukuliwa.”
19 Then came to him his mother and his brethren and coulde not come at him for prease.
baadaye mama yake Yesu na ndugu zake wakaja kwake hawakaribia kwa sababu ya umati wa watu.
20 And they tolde him sayinge: Thy mother and thy brethren stonde with out and wolde se the.
Na akataarifiwa, “Mama yako na ndugu zako wako pale nje wanahitaji kukuona wewe.
21 He answered and sayd vnto them: my mother and my brethren are these which heare the worde of God and do it.
Lakini, Yesu akajibu akasema “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulitii.”
22 And it chaunsed on a certayne daye that he went into a shippe and his disciples also and he sayde vnto them: Let vs goo over vnto the other syde of the lake. And they Lanched forthe.
Ilitokea siku moja kati ya siku zile Yesu na wanafunzi wake alipanda kwenye mtumbwi, na akawaambia, “Na tuvuke ng'ambo ya pili ya ziwa.” Wakaandaa mashua yao.
23 And as they sayled he fell a slepe and there arose a storme of wynde in ye lake and they were fylled with water and were in ieopardy.
Lakini walipoanza kuondoka, Yesu akalala usingizi, na dhoruba kali yenye upepo, na mashua yao ikaanza kujaa maji na walikuwa kwenye katika kubwa sana.
24 And they went to him and awoke him sayinge: Master Master we are loost. Then he arose and rebuked the wynde and the tempest of water and they ceased and it wexed calme.
baadaye wanafunzi wake wakaja kwake na kumwamsha, wakisema, “Bwana mkubwa! Bwana mkubwa! tuko karibu kufa!” Akaamka na akaukemea upepo na mawimbi ya maji vikatulia na kukawa na utulivu.
25 And he sayd vnto the: where is youre faith? They feared and wondred sayinge one to another: what felowe is this? for he comaundeth bothe the wyndes and water and they obey him?
Tena akawaambia, “Imani yenu iko wapi?” Wakaogopa, Walishangaa, wakasemezana kia mmoja na mwenzake,”Huyu ni nani, kiasi kwamba anaamuru hata upepo, na maji na humtii?”
26 And they sayled vnto the region of ye Gaderenites which is over agaynst Galile.
Wakafika kwenye mji wa Gerasini iliyo upande wa nyuma ya Galilaya.
27 And as he went out to londe ther met him a certayne man out of ye cite which had a devyll longe tyme and ware noo clothes nether aboode in eny housse: but amonge graves.
Yesu aliposhuka na kukanya kwenye ardhi, mtu fulani kutoka mjini, akakutana naye, na huyu mtu alikuwa na nguvu za giza. Kwa muda mrefu alikuwa havai nguo, na alikuwa haishi kwenye Nyumba, lakini aliishi kwenye makaburi.
28 When he sawe Iesus he cryed and fell doune before him and with a loude voyce sayde: What have I to do with the Iesus the sonne of the God moost hyest? I beseche the torment me not.
Alipomwona Yesu akalia kwa sauti, na akaanguka chini mbele yake. kwa sauti kubwa akisema, Nimefanya nini kwako, Yesu mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi, Usiniadhibu mimi”
29 Then he comaunded ye foule sprete to come out of the man. For ofte tymes he caught him and he was bounde with chaynes and kept with fetters: and he brake the bondes and was caryed of the fende into wyldernes.
Yesu akaamuru roho chafu imtoke mtu yule, kwa kuwa mara nyingi amepamgaa. hata kama alikuwa amefungwa minyororo na kubanwa na kuwekwa chini ya ulinzi, alivunja vifungo na kuendeshwa na mapepo mpaka jangwani.
30 And Iesus axed him sayinge: what is thy name? And he sayde: Legion because many devyls were entred into him.
Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” akajibu akisema, “Legioni” Kwa maana mapepo mengi yameingia kwake.
31 And they besought him yt he wolde not comaunde the to goo out into ye depe. (Abyssos g12)
Wakaendelea kumsihi usituamuru twende kwenye shimo. (Abyssos g12)
32 And ther was there by an heerde of many swyne fedynge on an hyll: and they besought him yt he wolde soffre the to enter into the. And he soffred the.
Kundi la Nguruwe lilikuwa likichunga juu ya kilima, wakamsihi awaruhusu wakaingie kwa hao nguruwe. Na akawaruhusu kufanya hivyo.
33 Then went the devyls out of the man and entred into the swyne: And the heerd toke their course and ran heedlynge into the lake and were choked.
kwa hiyo wale mapepo wakamtoka mtu yule na kuingia kwa wale nguruwe, na lile kundi likakimbia kwenye mwinuko wa mlima mpaka ziwani na wakazama humo.
34 When the herdmen sawe what had chaunsed they fleed and tolde it in the cite and in the villages.
wale watu waliokuwa wanachunga wale nguruwe walipoona kilichotokea, wakakimbia na wakatoa taarifa pale mjini na nje katika miji iliyowazunguka.
35 And they came out to se what was done: and came to Iesus and founde ye man out of who the devyls were departed sittynge at the fete of Iesus clothed and in his right mynde and they were afrayde.
Watu waliposikia hayo walienda kuona kilichotokea, na wakaja kwa Yesu na wakamwona mtu ambaye mapepo yalikuwa yamemtoka. alikuwa amevaa vizuri na mwenye akili timamu, amekaa kwenye miguu ya Yesu, na waliogopa.
36 They also wich sawe it tolde the by what meanes he yt was possessed of ye devyll was healed.
ndipo mmoja wao aliyeona kilichotokea alianza kuwasimlia wengine jinsi huyu mtu aliyekuwa anaongozwa na mapepo alivyoponywa.
