< Luke 8 >

1 And it fortuned after that that he him sylfe went throughout cities and tounes preachynge and shewinge ye kyngdom of God and the twelve with him.
Baada ya haya Yesu alikwenda, akawa anazunguka katika miji na vijiji akihubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walikuwa pamoja naye,
2 And also certayne wemen which wer healed of evell spretes and infirmities: Mary called Magdalen out of whom went seven devyls
pia baadhi ya wanawake waliokuwa wametolewa pepo wachafu na kuponywa magonjwa. Miongoni mwao alikuwepo Maria Magdalene, aliyetolewa pepo wachafu saba;
3 and Ioanna ye wyfe of Chusa Herodees stewarde and Susanna and many other: which ministred vnto the of their substaunce.
Yoana mkewe Kuza, msimamizi wa nyumba ya watu wa nyumbani mwa Herode; Susana; na wengine wengi waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
4 When moch people were gadred to gether and were come to him out of all cities he spake by a similitude.
Umati mkubwa wa watu ulipokuwa ukija kwa Yesu kutoka kila mji, akawaambia mfano huu:
5 A sower went out to sowe his seede: and as he sowed some fell by the waye syde and it was troden vnder fete and the foules of the ayre devoured it vp.
“Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia; zikakanyagwa, nao ndege wa angani wakazila.
6 And some fell on ston and assone as it was spronge vp it widdred awaye because it lacked moystnes.
Mbegu nyingine zilianguka penye miamba, nazo zilipoota, hiyo mimea ikakauka kwa kukosa unyevu.
7 And some fell amonge thornes and ye thornes spronge vp with it and choked it.
Nazo mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo ile miiba ikakua pamoja nazo, na kuisonga hiyo mimea.
8 And some fell on good grounde and sproge vp and bare frute an hondred foolde. And as he sayde these thinges he cryed: He that hath eares to heare let him heare.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri. Zikaota na kuzaa mara mia moja zaidi ya mbegu alizopanda.” Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti, akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
9 And his disciples axed him sayinge: what maner similitude is this?
Wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo.
10 And he sayde: vnto you is it geven to knowe the secretes of the kyngdom of God: but to other in similitudes that when they se they shuld not se: and when they heare they shuld not vnderstonde.
Naye akasema, “Ninyi mmepewa kufahamu siri za Ufalme wa Mungu, lakini kwa wengine nazungumza kwa mifano, ili, “‘ingawa wanatazama, wasione; ingawa wanasikiliza, wasielewe.’
11 The similitude is this. The seede is ye worde of God.
“Maana ya mfano huu ni hii: Mbegu ni neno la Mungu.
12 Thoose yt are besyde the waye are they that heare and afterwarde cometh ye devyll and taketh awaye the worde out of their hertes lest they shuld beleve and be saved.
Zile zilizoanguka kando ya njia ni wale ambao husikia neno, naye ibilisi anakuja na kuliondoa neno kutoka mioyoni mwao, ili wasije wakaamini na kuokoka.
13 They on the stonnes are they which when they heare receave the worde with ioye. But these have noo rootes which for a whyle beleve and in tyme of temtacio goo awaye.
Zile mbegu zilizoanguka kwenye mwamba ni wale ambao hulipokea neno kwa furaha wanapolisikia, lakini hawana mizizi. Wanaamini kwa muda mfupi, lakini wakati wa kujaribiwa huiacha imani.
14 And yt which fell amonge thornes are they which heare and goo forth and are choked wt cares and wt riches and volupteous lyvinge and bringe forth noo frute.
Zile mbegu zilizoanguka kwenye miiba ni mfano wa wale wanaosikia, lakini wanapoendelea husongwa na masumbufu ya maisha haya, utajiri na anasa, nao hawakui.
15 That in ye good grounde are they which with a good and pure hert heare the worde and kepe it and bringe forth frute with pacience.
Lakini zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo mzuri ni mfano wa wale ambao hulisikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mnyofu wa utiifu, nao kwa kuvumilia kwingi huzaa matunda.
16 No man lyghteth a candell and covereth it vnder a vessell nether putteth it vnder ye table: but setteth it on a candelsticke that they that enter in maye se ye lyght.
“Hakuna mtu awashaye taa na kuificha ndani ya gudulia au kuiweka mvunguni mwa kitanda. Badala yake, huiweka juu ya kinara, ili wale waingiao ndani waone mwanga.
17 No thinge is in secret yt shall not come abroode: Nether eny thinge hyd that shall not be knowen and come to lyght.
Kwa maana hakuna jambo lolote lililofichika ambalo halitafichuliwa, wala lolote lililositirika ambalo halitajulikana na kuwekwa wazi.
18 Take hede therfore how ye heare. For whosoever hath to him shalbe geve: And whosoever hath not fro him shalbe take even that same which he supposeth that he hath.
Kwa hiyo, kuweni waangalifu mnavyosikia. Kwa maana yeyote aliye na kitu atapewa zaidi. Lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani anacho atanyangʼanywa.”
19 Then came to him his mother and his brethren and coulde not come at him for prease.
Wakati mmoja mama yake Yesu na ndugu zake walikuja kumwona, lakini hawakuweza kumfikia kwa sababu ya msongamano wa watu.
20 And they tolde him sayinge: Thy mother and thy brethren stonde with out and wolde se the.
Mtu mmoja akamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje wanataka kukuona.”
21 He answered and sayd vnto them: my mother and my brethren are these which heare the worde of God and do it.
Yesu akamjibu, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wote wanaolisikia neno la Mungu na kulifanya.”
22 And it chaunsed on a certayne daye that he went into a shippe and his disciples also and he sayde vnto them: Let vs goo over vnto the other syde of the lake. And they Lanched forthe.
Siku moja Yesu alipanda ndani ya mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo ya ziwa.” Nao wakaondoka.
23 And as they sayled he fell a slepe and there arose a storme of wynde in ye lake and they were fylled with water and were in ieopardy.
Hivyo walipokuwa wakienda, akalala usingizi. Dhoruba kali ikatokea mle ziwani, hata mashua ikawa inajaa maji, nao walikuwa katika hatari kubwa.
24 And they went to him and awoke him sayinge: Master Master we are loost. Then he arose and rebuked the wynde and the tempest of water and they ceased and it wexed calme.
Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, Bwana, tunaangamia!” Yeye akaamka, akaukemea ule upepo na yale mawimbi; dhoruba ikakoma, nako kukawa shwari.
25 And he sayd vnto the: where is youre faith? They feared and wondred sayinge one to another: what felowe is this? for he comaundeth bothe the wyndes and water and they obey him?
Akawauliza wanafunzi wake, “Imani yenu iko wapi?” Kwa woga na mshangao wakaulizana, “Huyu ni nani, ambaye anaamuru hata upepo na maji, navyo vikamtii?”
26 And they sayled vnto the region of ye Gaderenites which is over agaynst Galile.
Basi wakafika katika nchi ya Wagerasi, ambayo iko upande wa pili wa ziwa kutoka Galilaya.
27 And as he went out to londe ther met him a certayne man out of ye cite which had a devyll longe tyme and ware noo clothes nether aboode in eny housse: but amonge graves.
Yesu aliposhuka kutoka mashua na kukanyaga ufuoni, alikutana na mtu mmoja wa mji ule aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, naye kwa muda mrefu alikuwa havai nguo wala kuishi nyumbani, bali aliishi makaburini.
28 When he sawe Iesus he cryed and fell doune before him and with a loude voyce sayde: What have I to do with the Iesus the sonne of the God moost hyest? I beseche the torment me not.
Alipomwona Yesu, alipiga kelele, akajitupa chini mbele yake na kusema kwa sauti kuu, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Nakuomba, usinitese!”
29 Then he comaunded ye foule sprete to come out of the man. For ofte tymes he caught him and he was bounde with chaynes and kept with fetters: and he brake the bondes and was caryed of the fende into wyldernes.
Wakati huo Yesu alikuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke huyo mtu. Mara nyingi huyo pepo mchafu alimpagaa, na hata alipofungwa kwa minyororo mikono na miguu na kuwekwa chini ya ulinzi, alikata hiyo minyororo na kupelekwa na huyo pepo mchafu kwenda nyikani.
30 And Iesus axed him sayinge: what is thy name? And he sayde: Legion because many devyls were entred into him.
Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Legioni,” kwa kuwa alikuwa ameingiwa na pepo wachafu wengi mno.
31 And they besought him yt he wolde not comaunde the to goo out into ye depe. (Abyssos g12)
Wale pepo wachafu wakamsihi sana asiwaamuru kwenda katika Shimo. (Abyssos g12)
32 And ther was there by an heerde of many swyne fedynge on an hyll: and they besought him yt he wolde soffre the to enter into the. And he soffred the.
Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe hapo likilisha kando ya kilima. Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu awaruhusu wawaingie hao nguruwe, naye akawaruhusu.
33 Then went the devyls out of the man and entred into the swyne: And the heerd toke their course and ran heedlynge into the lake and were choked.
Wale pepo wachafu walipomtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremkia gengeni kwa kasi, likatumbukia ziwani na kuzama.
34 When the herdmen sawe what had chaunsed they fleed and tolde it in the cite and in the villages.
Wale watu waliokuwa wakichunga lile kundi la nguruwe walipoona yaliyotukia, wakakimbia, wakaeneza habari hizi mjini na mashambani.
35 And they came out to se what was done: and came to Iesus and founde ye man out of who the devyls were departed sittynge at the fete of Iesus clothed and in his right mynde and they were afrayde.
Nao watu wakatoka kwenda kujionea wenyewe yaliyotukia. Walipofika hapo alipokuwa Yesu, wakamkuta yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu amekaa karibu na Yesu, akiwa amevaa nguo na mwenye akili timamu! Wakaogopa.
36 They also wich sawe it tolde the by what meanes he yt was possessed of ye devyll was healed.
Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine jinsi yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu alivyoponywa.
37 And all the whole multitude of ye cotrye of the Gaderenites besought him yt he wolde departe from the: for they were taken wt greate feare. And he gate him into the shippe and returned backe agayne.