37 And all the whole multitude of ye cotrye of the Gaderenites besought him yt he wolde departe from the: for they were taken wt greate feare. And he gate him into the shippe and returned backe agayne.
Watu wote wa mkoa wa Wagerasi na maeneo yaliyozunguka walimwomba Yesu aondoke kwao kwa sababu walikuwa na hofu kuu. Na aliingia kwenye mtumbwi ili arudi.
38 Then the man out of whom the devyls were departed besought him yt he myght be wt him: But Iesus sent him awaye sayinge:
Mtu yule aliyetokwa na pepo alimsihi Yesu kwenda naye, lakini Yesu alimwambia aende na kusema,
39 Goo home agayne into thyne awne housse and shewe what great thinges God hath done to ye. And he went his waye and preached thorow out all the cite what great thinges Iesus had done vnto him.
“Rudi kwenye nyumba yako na uhesabu yale yote ambayo Mungu amekutendea” Huyu mtu aliondoka, akitangaza pote katika mji wote yale yote ambayo Yesu aliyofanya kwa ajili yake.
40 And it fortuned when Iesus was come agayne that ye people receaved him. For they all wayted for him.
Na Yesu akarudi, makutano wakamkaribisha, kwa sababu wote walikuwa wanamngoja.
41 And beholde ther came a man named Iairus (and he was a ruler of ye synagoge) and he fell doune at Iesus fete and besought him yt he wolde come into his housse
Tazama akaja mtu mmoja anaitwa Yairo ni mmoja kati ya viongozi katika sinagogi. Yairo akaanguka miguuni pa Yesu na kumsihi aende nyumbani kwake,
42 for he had but a doughter only apon a twelve yere of age and she laye a dyinge. And as he went the people thronged him.
kwa sababu alikuwa na mtoto msichana mmoja tu, mwenye umri wa miaka kumi na wibili, na alikuwa katika hali ya kufa. Na alipokuwa akienda, makutano walikuwa wakisongama dhidi yake.
43 And a woman havynge an issue of bloud twelve yeres (which had spent all her substance amonge phisicios nether coulde be holpen of eny)
Mwanamke mwenye kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili alikuwa pale na alitumia pesa zote kwa waganga, lakini hakuna aliyemponya hata mmoja,
44 came behinde him and touched the hem of his garmet and immediatly her issue of bloud staunched.
alikuja nyuma ya yesu na kugusa pindo la vazi lake, na ghafla kutokwa damu kukakoma.
45 And Iesus sayde: Who is it that touched me? when every man denyed Peter and they yt were with him sayde: Master the people thrust the and vexe the: and sayest thou who touched me?
Yesu akasema, “Nani ambaye kanigusa?” Walipokataa wote, Petro akasema, Bwana Mkubwa, umati wa watu wanakusukuma na wanakusonga.”
46 And Iesus sayd: Some body touched me. For I perceave that vertue is gone out of me.
Lakini Yesu akasema, “Mtu mmoja alinigusa, maana nilijua nguvu zimetoka kwangu.”
47 When the woman sawe that she was not hid she came trimblynge and fell at is fete and tolde him before all the people for what cause she had touched him and how she was healed immediatly.
Mwanamke alipoona ya kuwa hawezi kuficha alichokifanya, akaanza kutetemeka, akaanguka chini mbele za Yesu alitangaza mbele ya watu wote sababu zilizofanya amguse na vile alivyoponywa gafla.
48 And he sayde vnto hyr: Doughter be of good comforte Thy faith hath made the hoale goo in peace.
Kisha akasema kwake, “Binti, imani yako imekufanya uwe mzima. Enenda kwa Amani.”
49 Whyll he yet spake there came one from ye rulers of the synagogis housse which sayde to him: thy doughter is deed disease not the master.
Alipokuwa akiendelea kusema, mtu mmoja akaja kutoka kwenye nyumba ya kiongozi wa sinagogi, akisema, “Binti yako amefariki. Usimsumbue mwalimu.”
50 When Iesus hearde that He answered the father sayinge: Feare not beleve only and she shalbe made whole.
Lakini Yesu aliposikia hivyo, alimjibu, “Usiogope. Amini tu, na ataokolewa.”
51 And when he came to ye housse he suffred no man to goo in with him save Peter Iames and Iohn and the father and the mother of the mayden.
Kisha alipoingia kwenye hiyo nyumba, hakuruhusu mtu yeyote kuingia pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohana na Yakobo, baba yake binti, na mama yake.
52 Every body weept and sorowed for her. And he sayde: Wepe not: for she is not deed but slepeth.
Sasa watu wote walikuwa wanaomboleza na kutoa sauti kwa ajili yake, lakini akasema, “Msipige kelele, hajafa, lakini amelala tu.”
53 And they lewgh him to scorne. For they knew that she was deed.
Lakini wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekufa.
54 And he thrust the all out and caught her by the honde and cryed sayinge: Mayde aryse.
Lakini Yeye, akimshika binti mkono, akaita kwa sauti, akisema, “Mtoto, inuka”
55 And hyr sprete came agayne and she roose strayght waye. And he commaunded to geve her meate.
roho yake ikamrudia, na akainuka wakati huohuo. Akaamrisha kwamba, apewe kitu furani kwa ili ale.
56 And the father and the mother of hyr were astonyed. But he warned the that they shuld tell noo man what was done.
Wazazi wake wakashangaa, lakini aliwaamuru wasimwambie mtu kilichokuwa kimetokea.

< Luke 8 >