Ndipo watu wote wa nchi ile ya Wagerasi wakamwomba Yesu aondoke kwao, kwa sababu walikuwa wamejawa na hofu. Basi akaingia katika mashua, akaondoka zake.
38 Then the man out of whom the devyls were departed besought him yt he myght be wt him: But Iesus sent him awaye sayinge:
Yule mtu aliyetokwa na pepo wachafu akamsihi Yesu afuatane naye, lakini Yesu akamuaga, akamwambia:
39 Goo home agayne into thyne awne housse and shewe what great thinges God hath done to ye. And he went his waye and preached thorow out all the cite what great thinges Iesus had done vnto him.
“Rudi nyumbani ukawaeleze mambo makuu Mungu aliyokutendea.” Kwa hiyo yule mtu akaenda, akatangaza katika mji wote mambo makuu ambayo Yesu alimtendea.
40 And it fortuned when Iesus was come agayne that ye people receaved him. For they all wayted for him.
Basi Yesu aliporudi, umati mkubwa wa watu ukampokea kwa furaha, kwani walikuwa wakimngojea.
41 And beholde ther came a man named Iairus (and he was a ruler of ye synagoge) and he fell doune at Iesus fete and besought him yt he wolde come into his housse
Kisha mtu mmoja, jina lake Yairo, aliyekuwa kiongozi wa sinagogi, akaja na kuanguka miguuni mwa Yesu, akimwomba afike nyumbani kwake,
42 for he had but a doughter only apon a twelve yere of age and she laye a dyinge. And as he went the people thronged him.
kwa kuwa binti yake wa pekee, mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa anakufa. Yesu alipokuwa akienda, umati wa watu ukamsonga sana.
43 And a woman havynge an issue of bloud twelve yeres (which had spent all her substance amonge phisicios nether coulde be holpen of eny)
Katika umati huo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa na tatizo la kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Tena alikuwa amegharimia yote aliyokuwa nayo kwa ajili ya matibabu, wala hakuna yeyote aliyeweza kumponya.
44 came behinde him and touched the hem of his garmet and immediatly her issue of bloud staunched.
Huyo mwanamke akaja kwa nyuma ya Yesu na kugusa upindo wa vazi lake. Mara kutokwa damu kwake kukakoma.
45 And Iesus sayde: Who is it that touched me? when every man denyed Peter and they yt were with him sayde: Master the people thrust the and vexe the: and sayest thou who touched me?
Yesu akauliza, “Ni nani aliyenigusa?” Watu wote walipokana, Petro akasema, “Bwana, huu umati wa watu unakusonga na kukusukuma kila upande.”
46 And Iesus sayd: Some body touched me. For I perceave that vertue is gone out of me.
Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, kwa maana nimetambua kuwa nguvu zimenitoka.”
47 When the woman sawe that she was not hid she came trimblynge and fell at is fete and tolde him before all the people for what cause she had touched him and how she was healed immediatly.
Yule mwanamke alipofahamu ya kuwa hawezi kuendelea kujificha, alikuja akitetemeka, akaanguka miguuni mwa Yesu. Akaeleza mbele ya watu wote kwa nini alimgusa na jinsi alivyoponywa mara.
48 And he sayde vnto hyr: Doughter be of good comforte Thy faith hath made the hoale goo in peace.
Basi Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
49 Whyll he yet spake there came one from ye rulers of the synagogis housse which sayde to him: thy doughter is deed disease not the master.
Yesu alipokuwa bado anasema, akaja mtumishi kutoka nyumbani kwa Yairo, yule kiongozi wa sinagogi, kumwambia, “Binti yako amekwisha kufa. Usiendelee kumsumbua Mwalimu.”
50 When Iesus hearde that He answered the father sayinge: Feare not beleve only and she shalbe made whole.
Yesu aliposikia jambo hili, akamwambia Yairo, “Usiogope. Amini tu, naye binti yako atapona.”
51 And when he came to ye housse he suffred no man to goo in with him save Peter Iames and Iohn and the father and the mother of the mayden.
Walipofika nyumbani kwa Yairo, hakumruhusu mtu yeyote aingie ndani naye isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, pamoja na baba na mama wa yule binti.
52 Every body weept and sorowed for her. And he sayde: Wepe not: for she is not deed but slepeth.
Wakati ule ule watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili ya huyo binti. Yesu akawaambia, “Acheni kulia. Huyu binti hajafa, ila amelala.”
53 And they lewgh him to scorne. For they knew that she was deed.
Wao wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekwisha kufa.
54 And he thrust the all out and caught her by the honde and cryed sayinge: Mayde aryse.
Yesu akamshika yule binti mkono na kuita, “Binti, amka!”
55 And hyr sprete came agayne and she roose strayght waye. And he commaunded to geve her meate.
Roho yake ikamrudia, naye akainuka mara moja. Akaamuru apewe kitu cha kula.
56 And the father and the mother of hyr were astonyed. But he warned the that they shuld tell noo man what was done.
Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote juu ya yale yaliyotukia.

< Luke 8 >